Nimehudhuria mkutano wa ukanda kuhusu mkataba wa EPA, Tanzania tumeonesha njia

Nimehudhuria mkutano wa ukanda kuhusu mkataba wa EPA, Tanzania tumeonesha njia

Anna Mghwira,

Lakini pamoja kukubaliana na hii hoja tunatakiwa kutafakari kua ni kwanini wenzetuwalikua wanakimbilia kusaini?

Ni opportunities walizokuwa wanazinyemelea kwetu? Na je, kwa sasa wamerudi nyuma kwakua wenye shamba la bibi sasa wameshtuka?

Jibu lolote hapo bado, Tanzania tunastahili pongezi, full stop.
 
Leo wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wameamua kwa pamoja kusitisha kuweka sahihi mkataba wa EPA hadi Januari mwakani. Awali, Kenya na Rwanda walikuwa wamekwisha weka sahihi mikataba hii.

Uamuzi huu unaziweka nchi za ukanda huu katika nafasi salama ya kutafakari na kupima faida na hasara za kusaini mikataba hii. Tayari Tanzania imeonesha mfano kwa kusita kuingia makubaliano hadi itakapojiridhisha kuhusu faida na hasara za mkataba huu.

Nimehudhuria mkutano wa ukanda kuhusu mkataba wa EPA Afrika Mashariki na kupata nafasi kujadili mambo haya wakati wakuu wa nchi wakiweka misimamo yao. Umekuwa wakati muafaka kwa matukio haya.

Kwa kusita kusaini na kuzishawishi nchi nyingine kusubiri, Tanzania imeonesha njia katika kusimamia mikataba ya aina hii.

Nitakuja na taarifa ndefu zaidi lakini kwa hatua hii, wenzetu toka nchi jirani wametuheshimu. Tutunze heshima hii na kuendelea kuonesha njia sahihi katika masuala ya diplomasia ya biashara.
Thank you m'lady.
 
Wanarudia kuutizama? Au wanawasubiri wasiosaini kwa vile ni mkataba kati ya union na union na sio single countries?
Ndalama sijakuelewa kama unahoji hoja yangu au lugha niliyotumia!

Nilimjibu mwanaJF ambaye anashangaa ati kama suala la EPA lilifanyiwa utafiti kwa nini uamuzi (kusaini au la) unaahirishwa!

Kwanza, asante kwa kusaidia kutoa jibu kwamba ni mkataba kati ya "union (EU)" na "union" (EAC) na siyo nchi moja.

Pili, kwa kuwa inahusu Jumuia ya nchi za Afrika Mashariki, ni muhimu na busara nchi zote zifikie mwafaka kabla ya kusaini, tukizingatia EAC iliwahi kuvunjika.

Hivyo ni matumaini kwamba ndani ya miezi mitatu, waliokubaliana viongozi wakuu wa nchi zinazounda EAC, suala hilo litajadiliwa kikamilifu.

PONGEZI KWAO
 
Tena mkubwa aliongea Kiswahili moja kwa moja na kuwa mfano wa kuigwa wa kuachana na lugha za kigeni.
 
Furaha uliyo nayo inanikumbusha ile habari ya kwenye Luka 10:

Ndipo wale sabini walipo rudi kwa furaha wakisema, 'Bwana, kwa jina lako hata pepo wanatutii?

Bwana akawaambia, 'Nalimwona Shetani akianguka kama mwanga wa radi toka Mbinguni'... Lakini basi, msifurahi kwa vile pepo wanavyo watii bali kwa kuwa majina yenu yameandikwa Mbinguni....
luka 10:17-20
 
Kwa sie tulioanza kufuatilia suala la EPA zaidi ya miaka 5 iliyopita inakera sana tena sana kusikia eti "...hadi itakapojiridhisha kuhusu faida na hasara za mkataba huu!" Mtu mwingine anaweza kudhani suala la EPA ni jambo jipya kumbe lina miaka na miaka sasa!! Ina maana hadi leo Waheshimiwa wetu walikuwa hawafanya tathminini kufahamu faida na hasara za EPA?! Nilitarajia kwa ile jana iwe ni YES au NO, PERIOD... kumbe bado tunatafakari kufahamu pros and cons!!!!

Mkataba wa EPA ni mzuri lakini unaonekana ni mbaya na YES, kwetu ni mbaya au hauna manufaa si kwa sababu EPA as EPA ni mbaya bali ni sisi wenyewe ndio tuna akili mbaya! Tusingekuwa na akili mbaya EPA ingekuwa ni opportunity! We have a lot to sell to EU but we don't know which among them! A country like Tanzania with abundant and virgin land ni kufuru kwa Mwenyezi Mungu hadi leo tunalilia kwamba sisi hatuna cha kuuza EU... community iliyojaa junk and inorganic produces everywhere wakati sisi tukiwa na uwezo na kuzalisha organic produces at minimal cost ambazo ni valuable anywhere na kuweza kulisha the whole of EU!!! Hapa napo Watendaji wa Serikali watalia lia kwamba ni ngumu ku-compete na European Farmers kwa sababu wanapewa subsidize... so why don't you offer the same kwa wakulima wenu?!

"Virgin land"? What do you mean?
 
Anna Mghwira,

Mkataba wa EPA umekuwa negotiated kwa miaka zaidi ya 10.

mkataba huo ulishakuwa tayari toka mwaka 2014 na EAC ikapewa muda mpaka mwaka huu kusaini mkataba huo.

sasa wewe ulikuwa MGOMBEA URAISI kwa hiyo suala hili lazima ulipaswa kulifahamu. Kama unafuatilia kampeni za Uraisi za Marekani wagombea wote wanajadili na wana uelewa wa masuala ya trade agreements.

vilevile wewe ni MWENYEKITI WA CHAMA na chama chenu kina sera zinazohusiana na masuala kama haya.

sasa naomba kujua msimamo wako, na wa chama chako kuhusu suala hili.

JE UNGECHAGULIWA KUWA RAISI WETU UNGESAINI MKATABA HUU? AU UNGEUKATAA?

Eric Cartman , chige, @Nguruvi3,MsemajiUkweli ,Geza Ulole
 
Mkuu JokaKuu,

Mama Anna Mghwira, si tu kwamba ni Mwanasiasa bali ni msomi vile vile. Kutokana na ukweli huo, ningefurahi sana endapo swali lako kwake lingepanuka zaidi ili tuelimike toka kwake... kwamba je, angesaini kuikubali EPA au hapana? Endapo angeingia, anadhani tungenufaika kwa kuzingatia mazingira tuliyonayo hivi sasa na endapo asingeingia, anadhani kuna justifiable reasons za kwanini tusingepaswa kuingia?! By justifiable reasons I mean zile sababu ambazo zipo nje ya uwezo wetu! Kwa mfano, malalamiko yetu Africa cku zote yamekuwa agricultural subsidies zinazotolewa na first world countries na hivyo kufanya farmers agricultural costs kwa hizo nchi kuwa ndogo na matokeo yake Waafrika tunashindwa ku-compete nao. Je, hivi hadi leo hii sababu ambayo tumekuwa tukiitumia over the past 30 years bado ni justifiable?!
 
Lakini hao wanaouza huko Ulaya ni wazungu wakenya wenye connections.

Mwafrika hapati kitu hapo.
Kuna madai hayo kuwa mkataba umelenga sana maua ya Kenya, ambayo ukichunguza pia ni maua ya Tanzania kwa sababu mengi yanasafirishiwa Kenya na wakati mwingne yananunuliwa na wachuuzi wa Kenya ndipo yasafirishwe Ulaya. Ni hivi kwa bidhaa zingine za mboga mboga, vitunguu, ufuta na bidhaa zingine tunazouziana na Kenya.

Washiriki Kenya wanadai kuwa hatua ya serikali yao kusaini ni usaliti kwa Kenya kwa sababu mikataba hiyo haina faida kwa wazawa. Inadaiwa kuwa asilimia 85% ya biashara inamilikiwa na wawekezaji toka nje. Kwa hiyo inakuwa kama mazingira ya mikataba inatengenezwa kwa ajili yao. Ndipo usemi huu kuwa Ulaya inafanya biashara na Ulaya kupitia kenya ama afrika ya mashariki. (Europe trades with Europe through Kenya). Waliokuwepo walitoa mifano kadhaa iliyoonesha jinsi biashara hii inavyoenga kuwaadhibu (nikitumia lugha yao) Wakenya.
 
Kama Uhuru Kenyatta na Paul Kagame wamesaini basi huo mkataba utakuwa uko vizuri tu make hao wawili ndo marais wenye bongo safi na zinazochemka ukanda huu.
Katika hili sitegemei watakuwa wameona kwa niaba ya raia wao ama kwa niaba yao wenyewe. Mikataba ya Kenya inawanufaisha wawekezaji wa Ulaya zaidi ya Wakenya.
 
Yaani nchi zingine ziifuate Tanzania wakati Tanzania inaongoza kwa kuingia mikataba mibovu?
EPA ni Mkataba mmoja. Mibovu mingine nayo iekwe. Hata hivyo EPA mkataba ndio ulikuwa unakwenda kuwekwa sahihi, haujakamilika bado. Naona tunachanganya mada. Huu mkataba ndio ungesainiwa kwa mara ya kwanza.
 
Hili suala linatakiwa kutuleta pamoja na kupunguza tofauti za Kisiasa.uchumi unatakiwa kuwa juu ya siasa.

..sasa mbona wewe hukuungana na wenzako kupinga marufuku ya mikutano ya kisiasa ambayo ni UVUNJWAJI WA KATIBA?

..Je utawala wa SHERIA na KATIBA si suala la VYAMA VYOTE na kila mzalendo wa TANZANIA?

..Unatakiwa uwaunge mkono wenzako ktk harakati zao ili na wao wakuunge mkono ktk yale mambo ambayo ni muhimu kwako.
 
Maana ya EPA: Economic Partnership Agreement / Makubaliano ya Ushirikiano wa Kiuchumi / Kibiashara.

Majadiliano katika Jumuiya ya Afrika Mashariki juu ya ushirikiano wa Kiuchumi /Kibiashara kati yake na Umoja wa Ulaya ujulikanao kama EPA/EU/EAC yalikamilika Oktoba 16, 2014. Mpaka Septemba 2015 taratibu za kisheria za kuingia mkataba, kusaini na kuridhia zilikwishakamilika.

Taasisi za uendeshaji na usimamizi wa mpango huu nazo pia zilikuwa zimekamilika. Ilibakia sehemu ya mwisho ya kusaini na kuridhia mkataba ili uanze kufanya kazi. Hii ni hatua kubwa iliyochukua takribani miaka 15 kuandaliwa. Mkataba ungesainiwa na kuridhiwa tarehe 30/09/2016.

Makubaliano ya EPA yanalenga kuimarisha mahusiano ya biashara ya bidhaa, uvuvi, na ushirikiano wa maendeleo. Mipango ya mbele ililenga kuimaisha sekta za huduma na matumizi endelevu ya rasilimali. Masuala ya haki za binadamu, demokrasia, utawala bora / sheria yameainishwa na kuingizwa katika maudhui ya mkataba.

Licha ya maandalizi haya kumekuwa na mjadala mkubwa na mvutano katika jamii juu ya suala hili: Uhalali wa kusaini ama kutosaini. Aidha maoni mengi yanadhihirisha uchanga wetu katika mikataba ya kibiashara ya kimataifa (mimi mmojawapo) na kuwataka wachumi wafanye kazi ya ziada kutuelimisha. Tunahitaji kujua na kuwajibika baada ya kujua.

Kwanza tupongeze hatua ya kuufanya mjadala uwe wazi kwa umma. Pili tutumie mwanya huu wa kuahirishwa kwake kujifunza. Kujua maana halisi ya makubaliano ya EPA, historia yake, mwelekeo wake na muktadha wake kibiashara: Tujue athari za kuendelea nao ama kuusitisha.

Mambo ya kuangalia katika mkataba huu:

-Uhusiano kati ya Afrika na Ulaya una historia ya utumwa na ukoloni. Kwa watu wengi hiyo ndiyo picha waliyo nayo na swali kwao ni kama tunaweza kuendesha biashara halali na watu hawa. Kwa muda mrefu pia Afrika imepeleka mali ghafi Ulaya ambazo zimepata bei ya chini ikilinganishwa na bidhaa zao za madawa, magari, vipuli nk vyenye bei kubwa.

-Wakati mwingine mali ghafi imetengenezwa bidhaa zilizosindikwa na kupata thamani kwa kiwango cha mzalishaji kushindwa kumudu bei ya nguo moja ya pamba aliyolima na kuuza tani nyingi, kwa mfano. Hii imeletea nchi nyingi changa kutaka kuendeleza viwanda vyake kujikwamua na gharama za uzalishaji toka nje.

Na hapa ndipo mtihani unapoanzia kama viwanda vyetu vidogo vipya vitazalisha bidhaa za ushindani. Je itakuwaje na suala la vipuli, tekinoljia na utaalam?

Kuanzisha viwanda bila utaalam wa kutosha kwenye uendeshaji viwanda kutaturudisha huko tena kununua mitambo na utaalam kwa gharama isiyofanana na thamani ya bidhaa zetu. Kwa hiyo tunahitaji kujipanga vizuri. Si kukata tamaa wala si kuingia tu bila kujua vya kutosha kila hatua tunayochukua.

Katika mahusiano ya EPA nchi zimegawanywa katika makundi mawili: zinazoendelea na zilizo chini ya kiwango cha kuendela. Katika ukanda wa Afrika Mashariki Kenya peke yake ndiyo imefikia kiwango cha kuitwa nchi yenye kiwango cha chini inayoendelea kuelekea kuingia katika daraja la uchumi wa Kati.

Nchi zote zinataka kuhama kutoka kuwa nchi masikini kuingia nchi zinazoendelea na kufikia uchumi wa kati. Hata hivyo kuna wajibu na majukmu kuifikisha nchi katika kiwango hicho.

Suala lililoibuka juzi kuhusu Tanzania kusita kuingia katika makubaliano haya ni la msingi kwetu kujadili na kujiridhisha juu ya mkataba huu ambao hata hivyo hatukushirikishwa vya kutosha nyuma. ....itaendelea..
 
Ukweli moja kati ya hazina kuu za ubora wa rais wetu Dr JPM nimeziona katika kikao cha wakuu wa EA. .kwanza kwa ile intro. Amenifurahisha sana. Na ukweli hakuna maslahi katika EPA kwa nchi maskini. Hasa za ulimwengu wa Tatu. Viongozi wanaopinga wafikirie tena kama kweli wana mapenzi mema Na nchi zao wasisaini huo mkataba.PLEASE Europeans help AFRICA.
 
Duh hapo ndio ninapochoshwa na wasomi wa nchi hii, inakuwaje mpaka leo hamjafanya utafiti kujua faida na hasara za EPA? Kichekesho cha hali ya juu. Kweli kabisa mwenyekiti wa chama unatoka kwenye mkutano unajisifu kuwa hamjui faida au hasara za EPA na kujipa muda zaidi?

Kama hakuna faida kwanini msionyeshe msimamo na kukataa na kama kuna faida kwa nini msikubali? Je hili suala la EPA limekuja Ghafla?

Nyie wanasiasa a wasomi msiofanya utafiti na msiojua wajibu wenu ni mizigo na majanga ya kitaifa. Kufanya utafiti kuhusu EPA mnaitaji miezi mitatu, are you serious?
Pale tume fanya maamuzi kama wana Africa mashariki. Hata kama TZ ilisha jiridhisha kuhusu Epa. Ni lazima turudi nyuma tujiridhishe pamoja kama wana EAC.
 
Mwaka 2014 Jumuiya ya Afrika Mashariki ilisaini makubaliano na European Union, wataalamu wa uchumi wa nchi hii hawakutoka na kueleza nini faida au hata kama kuna hasara katika makubaliano hayo.
Hapa ndipo elimu zetu na vyeti vinapopoteza maana, maana anavyoongea mtaalam wa uchumi na biashara na anavyoongea mtu asiye na weredi kwenye maeno haya ni kama sawa tu, wote wanabuni?
Niliwahi kumuuliza afisa mmoja wa serikali anaelewa nini kuhusu EPA? Hakuwa na majibu zaidi ya kutoa hisia zake na mambo aliyoyasikia kwenye magazeti.
Sasa kama maafisa kama hawa ndio wanamshauri rais katika mambo ya kiuchumi bado tuna safari ndefu.
Nisiingie kwenye maamuzi yaliyofanyika hivi karibuni lakini embu tujiulize maswali machache

1. Unaweza kuepuka kufanya biashara na European Union?
2. Wangapi wetu tumesoma makubaliano ya awali kati EAC na EU yaliyofanyika miaka miwili iliyopita? soma hapa http://trade.ec.europa.eu/doclib/docs/2015/october/tradoc_153845.compressed.pdf

3. Bidhaa/ biashara kutoka East African Community kwenda nchi za Umoja wa Ulaya ni kahawa, maua, chai, kahawa, samaki na mbogamboga - Hii ni exports, je nchi yetu ni shindani katika kuzalisha mazao hayo ukilinganisha na nchi nyingine za Africa Mashariki?

4. Bidhaa kutoka EU kuja EAC ni mashine na mitambo, vifaa vya viwandani na ujenzi, magari na vifaa vya tiba na madawa - Je kwenye njozi yetu ya kuwa na uchumi wa viwanda hatuhitaji EPA? Au tutatumia zana za mawe?

Note: Kilimo kinachangia asilimia 24.5 ya GDP
Viwanda na ujenzi asilimia 22.2
Haya ni maeneo ambayo wataalamu wa uchumi wa serikali hii wangeweka focus yao hapo, na kupima kama EPA itakuwa na faida kwa upande wetu.

Nimetimiza wajibu wangu wa kuchangia kwa mustakabali mwema kwa taifa letu.
 
Back
Top Bottom