Nimechukizwa na wananchi kushangilia vifo vya wanachama sita wa CCM kwenye ajali Njombe. Taifa limegawanyika, tusipuuze

Viongozi, siasa na dini zisitugawe.
Haya yanahitaji matendo siyo maneno matupu kama unavyodhania. Watawala wetu wapumbavu ndiyo wanasababisha hii hali. Ndiyo hasara ya kuwapa uongozi watu wenye upeo mdogo wa kuchambua mambo.
 
Msongamano wa hao ccm kwenye hiace ingekuwa ndo wapinzani hapo kwa askari wa barabarani wangejifanya wako firm kwenye sheria,chuki zinatengenezwa na mengi.RIP wote waliopoteza maisha katika mazingira/hali ya kutojitambua ila nasita kwa wale machawa ambao ni vinyonga kisa maslahi.
 
Uzuri hakuna mtu aliye wakusanya na kuwaambia haya sasa tushangilie , bali ni kila mmoja huko aliko akajikuta anashangilia kwa hiyo kwa sura hiyo hayo ndiyo mawazo ya walio wengi dhidi ya CCM kuna la kujitafakari
 
Si vzr watu kushangilia binadamu wenzetu wanapotutoka hapa duniani.Tatizo ninaloliona na lisipofanyiwa kazi nchi inaenda kumeguka vipande vipande.vijana wengi wamemaliza vyuo mbali mbali na wamekosa ajira sababu ya sera mbovu ya chama kilichopo madarakani.viongozi wanapeana nafasi kwa kufuata historia za wazazi wao bila kuangalia weredi wao.hali hiyo imewafanya vijana kuona kuwa wanatengwa na mifumo iliyopo kiasi cha kutengeneza chui baina yao.kama hilo halitarekebishwa basi ni hatari kubwa huko mbeleni kwani idadi ya machawa ni kubwa na ndo hupewa nyazifa sababu tu ya uchawa wao.
 
Hii sio sahihi ila wana hasira na utawala wa sshv maji kukatwa hovyo mara umeme bas wanachukulia km wanaCCM wote ndio sababu.
 
Pole sana kwa wafiwa na Mungu azilaze roho za Marehemu pahala pema peponi! Amina.
 
Mlaumu Tulia alivyoigiza jeneza la CHADEMA
 
Kushangilia kifo ni ujinga maana sio vizuri kabisa ila kama walikuwa wanawanyanyasa nakuwatesa ofcourse wao watafurahia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…