Hivi wewe umerogwaa huoni au?? umeshaambiwa wadada ni wachawi huko!!! sasa huoni hii ni Bonge ya fursa hiyo wewe??? ukifika huko sasa wewe fanya biashara ya uchawi una chukua uchawi Masasi/Lindi unapeleka kuuza Dar!! kwa bei mbaya!!
Usafiri km wa Ungo ukiupata huu tu!! hee! unatosha kabisaa kukutoa!!! Mwaka tu uko mbali!! ...usafiri ulivyo wa shida DSM wewe unatega ungo wako tu palee Salasala/Posta/kariakoo!! na wateja wako wa kudumu 60 tu!! una uhakika wa kutoka!
hakikisha unasafisha njia kwa wale waganga wanoko wa Kawe walipe kidogo kidogo wasilie njaa!! wakatungua ndege yako utakosa wateja!! Mama ntilie , wauza Magenge, Maduka hao!!! wa kule salasala watakuwa wateja wako wazuri tu!!
hivi navosema sasa, kuna watu wanapiga kazi huko!! wanapata mitaji si kawaida! km ukiona moja ya wateja ame kuwa mnoko mnoko hivi achana nae faster! yaani mpige chini! sasa wewe bado unalia lia!! lia!! tu .......fursa!!! fursa!! mfyuuuuxvc !