Nimeangalia takwimu za matokeo kidato cha sita, somo la physics hali ni tete. Shida iko wapi?

Nimeangalia takwimu za matokeo kidato cha sita, somo la physics hali ni tete. Shida iko wapi?

Physics ni ngumu ila ufaulu kama huo japo hiyo ni shule tunayoiamini kuwa ni shule bora, lazima kutakuwa na walakini. Physics imerahisishwa sana siku hizi. Sijui ubora wake bado ni ule ule.

Mwaka 2013, kulikuwa na C pekee ambayo ilikuwa marks kubwa kitaifa. Hiyo ndio ilikuwa Physics kwenye uhalisia wake.
Kwa kweli kupata "A" ya physics miaka mitano nyuma elikua sio rahisi kwa mtihani wa Nect, hata Kenya na Uneb kule uganda haikua rahisi lakini leo Necta ina A za physics zaidi ya 500 nchi nzima, tena hapo hapo na "F" zikawa zipo nyingi, kuna logic gani? Mimi siamini upangaji wa matokeo wa Necta wana mfumo wa kuchangua shule ipi iongoze
 
Unajuaje mwaka huo labda mlikuwa vilaza wote labda huyo wa c.
Physics Ni tamu ukiielewa sema ukikariri utaumia
Ulipata ngapi Physics mkuu?

Mimi nilipata B, nilitumia mbinu zote nilizozibaini kujifunza, nikabahatika na hiyo marks
 
Katika masomo yote, naamini Physics A level ndio somo gumu kuliko yote.

Mambo yote mtu anasoma kwa miaka 4 O-level, yanarudi A-level tena kwa kwenda deeper zaidi, halafu kwa miezi kama 18 tu.

Mtu anayegonga A kwenye physics A-level, hakuna kitu kitamshinda kujifunza chini ya jua.
 
Somo la physics, somo la physics.

Je Tz hatuna waalimu wabobezi kwenye hili somo amaa ni somo gumu sana...
Physics ni somo ambalo halina waalimu wengi . Hili somo linahitaji kusomwa kwa nadharia na vitendo. Sijui katika kuangalia kwako shule kama Feza, Mariani Girls na zingine za binafsi ufaulu wao wa somo la Fizikia uko vipi- nategemea shule hizi zitakuwa na waalimu wengi, maabara na vitabu. Fizikia inahitaji uwekezaji katika kupata waalimu wanaolielewa vizuri na kufundisha kwa kujiamini.
 
Watoto wenu wote sahv wanataka wawe wakta mauno tu

Ova
 
Somo la physics, somo la physics.

Je Tz hatuna waalimu wabobezi kwenye hili somo amaa ni somo gumu sana?

Nakumbuka mimi pia nlivyokua nafanya mtihani wa physics, kidato cha sita, niliteseka sana kwa kukutana na maswali ambayo sikujua hata nianzie wapi kusolve.

Bado namkumbuka mwalimu wangu ambae alikua anatumia lisaa lizima kusolve swali moja ubaoni, sembuse mwanafunzi mwenye maswali matano ndani ya masaa matatu.

Mna maoni gani juu ya somo hili wadau
Mimi mambo ya physical niliona niachane nayo, nimeamua sasa kuhamia spiritual!


YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI
 
Katika masomo yote, naamini Physics A level ndio somo gumu kuliko yote.

Mambo yote mtu anasoma kwa miaka 4 O-level, yanarudi A-level tena kwa kwenda deeper zaidi, halafu kwa miezi kama 18 tu.

Mtu anayegonga A kwenye physics A-level, hakuna kitu kitamshinda kujifunza chini ya jua.
Nimependa hapo mwishoni
 
Somo la Physics, somo la Physics.

Je, Tz hatuna walimu wabobezi kwenye hili somo amaa ni somo gumu sana?

Nakumbuka mimi pia nlivyokua nafanya mtihani wa physics, kidato cha sita, niliteseka sana kwa kukutana na maswali ambayo sikujua hata nianzie wapi kusolve.

Bado namkumbuka mwalimu wangu ambae alikua anatumia lisaa lizima kusolve swali moja ubaoni, sembuse mwanafunzi mwenye maswali matano ndani ya masaa matatu.

Mna maoni gani juu ya somo hili wadau
Kufaulu physics inategemeana na shule unayosoma
 
Hilo somo hata walimu wake kwa advance huwa wanaruka ruka tu unakutana na swali la mechanics mda wenyewe wa mtihani masaaa matatu waongeze mda kwenye mtihani wa physics pia walete walimu walio serious
 
Pole mkuu. Daah nini kilifuata mkuu?
Eti mimi ndio nikawa naongoza physics japo nimepiga E 😂😂😂, na hata chuo, E ndio ilikuwa kali kabisa kwa physics kwa wadahiliwa wote wapya 😂😂😂; yaani physics, aagh
 
Uzuri ulishalisoma hilo somo.

Wewe unaona tatizo nini?

Una maoni gani juu ya hilo tatizo?
Physics ni SoMo rahis sn.tatizo hatuna walimu competent.wao wanafundisha kusolve maswali na sio kuumpa mwanafunzi knowledge.km mpo mliosoma mkwawa high school humu mliomaliza mwaka 2000 PGM AU PCM mkumbukeni yule mwl mzungu Mr ANDY.dah alikuwa anafundiaha knowledge.dah ANDY ANDY
 
Physics ni SoMo rahis sn.tatizo hatuna walimu competent.wao wanafundisha kusolve maswali na sio kuumpa mwanafunzi knowledge.km mpo mliosoma mkwawa high school humu mliomaliza mwaka 2000 PGM AU PCM mkumbukeni yule mwl mzungu Mr ANDY.dah alikuwa anafundiaha knowledge.dah ANDY ANDY
Kwa sasa ingia youtube tu, utapata kila knowledge
 
Nakumbuka Kuna jamaa yangu alidisco chuo kwasababu ya courses za physics.

Okay physics inataka kichwa na sio kichwa Cha kitoto.
 
Physics ni kisanga hasa A-level,watu wengi wanaikimbia,hivyo kunakua na uhaba wa watu wanaosomea ualimu wa somo husika na hivyo kupelekea walimu kua wachache,at the end of the day,wanafunzi wanaobahatika kulifaulu hilo somo kwenda A-level,wanakumbana na ukosefu wa walimu competent,hence kupelekea Matokeo mabovu.
true
 
Back
Top Bottom