Nimechoka na ndoto za kula na kufanya mitihani

Ndoto ni issue ya kisayansi, sasa we doctor, halafu haujui ndoto inatokeaje?
 
Nakubalina na wewe.Future yake imeshakuwa blocked.Baadaye ataacha kabisa hiyo kazi anayofanya atabaki kupenda kukaa ndani na kuendelea kujitenga na watu.Dalili ni kwamba kwa sasa visioning horizon imeshakuwa squized. Kama unaota unapiga mitihani ya nyuma hivyo na bado inakuzingua,this tells a lot bro.

Na inawezekana pia imetokana zaidi na hao wanawake aliowaumiza. Spritualy ameshalishwa vitu vya kutosha in real sense.

Ila bado hajachelewa,the fact kwamba amekuwa na bahati ya kujitambua mapema.

So jaribu kuweka u-daktari wako pembeni kwa muda, fuata huo ushauri wa kuwaona viongozi wa Kiroho,Watakusaidia,
 
Achana na ngono! Soma biblia.
 
Kwanza usisome chochote kitakokufanya ujione huna matarajio (hope) yoyote, au maneno yanatakayokufanya uone huna mwelekeo, au ujione hufai au ujione we ni mbaya au ujione una mapepo au ujione umefungwa. ACHANA NAYO hayakusaidii chochote. Ukweli ni kuwa ndoto zako ni ujumbe wa nafsi yako kwamba kuna nini kinatokea, au nini cha kurekebisha au nini cha kufanya, we unachotakiwa kufanya ni kuisikiliza nafsi yako majibu yote unayo.
.
Umekuwa unawakubalia watu hata kama moyoni unakataa, unachukua malaya lakini unajisikia vibaya ukiwa nao ni hicho hicho mwili wako unakuambia kuwa huwezi sema hapana kwa nyege zako au kwa watu wengine. Kwa kuwa haukulifanyia kazi ndo mana nafsi yako inakuletea ndoto kuwa unashindwa kusema hapana na unaendelea kulishwa.
Nafsi yako inaleta hiyo ndoto ili upate kuelewa hali uliyonayo katika maisha ya mchana, na ufanyie kazi.
Ndoto ya pili inakuonesha umerudi mpaka level uliyokua vizuri, maana yake hiyo ndo sehemu ya maisha yako uliyokua una ishi kwa malengo kulinganisha na sasa. Na kufeli ni kwamba tu ulikua vizuri mpaka ulipofeli kwenye maisha ya mchana. Kiurahisi nafsi yako inakuonesha wapi uliishia kuwa mtu bora zaidi.
.
Anza hivi;
  • Jiwekee malengo mapya. Andika vile unataka uwe mbeleni kisha chukua iyo karatasi na ubandike sehemu utakayoiona kila siku.
  • Badili mazingira unayoishi, hii iwe ishara kwa nafsi yako na akili yako kwamba unabadili maisha yako. Na wewe pia jikumbushe mara kwa mara kuwa unabadili maisha yako. Kumaanisha una break cycle uliyoisema.
  • Washirikishe ndugu zako wa karibu kuwa upo kwenye mchakato wa kubadilika, na wanaweza wakakuona wa tofauti kidogo lakini lisiwatie shaka mana ni kwa ajili yenu nyote.
  • Kubali ndani yako kuanza kivingine. Ukikubali utakua umejipunguzia mzigo wakati wa mchakato wa kubadilika. We ni tabibu najua unajua kwamba ili mwili ubadili mfumo unahitaji takribani siku 30, hivyo kubali itachukua muda.
Pia katika safari ya mabadiliko utakumbana na hali ya kutaka kurudi kama mwanzo kwa kuwa mwili haujazoea lakini huo ndo muda mwili na seli zako zinaandika mfumo mpya ndani ya mwili wako. Ulichoishi hadi sasa ni mfumo tu, pitia uzi nilioandika kuhusu mfumo, ila ubadili baadhi ya maneno na uchukulie kama ndo maisha yako.
  • Anza kujizoesha kuwa na misimamo na uwe na thamani zako (values). Hii ni mihimili ambayo itakuongoza kwenye kufanya maamuzi yako yote. Jitahidi usome kitabu kimoja kinaitwa 'The Confidence Gap by Dr Russ Harris'.
  • Kutakua na siku utateleza. Sio kwa sababu umeweka malengo mapya basi utaenda moja kwa moja. Kwahiyo kuwa na amani siku utakazo poteza, jikumbushe kuwa na amani. ILA fanya juhudi siku mbovu ziwe chache kuliko siku nzuri.
  • Nenda katoe tu shukrani kanisani, au shiriki chakula na mtu asiye na uhakika wa kula hiyo siku, au mnunulie kiatu asiye na kiatu, au chochote ambacho kitakupa furaha kinachohitaji ujitolee kwa mapenzi yako. Hii haijalishi umeshafanikiwa au bado.
  • Hakikisha afya yako iko poa. Kunywa maji, fanya mazoezi. We ni tabibu najua utakua vizuri hapa.
.
Cha kufanya.
  • Anza kujifunza kusema hapana, haijalishi ni nani, ila anza taratibu. Ukijizoesha hili litakusaidia kusema hapana hata kwa mwili wako pindi unajikuta unafanya kitu usichotaka.
  • Weka malengo madogo madogo kwanza ili kujizoesha. Vuta kumbukumbu nyuma hadi muda uliokua una malengo na unaishi kimisingi. Kisha jikumbushe ulikua unafanyaje hicho kipindi, inaweza ikakuchukua wiki au mwezi au zaidi cha msingi tu ujikumbushie na upate ile hisia jinsi ulivyokua na uishi hivyo sasa.- Usibishane na nafsi yako. Anza kujifunza kuisikiliza nafsi yako, hata kama utaona kwa akili ya kawaida ni ngumu ila nafsi yako ina majibu mazuri. Acha nafsi yako ikuongoze. Fanya vile vitu nafsi yako inasikia furaha.
Ukitaka kujua (au ishara ya kwamba unakiuka nafsi yako) unabishana na nafsi yako, ni vile ukijisikia vibaya kama chuki, uoga, wivu, uongo au hisia zozote zinazokufanya ujisikie vibaya.
Na ukitaka kujua kama upo kwenye mstari utajisikia amani, faraja, matumaini na hisia zote za furaha.

Enjoy and have fun. Nikutakie kila la heri.
 
Nilikua karibia sawa na wewe kwa asilimia 95 lkn hivi sasa nimekua kiumbe kipya.

Sasa mimi nilikua naota nimebebwa kwenye jeneza naenda kuzikwa.
Ndoto ni ishara Mungu bado anakupenda na anataka akubadirishe.

Pombe na wanawake wa bar walikua wananisababishia hizo ndoto and i knew it.

Nikarudi kwenye uhalisia wa roho na nafsi yangu kwa njia ya toba na kubadiri tabia.
 
Kwahiyo sasa hivi unaendeleaje?
 
Amua kuacha Dhambi, Mrudie MUNGU... Mafanikio yako ni makubwa...lakini shetani amefanikiwa kukuzuia Usione mbele na Usifikie hayo mafanikio...Maumivu unayoyasikia na Majuto unaoyapata baada ya kushiriki Ngono...Ni wazi kuwa MUNGU anajaribu kukuonyesha kwamba unachokifanya si sahihi...Ni kama kujiangamiza nafsi yako mwenyewe....Hutasonga mbele kwa maana Dhambi unazozifanya zina mpa uhalali shetani kuendelea kushikilia Maisha yako...hivyo Mpe MUNGU nafasi aokoe Maisha yako.
 
Kwahiyo sasa hivi unaendeleaje?
Sasa hivi nimerudi enzi nikiwa hasa sekondar advance kurudi nyuma kwani nimekua nikiota ndoto za mambo yajayo na hutokea ktk uhalisia.
Pia naiona future njema ktk ulimwengu wa Roho kutoka kwa Bwana, zaidi sana nimekua mtu wa kkubarika kwenye vibarua tofauti na mwanzo.

Ndoto za kuwa nipo shule napambana na mitihani sahizi zimekata kabisa, saa nyingin naendesha gari huku giza au gari haina break n.k
 

Wacha nikwambie! Hicho ninkipindi tu ambacho unapitia kwenye maisha na tulio wengi tumepitia humo!

Miaka hiyo uliyonayo ambayo bado hujafika 30s ndiyo kipindi unahangaika kuweka maisha yako sawa kuwaza na kuwazua kwahiyo ndoto ni matokeo tu ya unachokiwaza na ukubwa wake…
Usiogope utafika umri fulan hizo ndoto utazisahau kabisa na utakuja kimshauri mdogo wako atakayekua anapitia hali hii!

Jitajid kusal kufanyakazi miaka uliyonayo mara nyingi hizo ndiyo ndoto zake!

Hakuna jipya watu washapitia na yakapita! Usijistress ongeza juhudi na maarifa za kaz
 
ukiota unakula ndoto kiuhalisia unalishwa vitu vya kichawi
Hata kama ni ugali na mboga za majani?

Vipi kama kwenye hiyo ndoto anaonekana kukifurahia hicho chakula, na anakula kwa hiari yake?
 
niko katika wakati kama wako ila nimejua njia yakukabiliana na io hali kwanza kabisa kama unakunywa pombe acha nafsi yako haitaki iko kitu cha pili kama kuna kitu unafanya na nafsi yako inafeel guilty acha nacho kuwa busy na ratiba zako jali ur physical health kwakufanya mazoezi kama una marafiki wa ovyo jaribu kujiweka nao mbali taratibu taratibu utaanza kujitambua na kujijua zaidi
 
Paranoia
Fear
Isolation
Small self
Lower self

My son you're very far from the river, and the river is not connected to the Great Ocean anymore, you're on the lake now

Jua kali la kuchoma sana limekuwakia na limetenganisha MTO uliokua unatoka km kijito katika Bahari kuu mithiri ya mirija ipitishayo damu mwilini na sasa limebaki kua Ziwa lenye upweke, wasiwasi na uoga,

MTO huu uliogeuka kua Ziwa baada ya kutenganishwa na Bahari kuu na sasa baada ya kua Ziwa nalo Ziwa limeingiwa na uoga, wasiwasi na huzuni kwamba litakufa baada ya kukaukiwa maji yake

Ziwa hili linaona kwamba haliwezi tena kukutana na Bahari kuu hivyo halitoishi bali litakufa, sababu hakuna mrija wowote wa maji km MITO na vijito utokao kwenye Bahari kuu na kuingiza maji yake kwenye Ziwa hili

Ziwa hili linaona limetenganishwa kabisa na Bahari kuu ingawaji sio kweli kwamba Ziwa hili limetenganishwa na Bahari kuu

Kwa sababu maji ya Ziwa upotea kwa mvuke na kwenda kwenye Bahari kuu na maji ya Bahari kuu hupotea kwa mvuke na kuja kwenye Ziwa hili lililotenganishwa na Bahari kuu kwa kupitia Mvua inyeshayo wakati wa kipindi cha Masika, hii humaanisha kwamba kwa kua Ziwa hili halikuzaliwa basi halitokufa kamwe

Lakini bado nafasi unayo ingia ndani yako nenda ukaulize maswali haya: wapi unapotokea, wapi unapaswa kuwepo, wapi unapaswa kuelekea, wapi unapokosea, nini unapaswa kufanya, na nini dhumuni la wewe kua hapa? Utajibiwa Ila sio hapo kwa papo itachukua muda

My son your eyes looked towards the river before so look on, there's a path via darkness, close your eyes and see what's inside that darkness, what do you see? Like a hoard of dark clouds smothering the Sun, my son there's a light inside the dark clouds.
 
Ukitaka kujua (au ishara ya kwamba unakiuka nafsi yako) unabishana na nafsi yako, ni vile ukijisikia vibaya kama chuki, uoga, wivu, uongo au hisia zozote zinazokufanya ujisikie vibaya.
Limited ego = denial, blocked & repression
Lower self
Small self
Na ukitaka kujua kama upo kwenye mstari utajisikia amani, faraja, matumaini na hisia zote za furaha.
Higher self = Free Soul

There are 4 options to choose between you, your body and your Soul,
1. Share
2. Call
3. Add
4. Block
 
Anza kujifunza kuisikiliza nafsi yako, hata kama utaona kwa akili ya kawaida ni ngumu ila nafsi yako ina majibu mazuri. Acha nafsi yako ikuongoze. Fanya vile vitu nafsi yako inasikia furaha.
One of the biggest reasons why we struggle to connect to our Souls is that we're carrying too much mental and emotional baggage.

Consider what needs to be surrendered, remove it from your life and let it go...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…