Nimeibiwa, nitamkamataje huyu mtu!?

Nimeibiwa, nitamkamataje huyu mtu!?

Habarini wana Jamvi,kwa faida ya wote na wengine Leo nitafunguka Jinsi nilivyo ibiwa Laki Mbili na Nusu yangu na watu hapa watanishauri nifanye nini au tunaweza saidiana Kumkamata huyu Mwizi! kwa faida ya wengine nitaomba Uongozi wa Jamii Forum Uache huu uzi hapa ili watu wajifunze na wajue ili wawe makini, nitasimlia kila kitu na nitaweka ushahidi hapa

Mimi ni mmoja ya watu wanao tumia sana Application ya Kupatana katika kununua vitu,Siku za hivi karibuni niliona kitu cha ajabu kupitia kupatana niliona mtu anapost anauza vitu vya gharama kwa bei nafuu,Cha kwanza nilicho kutana nacho niliona akitangaza kuuza laptop Mackbook Pro,500 HDD,8GB RAM,CORE i7 kwa laki 2.5,pia laptop nyingine Mackbook ila ilikuwa na 1Tb hard disk kwa laki 4.5,nilishangaa na wala sikuamini amini nikaamua kumtafuta kwa kumcondact kupitia namba alizo ziweka Kupatana nikamtext akajibu,nikamuliza unauzaje hio laptop akaniambia laki 2.5 sikuamini nikarudia tena akajibu vile vile,nikamwambia nitumie picha akanitumia picha,nikamwambia wewe uko wapi akasema yeye yupo Njombe ludewa na nje ya biashara hii yeye ni askari! View attachment 329306View attachment 329307View attachment 329308View attachment 329309

Baada ya hapo niliamua kumtext whatsap ndipo alipo niambia kua yeye ni askari na anafanya biashara ya vitu hvyo na kunitumia vitambulisho vyakeView attachment 329310View attachment 329311

Hapo Nikawa na inamani kidogo ila wasi wasi wangu ulikuwa ni kwanini auze vitu vya gharama kwa Bei rahisi hivi? sikutilia maanani sana nikasema labda ni mtu mwenye shida ya haraka na pesa

Inaendelea
Mbona huyo jamaa anajulikana kwamba ni mwizi mule kupatana, bei zake tu unajua kwamba ni mwizi maana hata galaxy s6 edge anauza 250k kwa hali ya kawaida huwez kuingia kingi.

Pole sana mkuu
 
Mimi nashauri Watanzania tusipende vya Bure Computer ambazo mtuhumiwa kazitaja hata iwe used vipi haziuzwi hiyo bei Computer za Apple ni expensive huwa zinafika hadi 4Million na zilizonyingi Laptop za chini kabisa ni 1.5million halafu mtu anakwambia 250K unakubali Kadhalika iPhone 6 Plus haiwezi kuuzwa 250 kwa sababu bei ya hizo simu nia kuanzia 1.6Million tutumie akili za kuzaliwa S6 haiwezi kuuzwa hiyo bei pia tuache Ujinga na kuibiwa kwako ni Sahihi kabisa Hizo bei Hata Screen ya iPhone haizwi kwa bei hiyo tusipende vya Bure!
 
Asante mkuu mimi kanipiga 250 huyu jamaa
Sema mkuu ulikua na mizuka sana..huyo jamaa bei zake tu unajua kwamba ni tapeli..hawezekan bei ya simu iwe sawa au kubwa kwa bei ya mack au envy. .namjua vizur huyo jamaa pole sana mkuu..next tym usipagawe na vitu vikal kwa bei chee.
 
Mimi nashauri Watanzania tusipende vya Bure Computer ambazo mtuhumiwa kazitaja hata iwe used vipi haziuzwi hiyo bei Computer za Apple ni expensive huwa zinafika hadi 4Million na zilizonyingi Laptop za chini kabisa ni 1.5million halafu mtu anakwambia 250K unakubali Kadhalika iPhone 6 Plus haiwezi kuuzwa 250 kwa sababu bei ya hizo simu nia kuanzia 1.6Million tutumie akili za kuzaliwa S6 haiwezi kuuzwa hiyo bei pia tuache Ujinga na kuibiwa kwako ni Sahihi kabisa Hizo bei Hata Screen ya iPhone haizwi kwa bei hiyo tusipende vya Bure!
Kabisa mkuu ukiona bei za huyo jamaa unajua tu ni mwizi..mimi alinambia anauza lg g2 kwa laki 3 then hp envy anauza kwa laki 250 sasa kwa hali ya kawaida et bei ya g2 simu iwe kubwa kuliko bei ya laptop tena hp envy...yani kwa mtu usiependa vitu vzur kwa bei chee huwez kuibiwa na huyo jamaa tena mbaya zaid anataka utume full cash jaman huu si wiz tayar?

kwel nakuunga mkono mkuu maneno yako.
 
Siku ambayo mtatia mikononi wakati wa kum mimina tafadhali naomba munijulishe wadau nimuandalie ky mbili zile za 250gm akione cha moto haina haja ya kumpeleka polisi huyo ni kumf******R* mwanzo mwisho ***** zake huyo
 
Mbona huyo jamaa anajulikana kwamba ni mwizi mule kupatana, bei zake tu unajua kwamba ni mwizi maana hata galaxy s6 edge anauza 250k kwa hali ya kawaida huwez kuingia kingi.

Pole sana mkuu
Na kwa inavyoonekana ni rahisi kumpata maana still yupo hewani hebu jaribu kushirikisha mfano TCRA ili tuone kama ni jipu au
 
Sema mkuu ulikua na mizuka sana..huyo jamaa bei zake tu unajua kwamba ni tapeli..hawezekan bei ya simu iwe sawa au kubwa kwa bei ya mack au envy. .namjua vizur huyo jamaa pole sana mkuu..next tym usipagawe na vitu vikal kwa bei chee.
Mimi ni Muumini wa Kujibana na Vitu vye bei Kubwa ndo huwa naamini Vina Vina Ubora hata Dawa za Meno huwa naona TZS. 2500 unapata whitedent gram 4000 kama kidumu cha lita moja hivi Wakati TZS. 4500 unapata Colgate gram 75-80 inatakiwa Ujiulize hapo ni Ubora haya Swakia hizo Colgate kwa Miezi Mitatu tuu unaona Difference so chenye Gharama huwa ni Bora zaidi hata nguo huwa natamani za Woolworth kuliko sehemu yoyo kwa sababu nikinunua Kadeti ya TZS. 126,000 Hiyo milele yaani mpaka naiacha mwenyewe ni kufua tuu.
 
Jeshi la polisi lipo kwa ajili ya ulinzi wa raia na mali zao, tembelea kituo cha polisi kilicho karibu yako utasaidiwa
 
Watu kama hawa wanafanya wanunuzi wakose imani na wafanya biashara wa kweli. Inabidi mtu uwe makini sana. Usikubali kutuma fedha kiholela.
 
Dah!! Poleni sana... hata hizo picha za hiyo MacBook pro ni za ku-google...
 
Hapa ni simple tu mkuu. Usiwaze sana. NENDA KAMLOGE TUMBO LIJAE MAWE. Inatosha sana.
 
Back
Top Bottom