Nimefurahi sana kumuona Rais Samia akiwa amekasirika

Nimefurahi sana kumuona Rais Samia akiwa amekasirika

Kasanzu The Great

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2013
Posts
310
Reaction score
223
Jana nilifarijika Sana kuona Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan akiwa amesarika na kuona hadharani wale wote wanaotafuna Mali za nchi. Alilazimika mpaka kutumia neno '' Stupid'' katika hotuba yake.

Siku za nyuma nilikuwa naingia na wasiwasi juu ya kauli zake za ' 'sitafoka" sitaki nidhamu ya woga nataka nidhamu yandhati'" kwa kauli hizi niliona kama vile Mama alidhani JPM aliwaonea wabadhirifu na wapigaji.

Nilidhani kuwa wale waliokuwa wanafokewa na JPM pengine aliona wanaonewa. Jambo la pekee lililonitia faraja nikwamba alikuwa bado hajajua mambo mengi ya hovyo katika nchi yetu kwasababu taarifa nyingi za kijasusi zilikuwa hazipitii kwake bali kwa Rais Wa kipindi chake.

Sisi wabara hatujawahi kuwa na nidhamu ya ukweli ukweli mbele ya hela, hatujawahi kuwa waadilifu mbele ya hela, sisi hatujawahi kutii mtu bila kumuogopa, taratibu watu walianza kukuona kama mama zaidi Kuliko Rais.

Watu lazima wajue kwamba wewe ni Rais sio Mama. Wanapotekeleza majukumu yako watambue kwamba hawatabembelezwa wala hawatanong'onezwa bali watakabiliwa na adhabu kali za kimaadili na kisheria. Kupitia hivyo nchi itapona.

Mama endelea kufika, ukifoka na ukaonesha vitendo hata yule Mtendaji kata aliyeko mtu kula au mganga aliyeko Tunduma atajua kwamba hii sio zama ya Mama, bali ni zama za Kazi na Rais Wa Jamhuri ya Muungano. Heri kusifiwa na wanyonge kuliko kusifiwa na manyang'au yanayojikomba kwako ili yapate kula.

Mwisho Mama waambie watu wapunguze mahafula na Makongamano yasiyo na tija ili pesa iende kuhudumia wananchi. Mfano Kuna haja gani kuita walimu wa Sayansi kutoka Kagera, Mara, Simiyu nk na kuwakusanya Butimba TTC kwenda kuwasimulia mambo ambayo yako Ndani ya majukumu Yao kila siku kwa wiki moja na kuondoka na fedha za walipakodi? Unahaja gani ya Kuwaita sijui maafisa Habari kuwalundika Dodoma kuwaambia mambo ambayo hata kwenye emails zao ungewatumia tu wakatekeleza?

Mama Asante kwa kutuinesha sura ya Urais
 
Kufokea wezi wasiochoka kutuibia ni kutudanganya, aagize wezi wote wakamatwe na kufikishwa mahakamani.
 
Magufuli alipokua anakasirika anatukana watu wapumbavu mkasema ni udikteta.

Mama anatukana watu stupid, mnasema mnafurahi, sio udikteta.

Mafisadi wanakula nchi kama kunywa juice, stupid haitasaidia.

Rais anaomba eti watu watupishe, hawatoshi, huyo ni rais?

Hua nasema kila siku, Samia hakustahili hata kua mwenyekiti wa nyumba 10 lakini ajabu ni rais wa nchi.

Miaka 7 ijayo kama ataendelea kua rais, hii nchi itabakia mifupa.
 
Kuna Maneno....!

Halafu Kuna Kutenda Vitendo....!

Siku Zote Matendo Yanaongea Louder...! Labda kama Wahenga Walikuwa Wanatudanganya Na misemo Yao..!
 
Jana nilifarijika Sana kuona Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan akiwa amesarika na kuona hadharani wale wote wanaotafuna Mali za nchi. Alilazimika mpaka kutumia neno '' Stupid'' katika hotuba yake.

Siku za nyuma nilikuwa naingia na wasiwasi juu ya kauli zake za ' 'sitafoka" sitaki nidhamu ya woga nataka nidhamu

Mama Asante kwa kutuinesha sura ya Urais
Kwaiyo wabongo ni wapigaji, ndio maana mulikuwa munanunuliwa ovyo awamu iliyopita, mnapenda hela mwakyembe jana ametaja list ya wapenda hela
 
Kukasirika inasaidia nini? tuna taka vitendo wahusika wote kuanzia PM wafukuzwe na kufikishwa mahakamani
 
That should have been followed by a swift disciplinary proceedings. Otherwise such acts will be repetitive.
 
Sema huyu mama anaongea kipole sana ama na yeye ni mpigaji
 
Msimpe stress mama yetu mpenzi, nyinyi majizi embu nendeni Burundi
 
Jana nilifarijika Sana kuona Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan akiwa amesarika na kuona hadharani wale wote wanaotafuna Mali za nchi. Alilazimika mpaka kutumia neno '' Stupid'' katika hotuba yake.

ri kuwalundika Dodoma kuwaambia mambo ambayo hata kwenye emails zao ungewatumia tu wakatekeleza?

Mama Asante kwa kutuinesha sura ya Urais
Tunataka siku nyingine achape mtu kibao jukwaani.
 
Kwa kifupi hii nchi ilipofika kalipio halitosaidia ila vitendo tu..
 
Jana nilifarijika Sana kuona Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan akiwa amesarika na kuona hadharani wale wote wanaotafuna Mali za nchi. Alilazimika mpaka kutumia neno '' Stupid'' katika hotuba yake.


Mama Asante kwa kutuinesha sura ya Urais

Alifikiri wabongo ni watu. Hawa si watu, ukiwachekea, utavuna mabua.
Yeye ashikilie pale pale alipoishia JPM. Wee unafikiri kipindi kile kuna mtu angeleta invoice iliyo na bei maradufu na zaidi. Hajipendi.
 
Back
Top Bottom