Nimeibiwa vitu vyote vya ndani

Njoo nikupeleke handeni sehemu moja inaitwa kwamsisi,hivyo vitu vinarudi ndani ya saa 24 na wezi wakishavirudisha vyote wanasahau njia wanawashwa mwili mzima wanajikuna mpaka wanatoka damu,watazunguka eneo Hilo hapo kwako huku wanajikuna na kulia kwa uchungu mpka wewe useme either waondoke lakini umewasamehe au waondoke ila hujawasamehe.Mimi binafsi nilisema waondoke ila sijawasamehe,haikupita wiki wakaugua uchizi,ndani ya mwezi kila mmoja alikufa kwa kifo chake(walikua wanne)
 
Kaa Kwanza utulie ndo urudi
 
Moshi kwetu ila pamekua pa ki*** nilienda kipindi cha likizo ya corona nipo home nikaanika nguo walipita nazo mixer boxer na ndala

Sent from my Redmi Note 8 using JamiiForums mobile app
 
washushe kidafu kidogo dogo ndani ya suruali ht cha buku tu..
 
Duh....
 
Yaani bado unaibiwa unalia,nenda kwa mganga ukawafanye wawe mataira
 
Wezi wapo ila hii habari ya watu kubeba hadi vijiko huwa inatokea maeneo flani flani sasa kama mji wa kijanja kama Moshi una mambo hayo sijui.Au kuna demu wako kaamu kubeba vitu ahame navyo maana hali ni tete.

Baadhi ya maeneo Moshi si mazuri sana ni hatari tupu na ujinga ujinga wa vijana, eneo kama njoro sio ajabu
 
Imeongezeka Rau siku hizi, saa 12 jioni mtu analizwa

Rau ni eneo hatari toka 1990s ila miaka ya 2000 kulipoa ila ikabaki kuiba kuku sasa hivi naona kizazi kimerudia ya baba zao.

Ajabu wapo karibu sana na ccp ila ndio hivyo
 
Buza hakufai
 
Pole sana mkuu,

Huu ni wakati mgumu ambao ni wewe ndio unajua uchungu wake kuliko yeyote.

Usiache kutoa taarifa kwa mamlaka za kisheria kuanzia ngazi ya mtaa hadi Polisi.

Utaambiwa mengi,Lakini baada ya taratibu hizo Usiache kumshukuru Mungu kwa mtihani aliokupa.

Naamini wameiba vitu,Ila hawajaiba Akili,nguvu na uthubutu uliokufanya kupambana na kujikusanya hata ukajipongeza kwa kuwa na vitu vyako mwenyewe.

Kuna siku maisha baada ya mtihani uliokupata.
 

Mkuu umeongea kwa hekima na busara sana,ubarikiwe sana
 
Pole mkuu kama vipi watimbie kwa wazee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…