Nimeishiwa nguvu na nimekuwa Mtu mwenye kukata tamaa kwa Mkasa ulionikuta

Kwa ile familia laki mbili naona ni Kama dharau hivi
Kumbe hii ndio sababu inayokupa mawazo kwa vitu vidogo, kijana mahari sio aibu, huendi kumnunua binti yao, bado ataendelea kuwa na mahusiano na nyumbani kwao, anaweza kwenda huko pakitokea tatizo lolote akatoe msaada hitajika hata kama utamuoa.

Mambo ya kuangalia uwezo wa kiuchumi wa familia yoyote usijichanganye nalo, kuwa mpole, usijipe mawazo ya bure.

Kumbuka wewe unaipelekea hiyo familia heshima kwa kile unachoenda kufanya kwa binti yao [kuoa], na wala sio kwa pesa ya mahari unayokwenda kuwapa, na kwenye maisha yenu mbele ya safari usipende kujilinganisha na wengine, hata vidole vyetu havilingani.
 
Toa tu taarifa ata ukionekana mhuni si umesema ukweli...

Kuna makabila huwa wanajiandaa sana yani mahari inaweza ikaishia kwenye hio sherehe, usipo peleka unaleta mzozo
 
Kumbe ni kupangiana Mahari, hata kama huna shs we nenda, usihofu... Labda uwe na kahela mfukoninka faini za hapa na pale... Ila Siku ya kupangiwa mahali sio lazima uwe nayo... Ingekua Siku ya kulipa mahali kweli... Vinginevyo uko swafi kabisa wala usipate hofu.. Usihairishe nenda tu alafunmtapanga kikao cha kupeleka mahali
 
Nasema huyo mchumba Ako kwani lazima umlipie mahari ya hapohapo?

Kwanza ana mabalaa Hela ya mahari imepata pancha[emoji23][emoji23]

Muache tu .( Kwa hasira)

Paragraph ya kwanza ndo nmecomment bila hasira.
 
Hakuna changamoto hapo: Mungu amekupa jaribio la kumpima mke wako mtarajiwa kama anafit kuwa na wewe.
Mshirikishe uone atakushauri vipi, akikubaliana na hali yako, huyo ndio mke wako, akikuzingua tafuta mwingine; mwanamke mwema umlinda mumewe kwa hali na mali.​
 
 
Ungetuomba ushauri kabla ya kulipa hizo pesa tungekushauri kitumia bima kulipia huo uharibifu uliotokea. Ila kwa sasa pole
 
Ungetuomba ushauri kabla ya kulipa hizo pesa tungekushauri kitumia bima kulipia huo uharibifu uliotokea. Ila kwa sasa pole
Mkuu kwa Hali iliyokuwepo pale, palikuwa hapatoshi, jamaa pia alikua na power Fulani serikalini Kama angetumia haki angenisumbua Sana.. ningelazimika kuwahonga yeye na ma police
 
Mkuu, yeye hana kosa Hata kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…