Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 7,799
- 14,215
- Thread starter
-
- #41
Wanashindwa kupambana na wenye silaha wenzao, wanahamishia mashambulizi yao kwa raia wasiokuwa na uwezo wa kujitetea hata kwa kisu.Waasi wa kishenzi sana.
Walipaswa wapigane na wanajeshi sio Raia wasioweza jitetea
Hao M23 hua wanavuma sana ila waasi makundi yapo mengi kuleHivi wameshi kuwadhibiti m23 mpka leo ?
Haya majitu mauaji yanatia hasira sana ki ukweli.Hayo majitu siku ukifanikiwa kulikamata hata moja wapo Kwanza mnalitafuna 071 ndio mnalichoma kama kiazi wallah
Hawa watu wengi wao hawajawahi kuwa na furaha ya kudumu maana kila siku wanauwawa wanatekwa na kuteswa.Inasikitisha sana, kuna siku niliwahi kusafiri na Mcongo aisee jamaa wanapitia mengi sana
Ya ni kweli mkuu, ila hawa wanavuma kwa sababu mashambulizi yao sio ya kitoto na wakivamia sehem basi ujue hakuna cha mswalie mtume hapo. Ni kuchinja na kuchoma watu moto kwenda mbele.Hao M23 hua wanavuma sana ila waasi makundi yapo mengi kule
Daah kumbe pamoja na mseto wote wa majeshi jumuiya ya Afrika mashariki bado wamewashindwaHao M23 hua wanavuma sana ila waasi makundi yapo mengi kule
Kumbe maana nilikuwa najiuliza sanaMkuu hawa M23 wana backup kubwa nyuma yao wakiwemo wababe wa dunia. Sasa sio rahisi kuwadhibiti au kuwamaliza kama tunavyofikiria.
Hili hata Umoja wa mataifa wanalitambua lkn hakuna mtu ambae yuko tayari kuliongelea kwa kuhofia usalama wake na wa nchi yake.
Yani mkuu kuna watu wanapitia maumivu makali kuanzia mwanzo hadi mwisho wa maisha yao.Poleni mkuu, hii ni mitihani ambayo binadam wengi huipitia.
RIP to Jems na wazazi wake.
Dah aisee. Hiyo style ya kupasua wajawazito tumbo na kupiga watoto ukutani ilifanywa sana na wahutu katika mauaji ya kimbari kule Rwanda mwaka 1994.Niliwahi kuishi nyumba moja na mkongoman kino/mkwajuni jamaaa anasema vita sikia tu ndugu, wajawazito wanapasuliwa matumbo vitoto vidogo vinashikwa miguuni vinabamizwa ukutani na kuweka sumu ya mamba kwenye vyanzo vya maji mnakufa kama uroboto na mengine mengi nimepotezana nae papaa kitambo 2004
Sio tu majeshi ya Afrika. Pale kuna majeshi mpaka ya India, Pakistan sijui Brazil nk walipelekwa kwa mgongo wa Monusco lkn wamechemsha. Tatizo ni kwamba jamaa wana backup kubwa sana kutoka kwa wababe wa dunia, ambao ndio huwa silaha na mafunzo ya kijeshi kupitia jeshi la nchi fulan ya jirani. Wababe hao wa dunia wamekuwa wakiwapa wapiganaji hao hela ya kula na silaha za kupambana, huku waasi hao nao wakiwapa wababe hao madini mbali mbali kama vile almasi, dhahabu, mchanga wa kutengeneza vifaa vya sim, betri nk.Daah kumbe pamoja na mseto wote wa majeshi jumuiya ya Afrika mashariki bado wamewashindwa
Hilo haliwezekani na lisingewezekana.Kongo ingelikuwa nchi tajiri sana kama serikali ingeweza kudhibiti rasilimali zake pamoja na vikundi vya waasi.
dah inasikitisha raia ndio wanaopata tabuHilo haliwezekani na lisingewezekana.
Congo ilipata uhuru wake huku wazungu wakiwa wameshajigawia maeneo yao ya kuchimba madini, gesi asilia nk.
Ndio maana tangu mwanzo wa uhuru, mpigania uhuru wa nchi hiyo na waziri mkuu wa kwanza mweusi hayati Patrick Lumumba alipotaka kutengeneza udhibiti wa rasilimali hizo aliuwawa kifo cha kutisha, tena aliuliwa na jeshi la nchi yake mwenyew ambayo aliipigania hadi uhuru.
Jeshi hilo lililoongozwa na Mobutu halikutaka kujali au kujua ni jinsi gani Lumumba alikuwa tayari kuweka maisha yake hatarini kwa ajili yao na nchi yao.
Walichofanya ni kumuuwa ili wazungu waendelee kuchota bila bughuza yoyote.
Kabila baba alipoingia nae alitaka kuleta za Lumumba matokeo yake akauwawa kiwepesi wepesi na mlinzi wake mwenyewe.
Toka wakati huo ikaamulika kama mbwai na iwe mbwai, watu waibe na nchi isitawalike maeneo fulani, ili iwe ngumu kuwadhibiti wanaotorosha madini yao.
Ya ni kweli raia ndio wanaoteseka. Ingetafutwa mbinu nyingine ya kuwaachia jamaa wachote, huku raia wanaoishi maeneo hayo wakihamishwa maeneo mengine salama kama vile Kinshasa nk. Ila wawambie waibaji wawe wanawapa hata angalau 30% tu ya kusaidia badget ya nchi.dah inasikitisha raia ndio wanaopata tabu