Nimelitathimini jengo la Makao Makuu ya CHADEMA pale Ufipa na nimeridhika chama hicho hakijali Maendeleo ya Vitu

Nimelitathimini jengo la Makao Makuu ya CHADEMA pale Ufipa na nimeridhika chama hicho hakijali Maendeleo ya Vitu

Sababu ya hao wengine kua na jengo kubwa la ghorofa, ni kutapeli wananchi. Kudhulumu rasilimali za taifa, na unyonyaji uliopitiliza!
Hivi michango yenu mnayochangisha huwa mnapeleka wapi?
 
Nyie mna majengo ya aina hiyo ila sera mbovu, hivyo hamna faida kwa nchi.

Korea waliopigana vita mwaka 1954 na tukawa tunawazidi kiuchumi, mwaka 1958 walikuwa na hali mbaya, ila leo wanatengeneza simu za Samsung huku Tanzania chini ya CCM kwa miaka 60 sasa, inahangaika na matundu ya choo-John Heche.

kila wanaposema makao makuu lazi uumie, dawa yake ni kujenga tu
 
Miaka yote hiyo kumbe mnatokea hapa[emoji23], nimesikia mnazindua CHADEMA Digital Marekani na bado makao makuu ni hapa.
KAMA HAMJAWEZA KUJENGA OFISI MTAWEZA KUJENGA NCHI?
View attachment 1884546
Mmesahau kuwa ubora wa chama ni uungwaji mkono na watu sio majengo.

Ata ivyo mmejimilikisha mali za umma,mmeiba, mnafisadi nchi na sasa mnatamba! Soon mtavitapika,uzuri ni kwamba hayo majengo na viwanja mlivyojimilikisha hamuwezi kuhamisha ivyo vitataifishwa soon.
 
Sasa hawa ndio wanataka wapewe nchi. Tutafika kweli.
Acha CCM iendelee kutawala mpaka Upinzani utakapokuwa na akili
Kupewa nchi kigezo ni kuungwa mkono na raia sio uwingi na ubora wa majengo.

Ata Nyerere alipewa nchi kwa kuungwa mkono na raia maana wakati ule majengo bora yalikuwa ya mkoloni,TANU haikuwa na kitu cha maana.
 
Majengo mazuri
Magari mazuri

Huku mwananchi hana maji na shule hazina vyoo nini raha yako
 
Kupewa nchi kigezo ni kuungwa mkono na raia sio uwingi na ubora wa majengo.

Ata Nyerere alipewa nchi kwa kuungwa mkono na raia maana wakati ule majengo bora yalikuwa ya mkoloni,TANU haikuwa na kitu cha maana.
Sawa hio iliwezekana kwa sababu ni uhuru ulikuwa unapiganiwa. Sahvi tunataka kujenga nchi na maendeleo.
Sasa kama chama chenu mmeshindwa kukijenga wala kukiletea maendeleo. Mmatushawiehi vipi tuamini kama mkipewa nchi mtafanya vizuri.
Maana japo ya kiasi kidogo mnachopewa mmeshindwa hata kuboresha ofisi zenu. Mnajali tu matumbo yenu. Itakuwaje mkipewa nchi.
Kama chama inabidi muwe na mikakati inayoonekana.
 
Ofisi za kisasa kabisa zipo mioyoni mwetu... CDM ni imani.
 
Mara kadhaa viongozi wa CHADEMA wamesikika wakinadi maendeleo ya watu badala ya vitu. Na wakati mwingine wameibeza CCM kwa kujikita kwenye maendeleo ya vitu ( miundombinu)

Ndiposa leo nikapata bahati ya kufika mtaa wa Ufipa hadi pale makao makuu ya chama hiki kikuu cha upinzani. Kimsingi nimekubaliana nao kwamba wao hawaamini katika maendeleo ya vitu maana jengo na samani za ofisini zinadhihirisha hilo.

Ni ukweli ulio wazi kama CHADEMA ingechaguliwa 2015 haya maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ikiwemo SGR, Bwawa la umeme Fly overs, ununuzi wa ndege nk. ingekuwa bado ni ndoto kwa watanzania.

Niishie hapo.

Maendeleo hayana vyama!
Chama ni watu(wanachama) sio majengo.

TANU haikuwa na majengo ya maana ukilinganisha na mkoloni wakati huo,lakini TANU kumuondoa mkoloni ni sababu ya watu sio majengo,muwe na akili kidogo.

ASILIMIA 90 YA MAJENGO YA CCM NI MALI YA UMMA.
 
2016 mpaka 2020 Chadema walipata ruzuku zaidi ya bilioni 20. Bilioni 2 tu wangejenga ofisi zenye hadhi yao. Ni kitendawili hadi leo wako ufipa. Hata hapo ufipa nahisi kama si juhudi za Mzee Ndesamburo pengine hawangenunua.
 
Aibu tupu, Makao Makuu ya CDM, hivi swali dogo tu, ikiwa hata ofisi Chadema hawawezi jenga, chadema watabomoa kabisa nchi badala ya kujenga.
Hata kiwanja hawana achilia mbali hiyo plan ya jengo
 
Mara kadhaa viongozi wa CHADEMA wamesikika wakinadi maendeleo ya watu badala ya vitu. Na wakati mwingine wameibeza CCM kwa kujikita kwenye maendeleo ya vitu ( miundombinu)

Ndiposa leo nikapata bahati ya kufika mtaa wa Ufipa hadi pale makao makuu ya chama hiki kikuu cha upinzani. Kimsingi nimekubaliana nao kwamba wao hawaamini katika maendeleo ya vitu maana jengo na samani za ofisini zinadhihirisha hilo.

Ni ukweli ulio wazi kama CHADEMA ingechaguliwa 2015 haya maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ikiwemo SGR, Bwawa la umeme Fly overs, ununuzi wa ndege nk. ingekuwa bado ni ndoto kwa watanzania.

Niishie hapo.

Maendeleo hayana vyama!
Joni mbatizaji mbona unaleta hoja yenye mawazo finyu kama vile tuko kwenye kijiwe cha kamali! Marehemu Ghadafi aliishi kwenye hema na aliweza kutupa misaada! Pamoja na kuishi ndani ya hema nchi yake ilikuwa na kiwango cha juu sana kimaendeleo, hiyo CCM na majengo unayoyapigia chapuo yalijengwa kwa fedha za umma na tulipoingia mfumo wa vyama vingi ikapora, leo wewe unasifia wizi! Haufai kuwa mbatizaji.
 
Back
Top Bottom