Nimelizwa, nimeumizwa na kufadhaishwa mno na kifo cha kijana huyu

Nimelizwa, nimeumizwa na kufadhaishwa mno na kifo cha kijana huyu

Daah poleni sana. Sijui mwisho wa hiyo vita lini
80% ya binadam wa miaka hii wana roho mbaya na ngumu zaidi ya shetan mwenyewe. Fikiria kumchoma mtu aliekuwa ndan kalala, hajamshikia mtu kisu wala bunduki. Hii inaonesha ni jinsi gan binadam wengi wasivyokuwa na huruma kwa wengine.
 
Daah poleni sana. Sijui mwisho wa hiyo vita lini
Kinachoiponza kongo ni rasilimali zake. Pale kila taifa kubwa linachaka lake la kuchimba madini na rasilimali mbalimbali.
Mfano Marekani wanachaka la dhahiri kupitia mikataba ya serikali na la siri kupitia vikundi kama hivi vya M23, Halikadhalika Wingereza, Ufaransa, Belgium na wengineo.

Solution ni serikali kuwatafutia raia wote wanaoishi maeneo yenye rasilimali na madini maeneo mengine ya mijini kama vile Kinshasa, Lubumbashi nk. Afu hayo maeneo waachie hao wanaochimba wachimbe na kuipatia serikali kiasi chochote watachoona hao wakubwa kinawafaa. Bila hivyo wataendelea kufa miaka kwa miaka.
 
😭😭😭😭 RIP asee!
Siku nikiwakamata hawa rebels nawepelekea moto
Hawa ilitakiwa wakikamatwa linachimbwa shimo kubwa, watu wanajaza kuni, zinawashwa afu wanadumbukizwa humo shimoni wapuuzi hawa.
 
M23 wanasababu za msingi kufanya mashambulizi, wamenyanyasika miaka yote kutoka serikali ya Congo na hata wananchi pia, kiasili M23 inaundwa na watutsi wenye asili ya rwanda ila walijikuta Congo baada ya wazungu kuigawa Afrika, kwahiyo serikali ya Congo haiwakubali Kama Ni wakongo halisi na wanatengwa kuanzia huduma za kijamii Hadi kwenye ajira, Kabila snr aliwatumia kipindi anaingia madarakani kwa ahadi kuwa atawajumuisha kwenye jeshi la serikali ila alipoingia madarakani akawageuka, ndio maana hao waasi wamekua wakibadili majina ila malengo yao Ni yaleyale.
 
Mfano Marekani wanachaka la dhahiri kupitia mikataba ya serikali na la siri kupitia vikundi kama hivi vya M23,
Halafu kuna watu bado wanaisifu Marekani eti imeendelea....wakati imejengwa kwa kumwaga damu za wasio na hatia kama Jems.

Putin pambana na hawa wauaji...usiposhinda wewe atashinda mrithi wako.
Haki ni lazima itasimama, hata kwa kuchelewa.
R.I.P James.
 
Dah pole sana mkuu. Naungana na wewe katika maombolezo haya. MUNGU ampe pumziko la milele yeye familia yake pamoja na msamaria mwema Rama.
 
M23 wanasababu za msingi kufanya mashambulizi, wamenyanyasika miaka yote kutoka serikali ya Congo na hata wananchi pia, kiasili M23 inaundwa na watutsi wenye asili ya rwanda ila walijikuta Congo baada ya wazungu kuigawa Afrika, kwahiyo serikali ya Congo haiwakubali Kama Ni wakongo halisi na wanatengwa kuanzia huduma za kijamii Hadi kwenye ajira, Kabila snr aliwatumia kipindi anaingia madarakani kwa ahadi kuwa atawajumuisha kwenye jeshi la serikali ila alipoingia madarakani akawageuka, ndio maana hao waasi wamekua wakibadili majina ila malengo yao Ni yaleyale.
Mkuu mbona hii historia inaonekana kupishana na zingine zinazodai kwamba watutsi walikimbilia huko miaka ya 60 hadi 70 kukwepa mauaji yaliokuwa yanasababishwa na serikali ya Rwanda iliyokuwa inaongozwa na wahutu.
Kama historia ingekuwa ni hiyo ya mipaka ya wakoloni basi tusingeona watutsi peke yake, bali tungeona na wahutu pia waliokuwa wakiishi maeneo hayo.
Sasa basi inasemekana baada ya kufika huko kama wakimbizi, walipewa haki zote za kikimbizi, baada ya kuzaliana na kufuata taratibu za kiichi ikabidi baadae na wenyewe wawe muongoni mwa makabila ya Congo.
Sasa wakati wa vita vya kumng'oa Mobutu, Kabila baba aliwatumia wanyarwanda original (jeshi la Rwanda) lililokuwa na watutsi wengi enzi hizo na waganda.
Baada ya vita vile ikabidi itokee kutokuelewana kati ya Kabila na viongozi wa hizo nchi nilizotaja kuhusu makubaliano yao. Sasa ndo hapo serikali ya Rwanda ikaamua kuwatumia hao vijana kama ngao ya kile wanachokitaka kutoka Congo, waganda nao wakawa upande wa hao waasi wengine ambao leo wanajifanya wako nchini Congo kupambana nao. Lkn yote hii inaonekana kuna mkono wa mataifa kabwa yapo nyuma yao ambayo yamekuwa yakiwapa hao waasi silaha kupitia hizo nchi nilizosema hapo juu kwa ajili ya masilahi yao.

Hata hivyo waasi hao walitakiwa wapambane na wanajeshi wa serikali ambao wanasilaha, na wale raia ambao wana uhakika kwa namna moja au nyingine kuwa wanatumika na serikali. Ila sio kuvamia sehem na kuuwa kila mnaemkuta hapo hata kama mtu mwenyew hana silaha yoyote au hana kosa lolote.
 
Dah pole sana mkuu. Naungana na wewe katika maombolezo haya. MUNGU ampe pumziko la milele yeye familia yake pamoja na msamaria mwema Rama.
Amiin mkuu, shukran sana kwa dua yako
 
Fikiria mtu unamchoma moto binadam mwenzako ambae hajakufanya chochote na hana silaha yoyote ya kukudhuru.
Tatizo la hizi terrorist groups hazina malengo yanayoonekana, unakuta wapo Mia tatu tu na AK-47 zao wakivuta drugs wanajiona wako milioni kumi, then wanataka waichukue Nchi nzima ya DRC?
 
Tatizo la hizi terrorist groups hazina malengo yanayoonekana, unakuta wapo Mia tatu tu na AK-47 zao wakivuta drugs wanajiona wako milioni kumi, then wanataka waichukue Nchi nzima ya DRC?
Hahaha.. mkuu Katumbasongwe mi nafikiri haya makundi hayana lengo la kuchukua nchi maana uwezo wa kuongoza serikali hawana, lkn pia wanajua wakichukua nchi watatokea waasi wengine kuisumbua serikali yao kam wao wanavyoisumbua serikali ya wenzao.
Hawa jamaa lengo lao kubwa ni kumiliki maeneo yote muhimu yenye rasilimali za nchi kama vile maeneo ya kuchimba madini, gesi, mafuta na yale yanayopatikana sijui mchanga wa kutengeneza vifaa vya sim na mabetri. Hayo ya kuchukua nchi hayana umuhimu wowote kwao, ndio maana hauwezi kusikia wamepigana maeneo mengine mbali na yale ya madini.
 
Apumzike kwa Amani kijana Jems
Halafu bado kuna nchi wanawatetea hao M23 na kununua/kuchukua madini kutoka kwao hakina hizo ni fedha za damu fedha Chafu damu za watu zinalia

Tunashangaa sana nchi za NATO Kugoma kununua mafuta/gas ya Urusi mafuta yale na gesi fedha zake ndio zinatumika kuwalipa wanajeshi wanaoua na kubaka wamama/wadada Ukraine

Tukatae vita,tuiombee nchi yetu tudai haki zetu kwa njia ya amani ila sio vita wanandugu
 
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.

Kabla ya yote, ningependa niweke wazi kuhusu jinsi nilivyofahamiana na huyu kijana kupitia uncle wake ambae niliwahi kufanya nae kazi katika kampuni fulan, miaka kadhaa iliyopita.

Kijana ninaemzungumzia hapa anaitwa Jems, na huyo mjomba wake ambae alikuwa rafiki yang alikuwa anaitwa Ramadhan. Ilikuaje hadi kufariki kwake, naomba unifuatilie hapo chini.

Jems ni kijana aliezaliwa mwaka 1997, katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo. Alikuwa mtoto wa kwanza katika familia ya watoto wa tatu, ambapo waliomfuata kwa kuzaliwa alikuwa mwanaume pia alieitwa Janvier (January) na wa mwisho mwanamk alieitwa Julieta.

Mwaka 2011, waasi wa M23 walivamia kijiji chao na kuuwa makumi ya wanavijiji. Hali hiyo ilipelekea Jems, ndugu zake na wazazi wake watoroke kwao ili kwenda kutafuta hifadhi sehem nyingine. Kwa vile ilikuwa usiku, basi Jems akapoteana na wazazi wake pamoja na ndugu zake.

Jems akakimbilia katika kambi ya ndan nje ya kijiji chao, ambapo alikutana na huyu rafiki yang alieitwa Ramadhan ambae alikuwa amekwenda kwao kutembea na kukutana na mkasa huo siku chache baada ya kufika.

Huyu rama hakuwa na undugu na Jems, lkn alijikuta anaguswa na yaliomkuta huyo dogo ambae tayari alikuwa ashapoteana na wazazi wake.

Baada ya kukaa kambini kwa muda, waliamua kukimbilia Tanzania kambini mkoani Kigoma ambapo walikaa kwa muda wa miaka miwili na nusu.

Mwaka 2014, Rama na dogo Jems wakaanza safari ya kuja Kaburu kutafuta hifadhi ya uhakika. Ikumbukwe Rama tayari alikuwa ni mkazi wa huku, ila alikwenda kwao kusalimia na kuona familia yake. So njia za kufika Kaburu alikuwa anazijua na pesa kidogo alikuwa nayo, ingawa nyingine pamoja na vitu aliviacha baada ya uvamizi ule wa ghafla wa waasi.

Baada ya kujikongoja na kijana wake huyo waliejuana nae njiani, mwaka 2015 wakafanikiwa kuingia Kaburu.

Baada ya kufika rama alianza kazi kama kawaida, ila Jems kwa vile alikuwa mgeni ilibidi aanze kwanza kukaa nyumban mpaka pale vibali vyake vya ukimbizi vitakavyokuwa tayari.

Baada ya vibali kuwa tayari Rama alimuuliza Jems kuwa anataka asome au afanye kazi, Jems akachagua kusoma. Basi Rama akafanya makeke dogo akafanikiwa kupata shule.

Baadae dogo akawa anasoma huku anajifunza kazi nyingine ya mkono (kunyoa)

Muda wote dogo hakuwa na amani moyoni mwake, maana hakuwa anafahamu mustakabali wa wazazi wake kwamba wamefariki au wako hai somewhere.

Mwaka 2019, akabahatika kupata mawasiliana na familia yake, kumbe inasemekana wazazi walikimbilia Uganda na baadae wakarudi, ila mdogo wake wa kumfuata Janvier alikuwa ameuwawa katika uvamizi mungine uliofanywa muda mfupi na waasi baada ya wazazi wake hao kurejea nyumbani toka ukimbizini Uganda.

Dogo alilia kwa uchungu mkubwa, ila sisi kama wajomba zake tulikuwa na kazi ya kumtuliza na kumliwaza.
Rama alimpenda, alimthamini na kumjali huyu dogo kama vile mtu anavyomjali mtoto wake au ndugu yake wa damu.

Hakuwahi kumbagua kwa lolote, na hata dogo Jems na yeye alipoanza kuongea na wazazi wake aliwambia kuhusu ambae alikutana nae njiani na kuamua kumsaidia kama mtoto wake au mtoto wa ndugu yake, kiasi kwamb wazazi waliguswa na msaada ule wa Rama na kuahidi siku atakayokwenda tena Congo kutembea watamwalika kwao na kumfanyia sherehe kubwa kama vile ndugu yao.

Mambo yalibadilika mwaka 2021, baada ya Rama kupatwa na maambukizi ya korona ambapo alifariki muda mfupi tu baada ya kufikishwa hospital. Kilio kile kilikuwa cha wote, lkn kilimuumiza zaidi Jems ambae kwake yeye Rama alikuwa ni sawa na mzazi wa kumzaa.

Baada ya kilio kuisha huku tukiendelea kumueleza kwamba ile ni kazi ya Mungu na kamwe huwa haina makosa. Basi ikabidi akubaliane na matokeo kwamba kweli Mungu amechukua kilicho chake. Dogo akakonda na kupoteza nguvu za mwili kutokana na kuwaza sana juu ya kifo cha uncle wake Rama.

Hajakaa sawa, mwaka huu miezi ya mwanzo akapokea tena taarifa kuwa wazazi wake wote wawili pamoja na dada yake waliuwawa na waasi huko Congo.

Wazazi waliuwawa kwa mapanga, huku dada yake akiuwawa kwa maumivu ya kubakwa na kundi la waasi hao.
Hapo ndo dogo alipotaka kuwa chizi kabisa, ilihitaji kazi ya ziada kutoka kwetu ili kumuweka dogo katika hali ya kawaida.

Ilifika kipindi mpaka tuliona dogo anaweza kujiuwa mwenyew, kwahiyo watu tukaamua awe anaishi na dogo mungine (rafiki yake) katika nyumba aliyokuwa anaishi na marehem Rama ambae alichukua nyumba nzima (flat) na kuweka wapangaji katika vyumba vingine.

Baada ya miezi kadhaa dogo akaomba tumsaidia kumchangia changia ili arudi kwao Congo maana haoni tena sababu ya kukiogopa kifo au kuishi mbali na kwao. Wengi tulijaribu kumsihi kuwa abaki tu huku maana kule hali bado haijawa shwari, lkn yey alikataa kwa madai kuwa wazazi wake waliacha nyumba na mifugo kwahiyo kwa sasa hajui ni nani anaeiangalia nyumba na mifugo hiyo.

Akasema ni bora aende akafanye mpango wa kuuza hiyo nyumba afu atafute nchi nyingine ya kwenda kama ni kurudi huku au aende Tanzania, au Kenya au Uganda.

Baada ya kuona dogo ashapoteza muelekeo wa kuishi au wa maisha ikabidi tukubaliane na ushauri wake, ila tulimtaka auze nyumba na kuwahi kutoka kabla wale jamaa hawajavamia tena kijiji chao, akakubali. Tukachanga ikapatikana kiasi fulan cha hela ambayo ilimsaidia nauli na nyingine ya kuanzia maisha huko aendako.

Dogo alisafiri na kufika kwao salama, na muda mwingi tulikuwa tunawasiliana nae na kushauriana mambo mbali mbali ya kimaisha.

Wakati akiwa katika mchakato wa kupata mteja wa kumuuzia nyumba, ghafla kijiji kikavamiwa na waasi tena ambapo yeye alikuwa ni mmoja wa waliouwawa na waasi hao.

Sisi tulipokuwa tunamtafuta tulimkosa, tukajua labda dogo amepoteza sim, au ashauza ila yuko njiania anakuja.

Ghafla tukapata taarifa kutoka kwa aliekuwa jirani yao ambae alikuwa anafamiana na mkongo mmoja anaeishi huku, kwamb Jems aliuwawa kwa kuchomwa moto na waasi hao akiwa ndani ya nyumba yao amelala usiku. Ni mauaji ambayo yamechukua maisha ya wakongo wengi katika eneo hilo.

Baada ya taarifa hiyo ki ukweli nilijukuta nalia bila kujijua. Dogo amepitia changamoto nyingi za maisha na sasa mwisho wake umekuwa wakusikitisha zaidi.

Walaaniwe hawa waasi wa M23 na wengineo wanaouwa maelfu ya raia wasiokuwa na hatia huko Congo na ulimwenguni kwa ujumla. Dah nimejikuta sina cha kuongea zaidi ya kumtakia pumziko jema dogo Jems.

Inna lillah wainna illayhi rajiun (Sisi wote ni wa Mungu, na kwake Mungu tutarejea)

Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Mungu ailaze roho yake na wazazi wake mahali pema peponi amiin.
Hayo majitu siku ukifanikiwa kulikamata hata moja wapo Kwanza mnalitafuna 071 ndio mnalichoma kama kiazi wallah
 
Halafu kuna watu bado wanaisifu Marekani eti imeendelea....wakati imejengwa kwa kumwaga damu za wasio na hatia kama Jems.

Putin pambana na hawa wauaji...usiposhinda wewe atashinda mrithi wako.
Haki ni lazima itasimama, hata kwa kuchelewa.
R.I.P James.
Hawa watu wanaangamiza maisha ya maelfu ya watu wasiokuwa na hatia kwa faida zao wenyewe.
 
Apumzike kwa Amani kijana Jems
Halafu bado kuna nchi wanawatetea hao M23 na kununua/kuchukua madini kutoka kwao hakina hizo ni fedha za damu fedha Chafu damu za watu zinalia

Tunashangaa sana nchi za NATO Kugoma kununua mafuta/gas ya Urusi mafuta yale na gesi fedha zake ndio zinatumika kuwalipa wanajeshi wanaoua na kubaka wamama/wadada Ukraine

Tukatae vita,tuiombee nchi yetu tudai haki zetu kwa njia ya amani ila sio vita wanandugu
NATO ndio chanzo cha yote yanayotokea Congo, Nigeria, Libya na kwengineko.
Wao wanawapa waasi silaha na vijihela kidogo vya kula, na waasi wanawapa wababe hao wa dunia madini, mafuta, gesi na rasilimali zingine wanazopata kutoka katika maeneo yao wanayoyateka.
 
Inasikitisha sana, kuna siku niliwahi kusafiri na Mcongo aisee jamaa wanapitia mengi sana
 
Back
Top Bottom