Nimefanikiwa kupambana na kunguni na kuwapunguza kwa kiasi kikubwa sana

Wakati niko hostel nilikuwa natumia dawa ya kupiga kwenye vyandarua maarufu kama NGAO. Ile ilikuwa kiboko. Inaua kunguni taratibu. Ndani ya wiki hakuna kunguni Wala Mtoto wa kunguni.

Sijui imeenda wapi,siku hizi haipo madukani!
Hiyo machine sio mchezo niliitumia kuua mende .Sehemu nilipomwagia kila mdudu aliekua anakatiza huo ukanda alikua anakufa kwa miaka 3 mfululilizo.
 
Nilitaka kuwaza kiboya ni tangazo I kwa hiyo picha nikajua umeandika kwa lengo la kutoa msaada kwa wahanga ambao wapo kimya. Kunguni wapo hata Mimi juzi nilikuwa na battle nao Ila niliwaangamiza kwa Nuvan na mafuta ya taa.
 
Hawa wadudu mimi hua nawateketeza kwa gharama ya shilingi miambili tu.

Ni Tsh200/-
 
Japo imekaa kama tangazo la biashara ila asante sana mkuu, kizuri mgawie jirani yako.... Mkuu ungesema uko sehemu gani maana kunguni wa Mwanza hawasikii sumu yoyote!
Huku MWanza Kunguni ni janga kuu la Mkoa! Ngoja tu
Kunguni hata MAJI YA POVU KALI unawaua vizur tu.. Nunua sabun ya buku 2 dofi alaf changanya yote na maji Lita 20 njoo nishkuru baada ya wiki alafu mwagia KO na zote Kama unaosha kitanda
 
Suluhisho pekee la Kunguni ni Maji ya Moto. Chemsha Maji yapate Moto kwa kiwango cha Juu kabisa halafu kamwagie Sehemu zote zenye Mazalia yao. Fua vitu vyote halaf anika Juani baada ya hapo kunguni utawasikia kwa wengine
nyumba ya jirani walikuwa wanaanika magodoro yao juu ya bati langu la bafu. kumbe wadudu wanatoka wanaingia bafuni ukienda kuoga wanadandia taulo. Tuligundua baadaye baada ya kuumiza vichwa sana kujua wanakotokea.
 
Dawa mojawapo kunguni ni mafuta ya ndege(airplane) .Namna ya kuyapata ni hasa kwenye viwanja vya ndege. Ndo shida kuyapata na yanaharufu kali sana. Waharifu huyatumia kama nusukaputi. Polisi wakikudaka nayo utaeleza ulipoficha mzigo.
Hayo mafuta ni kiboko kwa kunguni.
 
Nenda duka la dawa za kiliMo na mifugo uliza sumu ya kuua wadudu inaitwa Nuvan chupa moja sh 6,000/ hadi 7 utakuja kunishukulu baadaye,achana na hiyo D zon
 
Dawa ya kunguni ni petrol, weka kwenye sprayer nyunyiza pote unapohisi wapo,ila hakikisha unaponyunyiza usiwashe moto mpaka petrol ikauke. Hutaona kunguni tena kwenye ghetto lako.
 
Kuna dawa moja ya kuulia wadudu wa shamba ,nikichupa kidogo tu kama vile vya dawa za watoto.kuna kunguni walikuwa wakisumbua sana kwenye gari ,watu wanakimbia gari wakati wa usiku,ukiuliza nn jibu ni kunguni,kuna siku tukapewa gari moja wapo wa hizo,aisee kunguni akaleta valangati mchana huo huo,

Kuna jamaa akatuletea ile dawa bwana ,akasema hii ni komesha wala msisumbuke,hiyo dawa ni hatari ,mda wa nusu saa baada ya kupulizia tukapanda kwenye chombo safari ikaendelea,haina harufu wala nn.nitaiulizia jina nilete mrejesho,na bei yake 5k madukani,si unajua lori watu wengine wanahamisha wadudu kutoka majumban.hiyo dawa ni komesha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…