Moniel
JF-Expert Member
- Nov 17, 2020
- 274
- 603
Wakuu habarini!
Nimekuja kwenu naomba nisaidiwe kimawazo na ushauri.
Hivi karibuni nilipeleka barua ya uchumba (posa ) na Mambo yalienda freshi tu. Kikao Cha kupangiana mahari makubaliano yalikuwa kifanyike ijumaa hii. Nimejikuta nina mawazo Sana kwani hela niliyoiandaa kwa ajili ya kuitolea mahari kiasi Cha 700,000 nimekitumia chote kutokana na mkasa ulionipata pasipo kutegemewa jana usiku.
Hipo hivi, Mimi ni dereva bajaji DSM nilijikuta nimeikwaruza gari ubavuni na kuivunja taa ya kulia maeneo ya round about. So mwenye gari akaniamuru ili tusifikishane mbali nimlipe kiasi Cha sh. 650,000 ili akafanye matengenezo ya gari lake, vinginevyo atachukua hatua za kisheria kwani makosa yalikuwa ni yangu. Hivyo nikamlipa.
Nahisi kukata tamaa, kikao ni jumatatu na Sina mpango wa kupata hela nyingine kwa Sasa. Wazee wangu wapo mikoani hivyo hapa town nawatumia wazee tu wa kujuana, na ninaogopa hata kuwaambia kwani watahisi nafanya usanii.
Hivyo nilikua nauliza, Je itawezekana kwenda ku bargain mahali tu kwa sasa hiyo siku, then nitalipa siku nyingine? Hata baada ya mwezi? Au ni lazima kwenye kikao hicho watanitaka kulipa hela kidogo?
Kama Kuna mtu mwenye uzoefu au utaalamu na haya Mambo naomba anisaidie kimawazo au ushauri
Ahsante!
Moniely
Dsm.
Nimekuja kwenu naomba nisaidiwe kimawazo na ushauri.
Hivi karibuni nilipeleka barua ya uchumba (posa ) na Mambo yalienda freshi tu. Kikao Cha kupangiana mahari makubaliano yalikuwa kifanyike ijumaa hii. Nimejikuta nina mawazo Sana kwani hela niliyoiandaa kwa ajili ya kuitolea mahari kiasi Cha 700,000 nimekitumia chote kutokana na mkasa ulionipata pasipo kutegemewa jana usiku.
Hipo hivi, Mimi ni dereva bajaji DSM nilijikuta nimeikwaruza gari ubavuni na kuivunja taa ya kulia maeneo ya round about. So mwenye gari akaniamuru ili tusifikishane mbali nimlipe kiasi Cha sh. 650,000 ili akafanye matengenezo ya gari lake, vinginevyo atachukua hatua za kisheria kwani makosa yalikuwa ni yangu. Hivyo nikamlipa.
Nahisi kukata tamaa, kikao ni jumatatu na Sina mpango wa kupata hela nyingine kwa Sasa. Wazee wangu wapo mikoani hivyo hapa town nawatumia wazee tu wa kujuana, na ninaogopa hata kuwaambia kwani watahisi nafanya usanii.
Hivyo nilikua nauliza, Je itawezekana kwenda ku bargain mahali tu kwa sasa hiyo siku, then nitalipa siku nyingine? Hata baada ya mwezi? Au ni lazima kwenye kikao hicho watanitaka kulipa hela kidogo?
Kama Kuna mtu mwenye uzoefu au utaalamu na haya Mambo naomba anisaidie kimawazo au ushauri
Ahsante!
Moniely
Dsm.