Nimekuwa na mahusiano na mume wa mtu kwa miaka 3 nahitaji kuachana naye, nimuachaje bila yeye kuweka kinyongo

Mwambie wazazi wako wamekutafutia mchumba na unataka uolewe wamekushinikiza...

Ikiwa vipi hizo mali mlizowekeza mnaweza mkagawana nae ili aende salama na wewe uende kivyako..., usipoangalia utakosa vyote...

Fanya haya jana na sio kesho..

Bahati mbaya sana wazazi wanamfahamu kama mtu wangu. Kuna kipindi wazazi wangu walipatwa na changamoto kubwa tu na alitumia pesa nyingi tu kuitatua. Mama huwa ananiuliza tu tuna mpango wa kuoana lini najikanyaga tu naona aibu kumwambia ni mume wa mtu maana sijui atanifanya nini haki ya Mungu.
 
Polee tafuta mchepuko ila usimletee mkeo ukimwi
Mwisho wa siku inakuja kutokea kama ya mleta mada!
Kwa ufupi Mwanamke changamoto zake ni kubwa sana, unaweza kusema unakwepa hili kwa Mwanamke huyu unaenda kukutana na lingine gumu kwa Mwanamke yule.
Tuseme tu mmeturahisishia sana wanaume kutangulia mbele za haki kwa kweli
 

Kuwa mke wa pili tena wakati ndilo ninalotaka kulikimbia? Kuhusu kuolewa alishaniambia hicho ninachokwenda kukitafuta huko ambacho sikipati kwake ni nini?
 
Kubali tu, hili kidogo lina wasumbua! Hampendani!
We nae hebu tutue...hujaona komenti za wanaume walivyotukana kwenye huu uzi? Tungempa moyo pia ungetusimanga kuwa tunampelemba ili mwenzetu aendelee kutenda jambo lisilo sahihi ili aje aharibikiwe mbele. Jiheshimu mzee na heshimu maoni ya watu
 
Kuwa mke wa pili tena wakati ndilo ninalotaka kulikimbia? Kuhusu kuolewa alishaniambia hicho ninachokwenda kukitafuta huko ambacho sikipati kwake ni nini?
Mpendwa wangu kama huna kikwazo cha kuolewa mke wa pili olewa tu maana huyo bwana anaonekana anakujali, unaweza kwenda kutafuta wa peke yako naye akawa na mambo yake ya ajabu au akakuletea wenzio yakawa yaleyale
 

Sasa wewe dini inaruhusu.
 
Hii ba ngoosha !!!! Yan haya maswala hata kama roho ya kishetani huna inajiapload yenyewe, ye binti aombe ndoa kwa uyo kiongozi, ila ingekuwa kule ucgagani machame bibie angemtanguliza mbele za haki jamaa chapu tu
Mwambie tu mama yako huenda atakushauri kitu kizuri tu usimfifhe ,ili suala uamuzi utakaotoa lazima uwe equal ukibase upande 'mmoja umekwisha
 
Kwa nini usiolewe mke wa pili? Hivi unaujua uchungu wa kumchuna vyote hivyo halafu umuache? Hivi hujawahi kusikia matukio ya watu kuuana kwa sababu ya wivu wa kimapenzi? Fikiria kabla ya kutenda. Huo ndio ushauri wangu.

Dini hairuhusu mke wa pili.
 
Nimeifungua mahsusi ili niombe ushauri.
Kuna kitu kipo ndani yetu wanaume ambacho hamnacho nyie wanawake nacho ni kupenda.
Tunauwezo wa kupenda Mwanamke zaidi ya mmoja na kuheshimu wote kwa nafasi zao.
Kwenu wanawake ni changamoto kidogo kuwa na upendo kwa wanaume wawili.

Sisi tunaweza kutamani ukajua tumependa kumbe la!
Tunaweza kupenda ukajua tumetamani.
Kipimo cha mwanaume anayependa ni ile kujali na kuhudumia, fikiri mtu ama make na pengine ana familia lakini bado amejitoa kukujali na kukuhudumia na kukulinda.
Hapo hajakutamani bali amekupenda.

Na kama unavyojua maswala ya kupenda huenda mpaka ndani ya moyo na nafsi na akili na matokeo huonekana kwenye mwili.

Sasa mtu kama huyo kumtoka sio rahisi sana maana mchakato wake ni kuanzia ndani ya nafsi mpaka aje akubali atakua amesumbuka sana na pengine kupoteza vingi wakati akichakata kuondoka kwake moyoni mwake.

Kwa sisi wengine tunaweza kuvumilia kipindi kigumu kama hiko kwa tumaini ya kwamba yatapita tu lakini tutabakiwa na majereha makubwa sana moyoni.

Wengine kwa kweli hawana uwezo wa kuvumilia hali hiyo, wanafanya maamuzi magumu yenye gharama kubwa mpaka ya uhai, na vile umesema ana bunduki, jiadhari sana.


Unaweza ukafanya jambo hilo bila athari kubwa iwapo unatumia busara na akili kubwa na hoja za nguvu.

Kuna dawati la jinsia,kuna viongozi wa dini, kuna wanasheria,kuna watu wa heshima kwako na kwake, na pia nyie wawili mkikaa mkiambina ukweli naamini kabisa mtafika mwafaka ulio bora.

Binafsi nakuombea na kukutakia yote mema,naamini kidogo unapitia pagumu lakini wakati mmoja utafika na utakuwa na heri na furaha na amani.
 

Mali zake na kazi niko tayari kumuachia maana i can manage without him. Tatizo nawaza hatokuwa na kinyongo au hata kunidhuru maana ana wivu balaa. Halafu mpenzi wangu sio serengeti boy ananizidi umri, elimu hadi mali. Kiufupi yuko vizuri na anayamudu maisha vizuri tu.
 
We nae hebu tutue...hujaona komenti za wanaume walivyotukana kwenye huu uzi? Tungempa moyo pia ungetusimanga kuwa tunampelemba ili mwenzetu aendelee kutenda jambo lisilo sahihi ili aje aharibikiwe mbele. Jiheshimu mzee na heshimu maoni ya watu
Duuuu!
Haya bwana, na heshimu maoni ya watu na mimi pia maoni yangu yaheshimiwe.
Wanawake bila ya nyinyi maisha hamna,kwa maana hiyo umuhimu wenu hapa duniani hauna cha kufananishia ila pia mna changamoto ya kuona mwenzenu akiwa anaumia mnafurahi hata kama anaumia kwa ujinga wake.
Mwenzenu pia akiwa kwenye mafanikio mnachukia. Hilo kwa kweli wengi wenu mnalo.
 

Well natambua kabisaaa what i did sio kitu cha kuwa proud nacho na nimesema kabisa. Kabla ya kuwa na huyu mume wa mtu nilikuwa kwenye toxic relationship hadi pale nilipokutana na huyu. To be honest hajawahi nifanyia baya, amenipa good times sana, nimetembea nchi nyingi kwa sababu yake. Hizi good times na kujali kwake ndiko kulinipiga upofu japo kweli kuna muda nafsi inauma kuwa sio wangu. Lakini muda mwingi sana nakuwa nae kama tu vile watu wengine wenye mahusiano wanavyokuwa.

Anyway nimechoka kuwa mchepuko wake na nafsi inazidi kunisuta ndio maana nataka niachane nae.
 
Ni nani uliyeona amefurahia hili jambo hapa? Au umekuja kutema nyongo ulizotoka nazo kwa mkeo ndugu yangu?
 

Sasa nakuwa nimedhulumu vipi ilihali sijawahi mshurutisha wala kumuomba anifanyie hivyo? Nyumba na gari ni vitu wala sina shida navyo kwa sasa naweza nunua zangu hivyo kumrudishia wala sioni tatizo. Hofu yangu ni atalichukulia poa bila kunidhuru?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…