Nimehitimisha kwamba watu wasioamini uchawi upo hayajawakuta, na yakiwakuta huteseka bila kupona mpaka kifo

Vipi mkuu umetazama video hiyo?
 
hujaenda ulaya kwa muandiko huu hata la saba hujamaliza,endelea kuamini mambo ya kishirikina wenzako wanapiga kazi wanasonga mbele ingekua uchawi upo timu za afrika zingeshinda kombe la dunia,sumbawanga kungekuwa na matajiri kuliko bakhresa,fanya kazi kijana uchawi na ushirikiana ni imani tu za kipumbavu na wanaomaini pia ni wapumbavu
 
watu wanaua albino kwa ujinga tu kama mlio nao nyinyi kuamini vitu ambavyo havipo wafatilie hao walioua albino utakuta utumbo mtupo hakuna lolote,huko migodini na baharini ni imani tu ila ukienda hukuti lolote zaidi ya hearsay,wanawake kupata mimba na kuharibika ni jambo la kawaida la kisayansi akienda hopsital ataambiwa tatizo,mtu aliyelala akaamka amevuliwa nguo huo ni ugonjwa wa kawaida unaitwa symbulism kama sijakosea,yani mtu anaamka anatembea anatoka hadi nje akiwa usingizini halafu asubuhi hakumbuki,kunajisiwa ni nuongo otherwise uniambiwe wewe ushawahi kunajisiwa ila kama umehadithiwa tu endelea kuhadithiwa
 
Mkuu mbona hua nakuona muelewa sana umekuaje? yaani mtu na familia yake wakalale nje? huo ulevi wangapi wanakunywa na hawali nje ? mpka serikali ina ingilia kati hawajui kama ni ulevi?
huo ni ugonjwa upo,mtu anatembea anatoka hadi nje akiwa usingizini
 
ULAYA HAUKWENDA MWANDIKO WANGU NILIKWENDA MIMI HATA HIVYO KWA UPUMBAVU WAKO UNAAMINI WOTE WALIOKO ULAYA WANAANDIKA KAMA WEWE. KORANI NA BIBLIA ZIMEUTAJA UCHAWI TUKUAMINI WEWE PUNGUANI AU TUAMINI VITABU VINAVYOONGOZA DUNIA?
 
Watu wanaokuambia uchawi haupo ndo wachawi wenyewe hao wanakwepa kuzungumziwa.
 
Pale ununio stand kuna eneo haliuziki kila anayenunua anashindwa kuendelea na ujenzi eneo lishauzwa zaidi ya Mara 6 inasemekana wauzaji wa kwanza wana mgogoro
 
Roho ya kijasiri ndio roho gani kwenye uchawi mkuu?
Isiyo na wasiwasi maana unapokua muoga na uchawi ndio unajikuta Kua mhanga wa uchawi zaidi.

Unaweza kuumwa tumbo kawaida ukajihisi umepigwa ata zongo(kimbola) so wasiwasi unazidi kukuponza na uchawi
 
Huwezi kuroga bila sababu kila kitu kina taratibu zake
Wakoloni walitoka kwao wakaja kututesa, kutuonea na kupokonya mali zetu kwanguvu, kama uchawi upo kwanini hatukuwaroga wafe au waugue ukoma?

Kwanini hatukuroga zile mali zirudi kwetu?
 
Mzee wangu alilorogwa, aliumwa wiki moja akafariki...familia ilikua haiamini uchawi ndio maana tulimpoteza....

nilienda kwa mganga, akanitajia aliye mroga na akaniambia mtu huyo amemtoa kafara mzee wako ili awe na pesa za kumwaga...pia huyo mtu atakua tajiri wa kutupwa baada ya msiba...lakini na yeye hata maliza mwaka ni kwamba naye atakufa..

jamaa kweli akawa tajiri, akanunua magari ya bei mbaya, akahama mtaa, akajenga nyumba ya kifahari sana. na kweli hakumaliza mwaka akafa...
uchawi upo wadau.. R.I.P FATHER.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…