Nimeharibiwa week-end yangu.... lol!


unajua SnowBall. maswala haya yanahitaji kujitoa muhanga sana, manake mathalani wanawake wengi huwa tunahofia kuharibu sura zetu kwenye jamii. unaposema unaenda TAKUKURU ni sawa ila mpaka wathibitishe kuwa anayo hatia labda akukute naye chumbani nje na hapo kwakuwa wote ni mabosi watabebana tu ndio maana tunaona hawa takukuru hawana msaada kwenye swala la sexual harrasment.

yaani ukilivalia nuga sana hadi watoto wako wanakuwa humiliated manake watu watawacheka au kuwatania so unapokaa kimya una contain mengi sana. Msimamo wa mwanamke jasiri utabaki kuwa No tu. Hayo mengine yatasubiri neema ya Mungu manake unafika mahali huoni njia. hupendi kumuumiza mume na wanao.
 
Last edited by a moderator:
Alikutongoza nyuma au mbele?
 
Ukisimama imara utapata haki yako bila kuvua chupi, lakini ukilegea tu utapaka hiyo haki yako na kudhalilishwa juu! Nijuavyo wanaume, ukienda hiyo jmanne utakuta hajaifanyia kazi hiyo barua yako. Najua utapanic zaidi, ila uwe na moyo mkuu. Lakini jua kabisa hapo anapima stability, akiona uko ngangari atajiuliza huyu kwanini anajiamini hivi wakati wengine nimekula ndo nikawasaidia (kama ni tabia yake), hivyo ataifanyia kazi tu ingawa anaweza kuichelewesha kidogo.

Nina marafiki zangu wawili ni mabosi wa walimu, dah ndo tabia zao hizi, wenyewe wanadai ndo marupurupu yao! Hapo akili kichwani mwako, ila unavyolalamika, mhhh sijui kama una ubavu wa kuimili dada yangu. Tena unavyoenda kuomba ushauri kwa walimu wenzio wa kike ndo unaharibu kabisa, unadhani ambaye ameishapitiwa na huyo boss ktk mazingira kama yako atakushauri nini?
 
Filipo haiko hivyo, hata kama tunapenda kutongzwa ndo unitongoze ofisini tena ofisi ya serikali? kaziutafanya saa ngapi?

wewe unayafanya maisha kuwa magumu! Kwani where exactlly is the place kwa kutongoza au kutongoza!? Watu wanatongoza/wanatongozwa msibani, harusini, kanisani, kazini, hospitalini etc! Sio lazima ukutwe mtaani ndio uone ni sawa!
 
Last edited by a moderator:
Smart lady. Sasa nakupa mambo. Siku ukirudi kamsalimie halafu uwe friendly kabisa halafu muanzishe mawasiliano hadi uhakikishe mnapanga kwenda kula tunda. Huku nyuma wewe andaa takukuru na media. Maliza kazi.

itakuwa kujichoresha tu.... kakutongoza, umekataa, maisha yanaendelea... afterall kutongozwa ni sunna
 
Kumbe tatizo ni tumbo tu!
 

sijakubali na nilisha sema sitomkubali kuisaliti ndoa yangu.

sijui ujumbe haujafika....
 
Ungekubali tu, angekuongeza cheo zaidi. Kwani hutaki cheo kikubwa?
 
mito muda mwingine napatwa na uchungu wa haya maisha na kauli zako kuwa ndio marupurupu yao nazidi kuumia zaid. Tatizo mimi huwa nu mtu wa kulia sana nikikwazika nashindwa kuvumilia naanza kualia. Yaani sijui kama hiyo j4 hajanisainia nitafanyaje manake nitajikuta nalia tu. Sipendagi mateso au kitu kinachoumiza mwenzenu. sijui nimeumbwaje.

sasa wewe kama haja saini hadi j4 nifanyeje niondoke tu pasi kumuuliza? au niache kwenda hadi muda upite achoke aamue kusaini? na ataamua lini? nisaidie kaka yangu mpendwa.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo mimi huwa nu mtu wa kulia sana nikikwazika nashindwa kuvumilia naanza kualia. Yaani sijui kama hiyo j4 hajanisainia nitafanyaje manake nitajikuta nalia tu

hapo ndio jamaa atakapochukulia points...utabembelezwa, utafutwa machozi, utaambiwa ukachukue wikiendi maana atakuwa ameshaini then before you know it.....
 
hapo ndio jamaa atakapochukulia points...utabembelezwa, utafutwa machozi, utapewa ahadi tamu then...

sasa umenionyesha point of weekness, haya niambie jinsi ya kufanya basi.
 
Mkosefu wa akili na ni mfinyu wa akili so achana nae,Hana adabu na huenda ata shemeji na watoto zake anatafuna huyo. Pole mwenzangu hayo matatizo yanatukuta sana kwenye ofic za watu
 
Pole.....ila siku ingine uwe unamwambia hapo hapo ili ajifunze sio kwako tu na kwa wengine pia......kama wewe leo umeweza kumuepuka kesho atakuja mwingine atashindwa kumuepuka......ukiweza mrudie ukampe makavu live ili akome na akomae.....pole kwa kuharibu siku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…