Nimeibiwa takribani laki 5 na Binti wa duka langu jipya ndani ya miezi miwili. Nichukue uamuzi gani?

Kwa mshahara wa sh 6000 per day ni haki yako kuibiwa...Tanzania tulitakiwa tuwe na mfumo wa kulipana kwa masaa ambayo mtu amefanya kazi...kiwango cha chini kingekuwa sh 2000 kwa saa
Malipo ya mmfanyakazi zinaingia kwenye cost of production. Kama haingizi 2,000 Kwa siku minus other costs unamlipaje hiyo kwa saa?
 
Usisite kumwambia mdhamini wake eti anaogopa, kabla hujachukua uamuzi wa kumfanyisha kazi kufidia hasara alizokutia,
Waambie kwa uwazi kila kitu na yeye akiwepo ila uwazuie easimpe adhabu au kumdhlilisha ili aamini uwepo wako na staha zako ndizo zimetumika kumstiri,
Ukifanya siri ukampa adhabu hata akija hapa jf kulalamika hujampa mshaala wake, sisi tutakuponda umedhurumu binti wa watu,
Kila la kheri ktk maamuzi yako
 
Hata siku Moja usiamini mwanamke Kwa asilimia 100... Utakuja kulia
Jamaa mi nna mke na namuamini anasimamia ujenzi Dar mi nipo Dodoma memwambia akipiga kajipiga mwenyewe.


Na ana biashara yake namsapoti inaenda poa tu 🙂🙂🙂😄😄
 
Kama ameomba msamaha, muache aendelee na kazi lakini mwambie aachane na tabia hizo mbovu na watu wote wanaomshauri uovu aachane naye.

Kumpa nafasi ya pili ndio ubinadamu,kikubwa hakikisha unakuwa makini sana kama kuchukua pesa ya mauzo ya kila siku na kukagua mahesabu kila siku ili isije siku akakupiga na kitu kizito zaidi.

Ubinadamu ni mapungufu, na tunafanya uovu sana, kikubwa ni kama amekiri, ni kumsamehe na kumpa nafasi ya pili, huku ukifanya "close surveillance".
 
Nuzu
Wewe ni binti makini lkn hapa sikuungi mkono.

Watu wengi wanatia hasara sio kwa kuiba bali kukosa uzoefu na umakini.
Kuingiza hasara dukani ni sekunde tu.

Huenda hajaiba isipokuwa kukosa umakini, apewe nafasi na asimamiwe
Hasara ya laki tano mkuu ?kama hana umakini mpaka inatokea hasara kubwa kiasi hiki basi hastahili kukaa dukani.
 
Hasara ya laki tano mkuu ?kama hana umakini mpaka inatokea hasara kubwa kiasi hiki basi hastahili kukaa dukani.
Tuishie hapa tuwaachie wao...upendo wetu na heshima idumu😁😁😁
 
Kijana shamba boy anayemsaidia bosi mmoja wa serikali kutunza kuku wa mayai juzi kati alimkamata kijana wake ready handed akimuibia chakula cha kuku. Baada ya mahojiano ya hapa na pale, kijana akakiri kosa na kuahidi kukatwa pesa kufidia hasara aliyosababisha. Kwa kweli kijana huyu ni mchapakazi na ametoka naye mbali sana....na wakati mwigine hata humpa bosi ushauri wa kibishara.

Basi wakawa wameelewana na hadi sasa kijana yupo anachapa kazi kama kawaida. Unajua wakati mwingine hawa wasaidizi huingiwa na shetani, tamaa au hupata ushauri mbovu kutoka kwa watu waovu. Lakini ukimpa second chance anaweza akawa makini na kufanya vizuri zaidi. Hawezi akakuibia tena kibwege kwa kuwa anafahamu umeishang'amua mbinu zake za wizi.
 
usimfukuze kazi mkuu ni demu wangu huyo ukimfukuza mi nitaishije? hapo ndo sehem pekee ninayo itegemea
 
Siafiki apewe mke labda kama ana uwezo. Ubaya ukimpa mke akiharibu huwezi kumwajibisha
Kweli kabisa mkuu. Wake ni wapuuzi mara 100 ukilinganisha na wauzaji wa kuajiriwa.
 
Wewe kweli zwazwa yaani vilaki vitano ndiyo unavifingulia uzi. Sisi tunaowapa wanawake wetu 1m ya kuendea saloon au tunawahonga range rover vogue ya 400m mbona hatupigi kelele
 
Bora ya wewe laki 500,000 Mimi nina biashara na wife ,tumemuweka shemeji yangu,utaratibu wa urejeshaji wa pesa unafahamika na kuna akaunti ya nmb tulimpa kwa ajiri ya kuingiza pesa ya mauzo.

Biashara ipo nje ya mji ,mda wa masaa mawili kufika huko toka tulipo.
Kwa mda wa mwezi mmoja kama na nusu hivi amekuwa akisumbua sana kuingiza pesa kwenye akaunti ila mauzo yanaendelea na baadhi ya bidhaa kupungua sana .

Madai yake biashara anauza ila anahisi kuna chuma ulete,yaani anaibiwa pesa kichawi.
Na kuna watu amewakopesha bila kujua ni kina nani,yaani ameshawishika kukopesha watu kisha kawasahau hata detail hakuandika.

Nikaamua kwenda kufunga duka mwenyewe kwa hasira.Nashangaa usiku wa siku niliyo funga kijana anaandika meseji kwa dada yake kuwa mimi nilikuwa naenda dukani nachukua hela na hivyo kupunguza uwekaji wa pesa kwenye akaunti ya biashara.
Jumla ya pesa ni 750,000 nilizochukua na hasara kwa ujumla ni 1,400,000.

Kwa hiyo ikawa mzozo pesa imepotea dukani kichawi na na mimi nimechukua pesa kwa duka bila taarifa(kitu ambacho si kweli).kumbuka biashara ni ya pamoja.

Yule kijana tumemfukuza ila nimebaki na risik ya kulipa hela alizodai alinipa mimi mkononi .

Vijana niwapumbavu sana ,nimemwambia wife kama hanielewi kuwa sikuenda kuchukua pesa dukani basi na mimi sielewi kama mdogo wake kaibiwa kichawi pesa dukani.ninapo lipa mimi hiyo laki 7 na nusu na yeye alipe hiyo hasara ya mdogo wake over.

Nimepeleleza nikaambiwa dogo alisha kuwa kit*0 mbi mzuri sana maeneo hayo na mhongaji mzuri tu.

Nilicho uzika zaidi si kupoteza pesa tu,ila kusingizia kuwa shemeji alikuja kuchukua pesa 750000[emoji849] harafu namuuliza aseme ukweli kama nilienda kuchukua anakubali kuwa ni kweli na nilikuwa nimelewa eti mida ya saa moja jioni .
Mi natumia masanga ila si kwa kiwango cha kulewa niende sehemu umbali wa msaa mawili kufika nishindwe kuelewa[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Kwamba ana soma vitabu vya dini ina bidi uki mdaka na boyfriend yake uwa bananishe wote
 
Kumfukuza ni rahisi hata kwake, ishu ni kwamba huo wizi unafidiwaje ?

So unaona suluhisho afanye kazi miezi minne bila mshahara sio?
Anaweza kukubali ila nakuhakikishia mwezi wa mwisho utapigwa million na zaidi!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…