Nimeletewa Kesi: Mke wangu anatoka kimapenzi na Mume wa Mtu

Nimeletewa Kesi: Mke wangu anatoka kimapenzi na Mume wa Mtu

Ndugu zangu wana jamiiforums habari za asubuhi hii ? kwangu mimi ni mzima wa afya na nipo sawa kabisa

Sina cha kupoteza Kama mnavyoona hapo juu kwenye bandiko.

Jana jioni mida ya saa moja nikiwa kazini kwangu kuna dada ninayemfahamu kwa sura tunaishi mtaa mmoja alikuja kazini kwangu, hapo kazini kulikua na watu kadhaa wakipata huduma,

Baada ya watu wote kuondoka alinifata huyo dada akanieleza kwa uchungu mkubwa kuwa "mke wako anatembea na mme wangu mwambie mkeo aachane na mme wangu" maneno hayo aliyatamka kwa kuyarudiarudia na mpaka machozi yakamtoka

Kuna watu wakatokea pale kupata huduma yule dada akaondoka sikupata nafasi ya kuzungumza nae kiundani ili kujua mke wangu alitembea na mme wake lini, na nimeshindwa kuchukua hatua yoyote mpaka sasa nashindwa nianzie wapi, inavyoonekana mpaka dada huyu kulia kwa uchungu mbele yangu itakuwa kweli mke wangu anatoka kweli na mmewake

Ndugu zangu hili suala ni zito kweli kwangu nianzie wapi, majibu sina. Nimeamua kulileta hapa mimi kijana mwenzenu mnipe mawazo nifanye nini nimetuliza akili yangu sijakurupuka ila hatua ya kwanza nimeona nililete hapa.


Asanteni
Yuda_exalioth
Jamiiforums_Geita
Unapata wapi muda wa kuja kuomba ushauri humu jukwaani kabla ya kumtafuta kwanza huyo mtoa taarifa, ili upate ukweli wa hizo shutuma zake?
 
Ndugu zangu wana jamiiforums habari za asubuhi hii ? kwangu mimi ni mzima wa afya na nipo sawa kabisa

Sina cha kupoteza Kama mnavyoona hapo juu kwenye bandiko.

Jana jioni mida ya saa moja nikiwa kazini kwangu kuna dada ninayemfahamu kwa sura tunaishi mtaa mmoja alikuja kazini kwangu, hapo kazini kulikua na watu kadhaa wakipata huduma,

Baada ya watu wote kuondoka alinifata huyo dada akanieleza kwa uchungu mkubwa kuwa "mke wako anatembea na mme wangu mwambie mkeo aachane na mme wangu" maneno hayo aliyatamka kwa kuyarudiarudia na mpaka machozi yakamtoka

Kuna watu wakatokea pale kupata huduma yule dada akaondoka sikupata nafasi ya kuzungumza nae kiundani ili kujua mke wangu alitembea na mme wake lini, na nimeshindwa kuchukua hatua yoyote mpaka sasa nashindwa nianzie wapi, inavyoonekana mpaka dada huyu kulia kwa uchungu mbele yangu itakuwa kweli mke wangu anatoka kweli na mmewake

Ndugu zangu hili suala ni zito kweli kwangu nianzie wapi, majibu sina. Nimeamua kulileta hapa mimi kijana mwenzenu mnipe mawazo nifanye nini nimetuliza akili yangu sijakurupuka ila hatua ya kwanza nimeona nililete hapa.


Asanteni
Yuda_exalioth
Jamiiforums_Geita
Na Wewe ukamuacha?!.. dahh
 
Pole sana mkuu kwa maumivu unayopitia kipindi hiki kigumu. Hongera na endelea kutuliza akili. Usipaniki,acha akili itawale maumivu na hisia ulizokuwa nazo kwa wakati huu. Inawezekana kabisa mkeo sio muaminifu na wewe Kwa sababu upo bize au unakuwa kazini anapata muda kufanya huo uasherati. Na kama hauna tabia ya kujichanganya na watu inakuwa ngumu kupata taarifa za uzinzi wa mkeo. Mtafute kwa siri huyo dada ukae nae sehemu umdadisi kiundani akupe mkanda mzima. Na pengine kama Kuna ushahidi basi akupe Ili ukusaidie kufanya maamuzi yaliyo sahihi.

Though if the case is true.. breaking up is necessary ,vise versa is also is a decision. Considering the options and reasons available. Ni ngumu kuishi na mwanamke mzinzi.

Pole sana mkuu
 
Huenda huyo dada mumewe ni mkorofi ndio maana kakimbilia huko atakuwa ameshindwa kupata ushahid ikiwa watakana atafute ushahid kwanza
kama ni hivyo jamaa awasiliane na dada pasipo wazinzi kustuka, liandaliwe fumanizi
 
Kwakweli ni shida
Kunarafikiyngu Jana wameachana na mkewe mke kasomba vitu vyote vya ndani ndoa Ina miak 2 na ni ya kanisani nimemuonea huruma sana
Kataa Ndoa Wana hoja wakat mwingine
Kwa hiyo wasikilizwee... Haya mwakilishi wa Wakataa Ndoa Una la kuongezeaaa, mpeni maiki jamani 😂
 
Matatizo mengi ya ndoa ni matokeo ya msingi au mwanzo mbovu. Hapo usipokuwa makini hata huyo dada aliyekuletea kesi, ukimuweka karibu utatoka naye.

Atakuwa anasema ukweli. Wanawake anasense kali sana. Ongea na mke wako. Mwambie aache hiyo tabia bila kujali anabisha au la. Ila baada ya kujiridhisha.
Mwambie ukweli akiendelea baada ya katazo hilo, akaolewe na huyo jamaa.

Usizunguke sana.
 
Kwa Nilivomuona rafiki yangu nimeanza kuwaelewa kataa Ndoa😀😀 jamni ndoa mpya mtu anaondoka na vitu vyote vya ndani inamaana kamuacha na Bado aanze Tena maisha upya
Neuro mdogowangu sijakupa hii story😀😀😀ila usijiunge kataa Ndoa
Alikuwa na shida na zamani za ndani bila shaka lengo lake limetimia 😂
 
Back
Top Bottom