Nimegoma Kuwa Mnyonge Mbele ya Polisi

Nimegoma Kuwa Mnyonge Mbele ya Polisi

yaani gari ya kwangu, alafu mtu apande bila ridhaa yangu, zaidi sana anidhalilishe mbele ya mke wangu na watoto. hilo siwezi kulikubali. binafsi traffic akinisimamisha huwa namsalimia akisema anataka kukagua gari namwambia karibu, kagua.

Akiomba leseni uwa namwambia nimeiacha ofisini au nyumbani ila ninayo (kisheria unaruhusiwa kuipeleka ndani ya siku mbili), na sishuki kwenye gari.

Sasa atasema nishuke kwa ajili ya nini?na milango nimelock ataingiaje? aongelee pale dirishani akimaliza kwisha. kama hajipendi sana basi anizuie wakati mimi nimekaa pale usukani na gari inaunguruma.

Wanaangaliaga sura pia wakiona mjinga mjinga ndio wanakunyanyasa, wakiona huyu kichwa kina akili huwa wanajiongeza.

Nikiwa na mke wangu na watoto heshima ile huwa nailinda kuliko hata pesa. huwezi kunidhalilisha mbele ya mke au watoto wangu. huwezi.
Safi sana...
 
Hahaaa vichwa maji aka polisi , hahaaaa Simbachawene aliwaambia polisi haiitaji waliofaulu , halafu utakuta Hilo li Fala Lina F7 yaani fafafafafafafa
 
Sio siri jamaa wanakera sana barabarani...kuna kipindi walikamata kosa la seat cover kama inechanika mimi nikadhani utani....askari mmoja akanambia ni kweli siku hz kuna makosa ya ajabu lkn yapo...
Nilikuja amini pale Canter yetu ilipokamatwa x2 zikalipwa alfu 60

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Polisi sehemu nyingi duniani ndio wako hivi
Hii ni typical police state, traffic officer hana uwezo wa kuchukua chochote kutoka kwako, iwe driving license or gari unless kuna tatizo la uhalali wa license au gari ,yaani nchi hii inakatisha tamaa ya kuishi, ninaota hapa hivi itakuaje Botswana [emoji1052] police waje Tanzania even for 7days wafanye kazi hapa na wa kwetu waende Botswana!,Amina usiamini tutaomba hawa wa Botswana wafanye kazi milele hapa, Botswana cops na wanajeshi wao wapo very smart
 
Upuuzi
Mkuu pambana ndivyo hivyo ulichagua kumaliza hilo jambo,wenzako wakiona kelele nyingi wanachana wallet,kama hela hamna unawasikiliza tu.

Huyo RTO mwenyewe kakujibu kisiasa,bila kujali wewe ndiye unakutana nao kila siku yeye akiwa ofisini tu hajui chochote.

Sasa kama una akili kubwa mfate huyo askari mpange awe mshkaji,sio kwa sababu wewe ni dhaifu sana,ila ni kwa sababu hujui kesho utakutwa na janga gani road hiyo na wa kukusaidia atakuwa nani.

Ukiona ni umama endelea kukaza tu.
 
Mtakuja kufa kijinga nyinyi Watu Wamevurugwa na Maisha Na nyie mnawaletea fedheha mbele ya familia zao"
Hapa ndipo walipoharibu sijui polisi huwa wanatumia busars za wapi. Gari ni chombo kinachotembea na chenye usajiri wa kisheria mtu hawezi kukimbia. Walipaswa wakusikilize kwanza upeleke watu then kama kuna shida hizo nyingine sheria itafata mkondo.

Mwisho wa siku wanakutana na mtu kama hamza inakua historia.
 
Botswwn
Hii ni typical police state, traffic officer hana uwezo wa kuchukua chochote kutoka kwako, iwe driving license or gari unless kuna tatizo la uhalali wa license au gari ,yaani nchi hii inakatisha tamaa ya kuishi, ninaota hapa hivi itakuaje Botswana 🇧🇼 police waje Tanzania even for 7days wafanye kazi hapa na wa kwetu waende Botswana!,Amina usiamini tutaomba hawa wa Botswana wafanye kazi milele hapa, Botswana cops na wanajeshi wao wapo very smart
Botswana wamestaarabika. Vipi huko wskati wa uchaguzi wanakuwa kama hawa wakwetu?
 
Nawasalimu! Tarehe 25/7/2022 nikiwa mizungukoni nilisimamishwa na Askari wa usalama barabarani wakaniomba leseni nikatoa kisha wakaikagua gari na kubaini sina dosari kisha nikaruhusiwa kuendelea na safari zangu.

Kesho yake tarehe 26/7/2022 nikiwa na familia yangu yaani mke na watoto wawili mahali fulani nilikutana na askari wa usalama barabarani wapatao 7, Wakanitaka niweke gari pembeni nikatii , Wakaitaka leseni nikawapa, Mmoja akaizunguka gari kisha akaja dirishani na kuniambia tairi moja imeisha hivyo nishuke garini ili waipeleke kituoni.

Shida ikaanza nilipomwambia mkuu mbona jana tu nilionekana sina tatizo lakini leo tayari tairi imeisha? Akanijibu vibaya kidogo nikaona niwe mpole, Nikamuomba niifikishe familia kisha nitaenda mwenyewe kituoni akagoma akawa mkali, Nikamuomba anipe muda mfupi ili nilifanyie kazi tatizo Akakataa na Kulazisha tushuke garini ili ipelekwe kituoni.

Kama baba Mbele ya Mke na Watoto sikuiubali Unyonge kwani Wazi Niliona Sitendewi haki, Nilishindwa kujizuwia nikamwambia Afande kusema Ukweli hakuna mtu yeyote atakayeshuka kwenye gari na Wewe au mwingine yeyote hapa hataendesha gari yangu.

Hali ikawa tete, Askari wawili wakapandisha Mori lakini kwa hakika Nilivurugwa kidogo kisaikolojia kwa wakati ule Nikawaambia wakati wowote kuanzia sasa endapo yeyote atanigusa au kufanya tofauti na maelezo yangu Hakika jambo baya sana litaenda kutokea. Mimi ni Mhehe original na kwa wakati ule nilijiona naenda kuacha historia mbaya muda wowote. Kwa Ufupi nilidhamiria kufanya jambo baya sana.

Wife anajua kuwa mimi sio mkorofi lakini nikifika kwenye point of no return huwa nakua mnyama, hivyo alishuka akawasihi wanitreat kwa tahadhari, nadhani kuna mmoja aliniangalia akajua sitanii na baada ya kujumoisha maneno ya wife akaona hapa tutaharibu hali ya hewa, Akaanza kuwasihi wenzake watulie kwanza ili yeye asolve ishu lakini hakufanikiwa.

Kufupisha ni kwamba Wawili walikomaa wakakaa garini na kunitaka nifuate maelekezo yao lakini nilivurumusha gari mpaka Ofisi za Polisi za Mkoa Nikashuka na Kuelekea Ofisini kwa RCO jamaa wakawa hawaelewi wakanifuata. Mwisho wa Yote niliacha kizaazaa kati yao na RCO. Walifokewa mno mbele yangu kwakuwaa maelezo yao hayakuwa na maana. Kitu nilipenda ni pale Walipoambiwa kuwa

"Mtakuja kufa kijinga nyinyi Watu Wamevurugwa na Maisha Na nyie mnawaletea fedheha mbele ya familia zao"

Niliambiwa niendelee na safari zangu na niachane na lolote waliloniambia wale askari, Nikawasha gari nikaondoka. Jana nimepita njia fulani nikamkuta mmoja kati ya Wale askari aliponiona aliniambia Bro mji mdogo huu tutaona mimi na wewe nani mjqnja. Hii kauli imenifikirisha sana, Hebu nishaurini nifanyaje aisee manake naanza kuona dalili za kutokea kwa yale ya Iringa enzi zile za Yule mkuu wa mkoa na yule Mkulima. Nadhani nimeeleweka.

Nawasilisha.
Hii post yako imekuwa na funzo kwetu sote polisi na raia pia.
 
yaani gari ya kwangu, alafu mtu apande bila ridhaa yangu, zaidi sana anidhalilishe mbele ya mke wangu na watoto. hilo siwezi kulikubali. binafsi traffic akinisimamisha huwa namsalimia akisema anataka kukagua gari namwambia karibu, kagua.

Akiomba leseni uwa namwambia nimeiacha ofisini au nyumbani ila ninayo (kisheria unaruhusiwa kuipeleka ndani ya siku mbili), na sishuki kwenye gari.

Sasa atasema nishuke kwa ajili ya nini?na milango nimelock ataingiaje? aongelee pale dirishani akimaliza kwisha. kama hajipendi sana basi anizuie wakati mimi nimekaa pale usukani na gari inaunguruma.

Wanaangaliaga sura pia wakiona mjinga mjinga ndio wanakunyanyasa, wakiona huyu kichwa kina akili huwa wanajiongeza.

Nikiwa na mke wangu na watoto heshima ile huwa nailinda kuliko hata pesa. huwezi kunidhalilisha mbele ya mke au watoto wangu. huwezi.
Wabongo tumezid kuwapa hawa jamaa vichwa, wanafanya chochote wajisikiacho ikiwa tu wakikusimamisha ukasimama, shortly wakikusimamisha ukasimama tayari hilo ni kosa namba one, huwez achiwa bure.
 
Botswwn

Botswana wamestaarabika. Vipi huko wskati wa uchaguzi wanakuwa kama hawa wakwetu?
Hapana mkuu siishi huko nipo hapa hapa nchini ila nimebahatika mno kusafiri ndani ya nchi hii, chaguzi zao hazina migogoro na nilikua navutiwa mno na president wao ,mara nyingi alikua anatumia usafiri wa pikipiki (ride himself)na akiingia uwanjani anajichanganya na raia, Botswana wapo Safi sana mkuu, kwenye Army check points ndio pits stop za kulala usiku!,je unaweza park gari pale Lugalo Barracks na kuwaomba wale sentry kuwa unataka kulala!hii ni debate for another time
 
Polisi sehemu nyingi duniani ndio wako hivi
Acha kuhalalisha ushenzi na ukatili huu,Zambia tu hapo check points zipo Safi kabisa, na wazee sisi wa road trips ndio tunawekaga pit stops (na za jeshi pia),Namibia wapo safi, SA wapo Safi unaweza kuendesha kutoka mother city hadi Egoli city bila ya kuingia kwenye road blocks yoyote (1400kms),Botswana ni A1 police na jeshi lao,Tanzania police wetu hili jeshi linahitaji kufanyiwa total overhaul, tuanze upya ikiwa na kuachana na hizi uniform za kikoloni, joto la Dar police wa kiume wave pensi, shirt jepesi, mkanda na service 🔫 kwenye kiuno, rangi za uniform iwe light blue!!
 
Back
Top Bottom