Nimelitathimini jengo la Makao Makuu ya CHADEMA pale Ufipa na nimeridhika chama hicho hakijali Maendeleo ya Vitu

Nimelitathimini jengo la Makao Makuu ya CHADEMA pale Ufipa na nimeridhika chama hicho hakijali Maendeleo ya Vitu

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mara kadhaa viongozi wa CHADEMA wamesikika wakinadi maendeleo ya watu badala ya vitu. Na wakati mwingine wameibeza CCM kwa kujikita kwenye maendeleo ya vitu ( miundombinu)

Ndiposa leo nikapata bahati ya kufika mtaa wa Ufipa hadi pale makao makuu ya chama hiki kikuu cha upinzani. Kimsingi nimekubaliana nao kwamba wao hawaamini katika maendeleo ya vitu maana jengo na samani za ofisini zinadhihirisha hilo.

Ni ukweli ulio wazi kama CHADEMA ingechaguliwa 2015 haya maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ikiwemo SGR, Bwawa la umeme Fly overs, ununuzi wa ndege nk. ingekuwa bado ni ndoto kwa watanzania.

Niishie hapo.

Maendeleo hayana vyama!
 
Tatizo kila mwenye jengo anaogopa kumkodishia chadema jengo kwa ajili ya ofisi kwa kuogopa fitna za serikali

Nina mfano halisi, Chadema walitaka kukodisha jengo zima la mtu fulani pale maeneo ya kijitonyama, mwenye jengo alikua na shida kweli ya pesa lakini alipoambiwa mpangaji ni chadema akasema serikali haitoniacha ngoja jibaki na shida zangu
 
Chadema baba lao , ccm imerithi ofisi Zote za TAA na za TANU ,sasa Lumumba imejengwa lini ?ukum@ unawasumbua ccm
 
Picha tafadhali, sisi wa mwamagigisi tupate taswira ya makao makuu
 
Tatizo kila mwenye jengo anaogopa kumkodishia chadema jengo kwa ajili ya ofisi kwa kuogopa fitna za serikali

Nina mfano halisi, Chadema walitaka kukodisha jengo zima la mtu fulani pale maeneo ya kijitonyama, mwenye jengo alikua na shida kweli ya pesa lakini alipoambiwa mpangaji ni chadema akasema serikali haitoniacha ngoja jibaki na shida zangu
Wajenge majengo yao.
 
Ile ni nyumba ya makuti tu,mbowe anaswaga 326m za ruzuku kila mwezi plus michango ya wabunge wa chadema,kujenga ofisi hata yenye ukubwa wa banda la kuku imeshindikana 😃😃😃
 
Wekeni picha nami nione. Kila siku mnalalamikia ofisi hizo na sijawahi ziona.
 
Chadema ni genge la wakora ,wakuogopwa kama ugonjwa wa ukoma,hawafai,ni majambazi,majizi,matapeli
 
Back
Top Bottom