Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kama nakuona vile unavoenda kubargainWakuu habarini!
Nimekuja kwenu naomba nisaidiwe kimawazo na ushauri.
Hivi karibuni nilipeleka barua ya uchumba (posa ) na Mambo yalienda freshi tu.
Kikao Cha kupangiana mahari makubaliano yalikuwa kifanyike ijumaa hii.
Nimejikuta Nina mawazo Sana kwani hela niliyoiandaa kwa ajili ya kuitolea mahari kiasi Cha 700,000 nimekitumia chote kutokana na mkasa ulionipata pasipo kutegemewa jana usiku.
Hipo hivi, Mimi ni dereva bajaji dsm nilijikuta nimeikwaruza gari ubavuni na kuivunja taa ya kulia maeneo ya round about. So mwenye gari akaniamuru ili tusifikishane mbali nimlipe kiasi Cha sh. 650,000 ili akafanye matengenezo ya gari lake, vinginevyo atachukua Hatua za kisheria kwani makosa yalikuwa ni yangu. Hivyo nikamlipa.
Nahisi kukata tamaa, kikao ni jumatatu na Sina mpango wa kupata hela nyingine kwa Sasa.
Wazee wangu wapo mikoani hivyo hapa town nawatumia wazee tu wa kujuana, na ninaogopa Hata kuwaambia kwani watahisi nafanya usanii
Hivyo nilikua nauliza , je itawezekana kwenda ku bargain mahali tu kwa sasa hiyo siku, then nitalipa siku nyingine ? Hata baada ya mwezi?
Au ni lazima kwenye kikao hicho watanitaka kulipa hela kidogo?
Kama Kuna mtu mwenye uzoefu au utaalamu na haya Mambo naomba anisaidie kimawazo au ushauri
Ahsante!
Moniely
Dsm.
Nimekupata mkuu,Tafuta pesa ya kuwakimu na kuwasafirisha wazee wako wa mjini, kisha wapatia hata 100,000 kwaajili ya kutanguliza posa na wakatihuo watatoa ahadi ya kulipa mahari mwezi wa October au November inakua imeisha hiyo.
Hayo yafanye baada ya kuongea na mke wako mtarajiwa, naamini hakuna kitakacho haribika sababu lazima binti atamshirikisha mama yake changamoto yako.
Zingatia kwasasa ukweni kwako pressure kubwa walio nayo ni wewe kwenda kujitambulisha na kubagain mahari. Yaani saizi kwenda kwako ndio jambo kubwa kwao na sio mahari.
Shukran sana mkuuMkuu usiwe na hofu.Ipo hivi, wakati wakujadiliana Mahari watafikia muafaka kuwa Maharibhiyo iwe pesa kiasi Fulani au mifugo au vyote au na baadhi ya bidhaa kama nguo etc. Baada ya hapo wajumbe wa upande wako watawataarifu wale wa upande wa mke mtarajiwa kuwa ngoja wakajipange halafu watawaletea taarifa ni lini watawasilisha Mahari hiyo. Kipindi hicho Cha kujipanga kinaweza chukua hadi miezi 3 na kuendeleza hivyo utakitumia kupata pesa ya kulipa hiyo Mahari. Pia Mahari siyo lazima ilipwe Kwa mara moja bali inaweza kulipwa Kwa awamu. Ahsante
Wakuu habarini!
Nimekuja kwenu naomba nisaidiwe kimawazo na ushauri.
Hivi karibuni nilipeleka barua ya uchumba (posa ) na Mambo yalienda freshi tu.
Kikao Cha kupangiana mahari makubaliano yalikuwa kifanyike ijumaa hii.
Nimejikuta Nina mawazo Sana kwani hela niliyoiandaa kwa ajili ya kuitolea mahari kiasi Cha 700,000 nimekitumia chote kutokana na mkasa ulionipata pasipo kutegemewa jana usiku.
Hipo hivi, Mimi ni dereva bajaji dsm nilijikuta nimeikwaruza gari ubavuni na kuivunja taa ya kulia maeneo ya round about. So mwenye gari akaniamuru ili tusifikishane mbali nimlipe kiasi Cha sh. 650,000 ili akafanye matengenezo ya gari lake, vinginevyo atachukua Hatua za kisheria kwani makosa yalikuwa ni yangu. Hivyo nikamlipa.
Nahisi kukata tamaa, kikao ni jumatatu na Sina mpango wa kupata hela nyingine kwa Sasa.
Wazee wangu wapo mikoani hivyo hapa town nawatumia wazee tu wa kujuana, na ninaogopa Hata kuwaambia kwani watahisi nafanya usanii
Hivyo nilikua nauliza , je itawezekana kwenda ku bargain mahali tu kwa sasa hiyo siku, then nitalipa siku nyingine ? Hata baada ya mwezi?
Au ni lazima kwenye kikao hicho watanitaka kulipa hela kidogo?
Kama Kuna mtu mwenye uzoefu au utaalamu na haya Mambo naomba anisaidie kimawazo au ushauri
Ahsante!
Moniely
Dsm.
Shukran sana mkuu
Kikubwa sitaki wanione Kama msanii aubabaishaji ndo nachofikiria kwa sasa
Wetafuta pesa ya kutumia siku hiyo, then ongea na mkeo mtarajiwa kuhusu changamoto ukilioata. Then nendeni mkapatane mahari bila shaka alafu unawapiga tarehe, na lazima watakubali kwasababu binti atamwambia mamake shida uliopata na mama atamwambia baba, then baba atafanya wepesiNimekupata mkuu,
Posa tayari ilishaenda mkuu, ilikuwa ni suala la mahari tu na kupatana.
Ntafuata ushauri wa kutoa august
Ahsante Sana 🙏🏼 kwa ushauri huu mkuuMbona unaogopa wakati hata mahari yenyewe hujafahamu ni bei gani?
Haya mambo ya mahari mara nyingi huwa hailipwi yote, wanaojielewa hufanya hivyo, wale wabishi tunawaacha wadai mpaka wanasahau wenyewe, siku mtoto wao akiwa na mimba tu ndio mwisho wa hizo kelele.
Hapo usiwe na shaka, tafuta kiasi cha kuanzia, hata laki mbili iwepo mfukoni, siku ukienda iwepo, au hata kama haitakuwepo, iweke karibu, muhimu wakikupa kiasi usisahau kuwauliza namna ya kulipa.
Kama ni mafungu au yote, wakisema yote waambie unaenda kujipanga, ikifika tarehe ya kulipa, toa ile laki mbili ya mwanzo wapelekee waambie yakuanzia.
Hapo wazazi wa mtoto wa kike kama wanajielewa tayari watajua una maanisha kumchukua binti yao, wataiona nia yako, watakuamini, kwasababu wanajua hapa mjini hatushindani kwa pesa, kupata na kukosa yote ni majaliwa tu.
So utaendelea kuwalipa kwa kadri utavyojaliwa, ila hata usipomaliza sio kesi, muhimu tarehe ya ndoa ijulikane ujibebee mtoto mazima, iliyobaki itaenda kumlisha ugali ghetto.
Shukran sana ndugu yangu ✊🏿Wetafuta pesa ya kutumia siku hiyo, then ongea na mkeo mtarajiwa kuhusu changamoto ukilioata. Then nendeni mkapatane mahari bila shaka alafu unawapiga tarehe, na lazima watakubali kwasababu binti atamwambia mamake shida uliopata na mama atamwambia baba, then baba atafanya wepesi
Ok sawa,ngoja wajuzi watakujuza kwamimi sijui Dini inasemaje kwa upande huoKikristo mkuu