Nimejifunza pakubwa kuhusu elimu ya fedha baada ya jamaa yangu kuchukua mkopo wa Milioni 10 kazini kwake ili anunue gari

Bila kukopa Dangote asingejenga kiwanda cha Cement Mtwara
Tofautisha mikopo ya matajiri, Level za kina dangote hakopi kwa kuwa hana fedha, kuna financial intelligence huwa zinawafanya matajiri wakope ili kuendesha mambo yao na sio kwamba wamepungukiwa hela 😁
 
Uzi umenifikia too late,pengine kama ningekutana na wewe mapema nisingefikia huku,mkopo unaofaa ni ule usiozidi miaka 3
 
Seriously, kukopa ili kununua gari ni risk.

Kutegemea na mkoa aliopo inawezekana hata swala la bolt haliwezekani.

Kinachotokea ndiyo unakuta mtu kila training anataka aende yeye. Yupo kwenye hiyo training inakuja nyingine analazimisha aunge training mbili huko huko.

Kila safari anaitolea macho. Kazi kukimbizana na madokezo tu.

Sasa walimu mna hata madokezo? Training? Na si ndo mafunzo yenu yale mnalipwa buku tatu?
 
Tofautisha mikopo ya matajiri, Level za kina dangote hakopi kwa kuwa hana fedha, kuna financial intelligence huwa zinawafanya matajiri wakope ili kuendesha mambo yao na sio kwamba wamepungukiwa hela 😁
Ndio elimu niliyoitoa hapo maana yake kopa ila kopa kwa faida, yaan mfano ukikopa million 100 basi jua hio million 100 itakuingizia million 500 ndani ya muda fulani, kukopa gari sio vibaya swali ni kwamba analitumiaje hilo gari kurudishia pesa ya mkopo? Unaelewa hapo sijui
 
πŸ™ŒπŸ™Œ safari kwa mwalimu ni ngumu
 
Ukianza tu kuwaza wao (Bank) watachukua kiasi gani kwenye mkopo wako then huwezi kukopa kamwe!

Kikubwa ni kukopa kwa malengo yanayoeleweka tu!
 
Yaani mtu akope m 10 mfano akafanya jambo halafu uwe naye level moja na wewe unasubiri 600k kwa mwezi???

Kama hili ni la kweli basi jua umezungukwa na kundi la wajinga na usiposhituka na wewe utaambukizwa ujinga.

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Kama miaka yote saba ujakopa, na bado hauna nyumba kali na ipo location ya maana, na huna gari basi na wewe inabidi tukuchunguze pia.

Kwa mishahara yetu ikifanya saving inakuchukua almost miaka 10 au zaidi kupata nyumba na gari. Kama mtu ameamua kuchukua risk basi tumpe hongera zake tu.
 
Kimaendeleo ukoje mkuu? Natamani sana kujua kwa miaka saba upo kazini na hukopi hata mia, umewezaje kupiga hatua za kimaendeleo?
Umeulizwa swali moja zuri sana.

Kuna mwalimu mkuu mmoja alikuwa na notion kama ya huyu mwamba hakuwahi kukopa ila alikuwa na maisha magumu kuliko hata wenye mikopo. Akiitwa kwenye vikao katani anatembea kwa miguu kwenda katani zaidi ya km 7, hana hata TVS.

Wakati mwingine kukopa ni security, kazi zenyewe za watu hizi. Kuna mwamba mmoja alipona kufukuzwa kazi kisa tu alikuwa na mkopo mkubwa benk m 20+.

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
mkeka nimeuelewa mkuu, ila hapo kwenye 4.5 ndo hujafafanua vizuri. hii 4.5 ina nini cha kufanya na kulipa mkopo twice???

anyway, kwa riba ya 16% ambayo ni sawa na 1.6M/mwaka, mtu huyu anapaswa kulipa jumla ya 19,600,000/=TZS kwa kipindi cha miezi 72 (5 years). hapo unaeleweka vizuri. tuambie sasa hiyo 4.5 nayo ina maana gani????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…