Nimeamua Kulima kwa mara ya Pili kilimo cha mahindi

Nimeamua Kulima kwa mara ya Pili kilimo cha mahindi

Habari wandugu, ashukuliwe Mungu kuwa tuwazima na anatupigania kwenye changamoto za maisha.
Kwa hali ya kiuchumi ilivyo kwa sasa inatubidi kutafuta miradi tofauti tofauti ili kumudu hali ya sasa. Kwa mtazamo wangu naona sasa ipo haja ya kuitumia ardhi tulio nayo kutuletea maendeleo na sio kukaa na kulalamikia hali ngumu ya maisha.
Katika hayo naombeni kujuzwa kuhusu kilimo. Cha;

1: maparachichi.
Kilimo hiki kipoje, kinahitaji hali ya hewa ya namna gani?
Ni maeneo yepi hapa nchini yanafaa kwa kilimo hiki.?
Vipi kuhusu masoko yapoje?

2:. Matikiti major:
Hapa pia naomba kujuzwa, nifanye nini ikiwa nataka kulima matikiti maji,
Changamoto zake zikoje?

3: Mahindi:
Kilimo hiki kinaonekana kudharaulika lakini kila uchao unga unapanda bei.
Hivi ni njia zipi Bora za kilimo cha mahindi?
Ni mbegu zipi ni bora zaidi kwa hapa nchini hasa kwa mkoa wa morogoro?

Kwa wale wataalamu wa kilimo naomba mnijuze hayo, naamini itasaidia wengi wenye nia kama yangu.
Natanguliza shukurani zangu kwenu.
Unaweza kunicheck kwa hii no 0715162344 naweza kukupa CBA na masterplan ya matikiti
 
Je waweza nijulisha ni mbegu gani unatumia katika kilimo cha mahindi na sifa zake! Me ni mkulima mchanga nahitaji uzoefu wenu tafadhari
Mkuu huyo aliyepata gunia 43 alitumia maji ya kumwagilia au alitegemea mvua tu?
Huyu anategemea mvua. Bado hapa nchini kuna maeneo bado mvua ni nzuri hasa za masika. Mfano mkoa wa Iringa wilaya kama mufindi. Lakini anapractise kilimo cha kisasa. Na kikubwa anacheza na afya ya udongo na technologia ya zero tillage. Lakini pia spacing yake inampa miche mingi kwa eneo.
 
Inategemea na mahali unapolima.kisiasa ni gunia 30-40.ki uhalisia ukifuata kanuni 10 za kilimo bora ni gunia 10-12.milele na milele
 
Inategemea unalimia wapi?

Kaskazini wanalima kisasa,wamesoma na wanamwomba Mungu,hawa hupata gunia 20.

Mikoa mingine inayoomba mizImu hupata gunia 9
Hahahaa mkuu umenichekesha...hahaahaa mikoa tofauti na kaskazini wanatumia mizimu gunia hazizidi 9 kwa ekari.
 
Naam swali lako ni pana sana. Mfano nyanda za juu kusini wao ndio wanaoongoza kwa kuzalisha zaidi. Wao mvua zao ni ndefu na wanaweza kupanda mbegu inayokaa shambani hadi siku160 kukomaa.

Hii inazaa sana mandhali tu mbolea itakuwepo. Hapa panawezekana kupata tani 40 kwa mkulima mtaalamu. Ukanda pwani mvua zao fupi na.mbegu zao fupi na hivyo kiwastani mkulima mtaalamu akivuna saaana ni hizo gunia 15 hadi 20.

Kumbuka kadiri unayoipa mbolea ardhi ndivyo utavyovuna
 
Je waweza nijulisha ni mbegu gani unatumia katika kilimo cha mahindi na sifa zake! Me ni mkulima mchanga nahitaji uzoefu wenu tafadhari
Mbegu zipo nyingi sana lakini ni location specific. Lazima ununue ambazo zimeshathibitishwa kwenye zone yako
 
Inategemea unalimia wapi?

Kaskazini wanalima kisasa,wamesoma na wanamwomba Mungu,hawa hupata gunia 20.

Mikoa mingine inayoomba mizImu hupata gunia 9
Mngekuwa mnalima kisasa na mmesoma na mnamuomba huyo Mungu wenu si mngekuwa mnailisha Tanzania nzima nyinyi,acha logic zako za kijinga..kwa mahindi nyanda za juu kusini ndo wakulima hodari, hizo pumba ulizoandika wapelekee hukohuko
 
Kilimo cha mahindi
2014-06-18-120.jpg

2014-06-18-121.jpg
2014-06-18-120.jpg
2014-06-18-121.jpg
2014-06-18-136.jpg
 
Asante kwa darasa zuri sisi wakulima tumekuelewa. Mimi niko Tanga mbegu niliyotumia ni seed. co vp unaweza kunisaidia sifa ya hii mbegu?
 
Asante kwa darasa zuri sisi wakulima tumekuelewa. Mimi niko Tanga mbegu niliyotumia ni seed. co vp unaweza kunisaidia sifa ya hii mbegu?

mbegu za seedco zipo za aina nyingi na zina namba na sifa tofauti lakini nyingi zinakomaa muda wa kati kuanzia siku 130
 
Back
Top Bottom