Nimeangalia takwimu za matokeo kidato cha sita, somo la physics hali ni tete. Shida iko wapi?

Nimeangalia takwimu za matokeo kidato cha sita, somo la physics hali ni tete. Shida iko wapi?

km ingekua kipindi cha kufaulu hili somo basi ni kipindi hiki, kuna mifano mingi sn ya soma ya physics, mfano wafungaji wengi wa magoli mpira wa miguu wanatumia sana projection which is part of physics, light za barabarani, simu, hata games zao wanazochezea majumbani kuna maths and physics kwa wingi, shida ni kua wanaowazunguka ndio wamejaa ambao sio watu wa science or kujua hilo somo kabisa. they do things without knowing nini wanachofanya.

In short muongozo wa mazingira wanayotumia muda mwingi hawana muongozo wa hilo somo, kingine walimu wa zamani walikua wapo vizuri sana kwenye practicals kuliko theory, wale waliopata GPA kubwa ndio wanaopelekwa ikiwa practicals hawajui, mimi nifikia waalimu toka vyuo km DIT, veta,au hata watu waliopo kwenye field inayoendana na physics wangepelekwa hasa kwenye vipindi vya practicals kwenye shule mbali mbali at least ingesaidia.
Hii mifano alikuwa nayo mwalimu wangu Kulwa, nikaikuta kwa mzee Mamuya 😂😂😂 ila kimsingi swala la kuchomoka na D-Lock lilikuwa mtambuka.
 
Pale Tabora boys nimeona matokeo yao kuna vijana zaidi ya 50 PCB wana 1 ya 3, hao wana someshwa na waalimu gani? Some time metokeo ya Necta yako selective na un predictable msishangae tena mwakani somo la biology kua gumu kuliko physics au Math.
Unafanya reference kwenye shule moja... fanya research,halafu unatakiwa ujue,hizo shule za BOYS,in most cases,wanapiga msuli wenyewe,i.e wanakomaa wenyewe,msaada wa waalimu,ni mdogo sana.
 
Tatizo sio waalimu, ni Msingi mimbovu uko o-level watu wana fauli physics chemistry uko olevel bila kua na maabara shuleni, wakifika advance ngoma nzito kweli kweli, lasima wachemshe tu.
Maabara ndiyo inafanya mtihani? Hamkosagi pa kujificha. Vitoto vya siku vichwa maji haviko serious. Physics A-level Paper 1 na 2 hakuna cha maabara, Paper 3 ndiyo mambo ya practicals. Hata hivyo maswali yenyewe ya kawaida na ni maswali machache tu. Watoto hawako makini hawasomi inavyotakiwa wameshajaza mambo mengi kichwani yasiyowahusu.
 
Huu ni mfano wa paper ya physics kwa watoto wa form two.... vp mkuu mwanao atatoboa hapa
Screenshot_20230111-175556.jpg
 
Shida ya physics ambayo ni shida pia ya Masomo mengine ya science advance ni muda wakuisoma haujawai kutosha, ukitaka kufaulu inabidi unapoenda 5 uwe ushamaliza form 5 unapoenda six ushamaliza six, mwaka wa mwisho we somo chand, Nelcon, up na madude yote maswali ushapitia yote unayakumbuka vizuri approach yake..

Angalizo: hii ni constant kama pi. ukichanganya advance na mapenzi ushapata div 3 au 4 kabisa hili ndilo janga la boys wengi,
 
Na bado ya form four hayajatoka
Aisee, Physics NECTA ya form four wamezingua, wametoa maswali ambayo hata kwenye syllabus hayapo, na mengine ni maswali ya between lines kabisa. Vitu vingi ambavyo wanafunzi wamevisoma kwa miaka yote minne hawajavitumia kujibia mtihani wao wa kidato cha nne..
Mi naona kwa namna hii serikali inashindwa kujua hali halisi ya Wanafunzi katika somo la Physics. Matokeo ya form four physics 2022 yakiwa mazuri, basi kuna michongo imefanyika
 
Shida ya jamii yetu haipo kivitendo tunakariri sn not kuelewa ndio mana tunawatu wasiweza hatakujieleza wao wenyewe ni nani. ..science ni vitendo cku zote ukifuatilia hata maisha yako kwa siku ni sayansi tosha,u burn energy kwa kutembea while generating heat kwakutoka jasho(physics)..while increasing blood pressure(biology).huo nimfano tu
 
Back
Top Bottom