Nimefuatilia Soka Tanzania tangu 1980s sijaona kama Chama

Nimefuatilia Soka Tanzania tangu 1980s sijaona kama Chama

Chama wakawaida sana!! Bongo hii kuna Raia alimzidi Lunyamila tu hapo sijamtaja Said Mwamba Kizota
 
Siku hizi sio mpenzi sana wa soka Tanzania. Niliwafahamu kwa kusikiliza RTD, kusoma magazeti ya Uhuru/Mzalendo, na Mfanyakazi la mwandishi James Nhende aliyepigwa na Zamoyoni Mogella kwa madai ya kumuandika vibaya.

Walikuwepo viungo wa maana kama Charles Boniface Mkwasa (Master), Nico Njohole (Mapafu ya Mbwa), Hussein Ngulungu, Said Mwamba (Kizota), Ramadhan Lenny, Athumani China, nk.

Kutoka enzi za hao niliowataja hapa, sijawahi kuona kiungo mwenye akili kama Clatous Chota Chama (Mwamba wa Lusaka). Goli alilofunga leo dhidi ya Vipers, ni yeye pekee katika Tanzania anayeweza kufunga katika mazingira ya namna ile, wengine wangekuwa na papara ya kupiga ama cross au shuti kali kipa apambane nalo, lkn Chama akatulia na kumgeuza beki wa Vipers na kisha kumuangalia kipa na kumfunga kirahisi.

Chama ana akili sana ya mpira, tatizo lake [weakness] ni kutokuwa na haraka, yawezekana pia hawezi kucheza kwa haraka na makocha wengine hawawezi kuvumilia hilo, lakini hiyo kwa kuwa matokeo yake ni chanya inabidi tu makocha hata wasiopenda kasi yake wamkubali tu hivyohivyo. Kwa upande wangutangu nianze kufuatilia soka letu, sijaona kama Chama.

Vv
Wahi Mirembe hujachelewa sana!
 
Chama ana akili nyingi sana ya mpira.
 
Wakati mwingine muwe mnaweka ushabiki pembeni na ku-judge mambo kwa uhalisia. Kwani Chama amewafunga Vipers tu kwenye CAFCL tangu aje Simba? Vipi Nkana Red Devils na wengine (aliowafunga misimu kadhaa nyuma) nao walikuwa vibonde? Yale magoli yake ya visigino, ambayo Aziz hajayafunga hapa nchini hujawahi kuyaona?
Naamini hata wewe huamini Chama ni mchezaji bora wa wakati wote katika historia ya mpira Tanzania!

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Pamoja na heshima yangu kwako mtoa hoja,kwa hili kwangu its a NO,kunifananishia Chama na legends kama Kizota, Marsha huu ni utopolo, Chama hamfikii hata kwa 40%ya Hamis Gaga (kama ni kijana wa dot.com hujawahi kumwona uwanjani,pole na I can't help kwa hili )hii Tanzania ilikuwa super, Chama dola kimevuruga mambo mengi sana nchi hii na kutuletea wakata viuno na wabana pua, watoboa pua (ME, why utoboe pua?)
 
Huenda ulikuwa ulikuwa unafuatilia kitu usichokielewa. Akina Nonda wamecheza hapo Yanga mpaka club bingwa Ulaya wanafananishwa na reject ya Berkene. Kiuhalisia Chama hafiki nusu ya akina Said Mwamba au Dua Said.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
Nonda unaweza mlinganisha na Samatta!?
 
Nonda alifanya makubwa akiwa Tanzania?
 
Back
Top Bottom