Nimehitimisha kwamba watu wasioamini uchawi upo hayajawakuta, na yakiwakuta huteseka bila kupona mpaka kifo

Nimehitimisha kwamba watu wasioamini uchawi upo hayajawakuta, na yakiwakuta huteseka bila kupona mpaka kifo

Acha kuamini ushirikina ndio mana africa hatuendelei kwa akili hizo za kuamini upuuzi.wenzetu wanawaza kwenda sayari nyingine sisi tunaamini ujinga wa ushirikina ,hakuna uchawi wala nini duniani ni imani tu za kijinga

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
PUMBAVU WEWE DUNIA NZIMA INATAMBUA UCHAWI UPO NA VITABU VYOTE VYA DINI VIMEZUNGUMZIA UCHAWI WEWE NI NANI TUKUAMINI TOFAUTI NA VITABU VYA DINI SUBIRI SIKU INAKUJA UTASHIKA ADABU ULAYA KOTE NI,MEKWENDA UCHAWI UPO WEWE NI MJINGA TOKA JAMHURI YA WAPUMBAVU AREA 51 UNAIJUA WEWE BERMUNDA TRIANGLE UNASEMAJE JUU YA HIYO TOA UPUMBAVU WAKO HAPA.
 
[emoji16][emoji16][emoji16]...Sasa hasira zako za kurogwa ndo unazileta Huku.
HATA HASIRA ZIMEKWISHA KWA JINSI ULIVYONISEMA MBAVU SINA ILA UCHAWI UPO TUSIDANGANYANE KABISA HAKUNA ULAYA WALA AFRICA REJEA AREA 51 YA USA KUNANI PALE ?
 
Mimi simjui Mchawi wakukuroga Wala sikuombei kurogwa..

Ila Ni kheri kukaa kimya kuliko kuomba mikosi ikupate.

Mkuu, wengine hatuna hiyo fear of the unknown ambayo wengine wanayo kwa story za hearsay.
 
Mkuu mbona mgumu kuelewa, naona una tatizo la kuelewa vitu kwa haraka inabidi ueleweshwe mara nyingi ili uelewe (kilaza).

Ushaambiwa uchawi unahusisha nguvu za giza wewe unaanza kuleta tena hoja za mapolisi, Duh ipo kazi, Labda utafute mtu mtaekaa nae siku nzima akueleweshe, Mbona wengine wanaelewa fasta tu, wewe siku ya pili hii huelewi tu [emoji16][emoji16]
Huyo jamaa mtabishana mpaka mwakani mimi nisha nyoosha mikono
 
Me naombea mkuu kama unamjua mchawi awezaye kuniroga tafadhali fanya hivyo.
Unadhani hata ukirogwa utajua sasa??? Usikute hata hapo ulipo wanaozungumza ndani yako, siyo wewe na nafsi yako, bali mapepo ya kishetani.
 
Mimi Pia nilikua siamini hadi nimepata matatizo sasa NAAMINI ASILIMIA MIA UCHAWI UPO!!!

Nikiwa na mimba ya miezi mitano niliota nagombania mtoto wangu na watu wawili mwisho wa siku na kweli mwanangu kafa kiajabu ajabu

all in all Mungu yupo ye ndio anaruhusu kila jambo linalotokea cha muhimu ni kumuomba Mungu kwa imani yako!
I agree with many of your statements. Angalizo tu ni kwamba siyo kila bad event ikitokea, basi mtu anakuwa amerogwa (unless kama maana ya kurogwa ni kwamba tukio hilo mwisho wa siku kimsingi chanzo chake ni Shetani, kama alivyo tu msababishaji, mchochezi & mwongozaji wa matukio yote mabaya duniani). Mambo mengine yanayotupata huwa ni normal natural phenomena kwenye ulimwengu huu. Of course the root cause mwishowe ni Iblisi.
 
Ninapoishi hapa kuna mlokole mmoja hivi yeye na kanisa ,kanisa na yeye Ila juzi kampeleka mwanaye Kwa mganga baada ya mambo kuwa mengi...
Hii inaonesha wazi hakuna yeyote mwenye uhakika wa usalama dhidi ya nguvu za giza kama amejiweka pembeni na Mungu, hata kama jina lake na matendo ya nje yanaonekana anafaa sifa ya malaika. Moyo wa mtu anaujua mtu na Mungu anayeuona. Kama first priority yake ni Mungu, lazima anakuwa salama. Kama anaishia kutaja jina la Mungu tu kama chambo na usahihi wa kidini, hiyo haimfanyi awe tofauti na mtu mwingine yeyote asiyemcha Mungu.
 
yaani kama kwangu aisee,kuna kipindi nilikuwa nikilala kuna milango ya vyumba vingine ilikuwa inajifungua yenyewe ni vyumba vilikuwa havitumiki kabisa
Sasa ushasema vyumba havitumiki unashangaa nn sasa??ushawah kutoka kutoka na kuangalia LIVE jinsi milango inavyofanya mauzauza??
 
Unadhani hata ukirogwa utajua sasa??? Usikute hata hapo ulipo wanaozungumza ndani yako, siyo wewe na nafsi yako, bali mapepo ya kishetani.

Kama mtu akirogwa hajulikani nyie mnajuaje fulani karogwa?
 
Uchawi upo siku zote.

Ila watu wanachochanganya ni kuamini uchawi haupo badala ya kuamini kwamba haya maisha unaweza kuishi bili kutumia uchawi.

Mfano mtu aliye elimika kufanya biashara, anaweza kutumia elimu hio kufanya biashara bila kwenda kutumia uchawi wa kutoa kafara.

Ishu inakuja kwamba mtu haamini kabisa uchawi upo, Hawa ndio huwa wanateseka sana, Anaamka kila siku kapigwa chale anadhani kakunwa.

Alafu wachawi wajanja sana, wanatuwekaga katika hali ya kuzoea matatizo kama chura, chura ni kiumbe ambae anaweza ku controll joto la mwili wake, huko china wanapokula vyura ukimweka chura kwenye maji yamoto anaruka anatoka kwenye sufuria, ila ukimweka kwenye maji ya baridi ukaanza kuyachemsha kwa moto wastani basi huyo chura hawezi kutoka humo na mwisho wa siku anafia na kuiva humo humo kwenye sufuria.

Sasa na wachawi ndio wapo hivi, Leo unaweza kuamka na ka chale kadogo sana ukasema umejikuna, wiki ijayo wanarudi tena wanakupiga, inafikia kila siku unaanza kupigwa hizo chale tena sehem mbali mbali, kipindi hicho wewe kwako ushazoea unaona sio ishu sana kumbe ndio unaangamia hivo
Exactly! Jamii nyingi zinazoendekeza uchawi, mara nyingi ndizo zinazoongoza kwa umaskini na elimu duni na maradhi. Uchawi unaharibu ubongo, uwezo wa kufikiri, nk. Inafikia hatua mtu anapuuza tu tatizo alilonalo akidhani ni kitu cha kawaida kinachoweza kutoweka chenyewe.
 
amekariri huyo.
Sema tu wachawi wanawapotezea kwa sababu ni wageni na hawana bifu nao
Kwahyo wachawi wanawapotezea boko haram,IS, Al shabab etc kwasab ni wageni na hawana bifu nao,wanawapotezea mabeberu yanayotunyonya waafrica kwenye madini na rasilimali zetu nyingine kwasab ni wageni na hawana beef nao,[emoji848][emoji848][emoji848]
 
Kama mtu akirogwa hajulikani nyie mnajuaje fulani karogwa?
Ndiyo maana tukasema usichukulie uchawi kwamba ni kitu unachoweza kukifahamu mwanzo mwisho. Mtu anaweza akawa amerogwa lakini kwa mwonekano ana akili timamu kabisa.
 
Acha kuamini ushirikina ndio mana africa hatuendelei kwa akili hizo za kuamini upuuzi.wenzetu wanawaza kwenda sayari nyingine sisi tunaamini ujinga wa ushirikina ,hakuna uchawi wala nini duniani ni imani tu za kijinga

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Unadhani kwa nini watu wanaua albino au kutoa kafara za damu na wengine wanatajirika??? Fuatilia vimbwanga kwenye migodi na baharini na maeneo mbalimbali kama hayo utaelewa hiki tunachozunguza. Kuna wanawake wanapata mimba miezi tisa kabisa mtu anapimwa hospital, then mimba inatoweka kabisa, bila miscarriage wala maumuvu yoyote -- yaani, inapotea tu hivyo basi. Mtu amelala, anaamka asubuhi amevuliwa nguo na kunajisiwa. Au jamaa amegombana na jirani, halafu ghafla anakuwa bubu kama alivyoapizwa na adui yake.
 
Kuna sister alienda chimbo anataka kuolewa na yule Mzee akamfanyia kazi Kisha akamwambia mwanaume wa 3 kukutongoza ukirudi town lazima akuoe kwa harusi ndani ya siku 90 zijazo. Wiki mbili zilizopita tumekula wali ndani ya time frame ile ile ya mtaalam.
Alikuwa ni sister wako au??hiyo mganga tunaweza tukampeleka kwenye ile nchi ambayo ina idadi kubwa ya wanawake kuliko wanaume ili awasaidie dada zetu huko??
 
Mimi Pia nilikua siamini hadi nimepata matatizo sasa NAAMINI ASILIMIA MIA UCHAWI UPO!!!

Nikiwa na mimba ya miezi mitano niliota nagombania mtoto wangu na watu wawili mwisho wa siku na kweli mwanangu kafa kiajabu ajabu

all in all Mungu yupo ye ndio anaruhusu kila jambo linalotokea cha muhimu ni kumuomba Mungu kwa imani yako!
Samahani,Kama great thinker na mfatiliaji wa vitu unaweza ukatutajia sababu zinazoweza pelekea mimba kutoka au kuharibika??go straight to the point please!! Mm naanza na hizi
Kushika ujauzito kwenye umri mdogo kwani mfumo wa uzazi haujakomaa vizuri
Kuharibu kizazi hasa kwamadawa Kama ya kutoa mimba,ulevi etc
You may go on
 
Unadhani kwa nini watu wanaua albino au kutoa kafara za damu na wengine wanatajirika??? Fuatilia vimbwanga kwenye migodi na baharini na maeneo mbalimbali kama hayo utaelewa hiki tunachozunguza. Kuna wanawake wanapata mimba miezi tisa kabisa mtu anapimwa hospital, then mimba inatoweka kabisa, bila miscarriage wala maumuvu yoyote -- yaani, inapotea tu hivyo basi. Mtu amelala, anaamka asubuhi amevuliwa nguo na kunajisiwa. Au jamaa amegombana na jirani, halafu ghafla anakuwa bubu kama alivyoapizwa na adui yake.
Kwa hizo story zako tunaomba ushahidi kwamfano hiyo aliyenajisiwa ucku tuambie anaitwa man,anaishi wap,kabla ya kwenda alikuwa ktk haki gan ulevi au kawaida,rabia zake kiujumla zipoje (IQ).
 
HATA KABLA YA HZO HADITHI ZA KWENYE VITABU VYA DINI UCHAWI ULIKUWEPO KAMA HUAMINI BASI HULAZIMISHWI ILA USIPOTOSHE WATU ETI UCHWI HAKUNA UNAJIDANGANYA.
 
Kwa hizo story zako tunaomba ushahidi kwamfano hiyo aliyenajisiwa ucku tuambie anaitwa man,anaishi wap,kabla ya kwenda alikuwa ktk haki gan ulevi au kawaida,rabia zake kiujumla zipoje (IQ).
Hawez kukujibu huyo..wakishakaa kwenye vijiwe nongwa ndio wanaajazana upumbavu wao na story za kusadikikaa...tunaendelea kusisitiza uchawi haupooo
 
Back
Top Bottom