Nimemchukia mke wangu

Nimemchukia mke wangu

Mkuu hujaona kama jamaa ana matatizo?
kumchukia mtoto sababu pekee ikiwa ni kutokufanana kwa sura?

kukubali kupangiwa siku za kusex unahisi imesababishwa na nini?

kutafuta furaha yake kwa michepuko na kuhonga nusu ya mshahara wake!

Sidhani kama unafahamu jinsi inavyouma unavyohisi mtoto siyo wako? Labda nikugusie kidogo,humchukii mtoto,ila kama baba roho inakataa kuwajibika kwa kupenda,unakuwa unaforce kwa vile mahitaji mengine ni muhimu kwa mtoto.
 
Habarini wanajamvi, kama tittle inavojieleza, sina amani ndani ya ndoa kwanmda mrefu sasa najikuta nina stress hadi afya imeanza kuzorota.
Nipo kwenye ndoa mwaka wa 10 sasa, nlifurahia mapenzi ya mke kwa miaka 2 tu ya kwanza ya ndoa. Wakati namwoa mke wangu alikuja na mtoto ambaye alidai ni wa kwangu nami nikampokea, ila kadri siku zinavyosonga namwona kabisa mtoto huyu sio dam yangu kwani hana anachofanania na mimi tofauti tu na tabia kachukua za kwangu , nisichokula naye hali, si kwa kuniiga bali vinakuja natulary. Kingine sina ile parental feeling na huyu mtoto, yaan naweza kumpenda mtoto wa ndugu yangu zaidi kuliko huyu mwanangu, nimempeleka boarding school yaan hata sifikirii kana nina mtoto huko japo nawajibika kwa kila kitu, Amezaliwa mtoto wa 2 mwaka jana ni binti, huyu wala hina swali anafanana na mimi kama mayai, and ninampenda kiasi hata cha kutoa uhai wangu nikampa, huyu kunamda nakaa nimemwangalia tuuu hata sijui naangalia kitu gani.
Kingine nlichoanza kupata machungu ni kunyimwa papuchi, hii ilianza mwaka wa 2 wa ndoa nikawa napangiwa weekend tu ndo napewa, ilileta ugomvi sana, yy akaenda chuo ambacho ninkama 50km toka tunapoishi kwa makubaliano kuwa kila weekend aje, matokeo yake akawa anakuja kwa mwezi na baadae akawa anakuja wakifunga. Nikaona isiwe shida nikawa namfuata huko. Baadae napo ikaonekana ruhusa za kutoka ni shida afu anatoka na uniform kuingia gest ni tabu tu.
Nikaacha kuwa nakwenda, rafiki yanfu akanishauri nitafute mchepuko, nikafanya hivo hadi nikamsahau kabisa.
Nimeendelea hivo kwa maumivu maana sikuzoea kuchepua, baadae nikawa mzoefu nikaona ni haki yangu kuchepuka hata akinikamata nlikuwa namwambia unaweza kuondoka ama kutafuta mwanaume mwingine akuoe.
Shida nliyonayo sasa ni kuwa natumia hela nyingi sana kuchepuka karibu nusu ya mshahara wangu unaishia kwa wanawake. Sina mshahara mkubwa saaana, si wa chini pia.huwa naangalia chain ya wanawake nilokwishatembea nao ni wengi kidogo toka nlipooa. Nikiri tu kabla ya kuoa sikuwahi kufanya ngona saaaana. Yy ni kama alikuwa mwanamke wangu wa 3, hivo sikuwa na experience na wanawaka. Hata kumwoa sikuchukua mda wa kumfahamu maana tulikuwa tunaishi mikoa tofauti so tulitongozana kwenye simu tu na tukafikia hatua ya kuoana tukiwa tumekutana mara 2 au 3 hivi. Kwa ss nikihesabu nilokwisha date nao wanafikia hata 30
Sasa hivi sina hisia naye hata kidogo toka alipobeba mima alikataa kushiriki tendo la ndoa, na baada ya kujifungu sijamgusa wala kuomba papuchi na mtoto ana miezi 7sasa.

Kuna kipindi nafikiria kuoa mke mdogo niwe nao wawili, wasiwasi wangu ni dini nitatengwa hadi na ndugu zangu( hili sio tatizo kubwa sana najua litaisha kadri mda unavyoenda), ila tatizo kubwa sijapata mwanamke sahihi wa kuanzisha naye fakilia kama mke mdogo. Kila ninaokuwa nao maona sio wife material. Natamani sana kuoa mtoto wa kiislam kutoka tanga, arusha, zanzibar, au kigoma awe km mke mdogo.
kutoka na uniform tena kwani anasoma veta
 
1.Anakufumania mara kwa mara,huombi msamaha unamwambia kama anataka kuondoka aondoke,inaonesha yeye anakuvumilia ilihali umeshamchoka
2.wakati unamuoa hukuwa mzoefu sana kwenye masuala ya ngono,je unahisi unamridhisha kunako sita kwa sita?
3.kuhusu kunyimwa tendo mara nyingi inasababishwa na shoo mbovu kitandani,mwanaume mwenye shoo ya uhakika ananyimwaje sasa kwa mfano?inawezekana pia ukawa sio romantic mapenzi ni sanaa
Sikushauri kumuacha huyo mwanamke inawezekana akawa anakuvumilia kwa mengi kuliko unayomvumilia wewe
 
Sidhani kama unafahamu jinsi inavyouma unavyohisi mtoto siyo wako? Labda nikugusie kidogo,humchukii mtoto,ila kama baba roho inakataa kuwajibika kwa kupenda,unakuwa unaforce kwa vile mahitaji mengine ni muhimu kwa mtoto.
unahisi na unafikia conclusion?
na je ukienda kupima ukapata mtoto ni wako? will you burn away all the pain and anger you caused to the baby and mother?
 
Habarini wanajamvi, kama tittle inavojieleza, sina amani ndani ya ndoa kwanmda mrefu sasa najikuta nina stress hadi afya imeanza kuzorota.
Nipo kwenye ndoa mwaka wa 10 sasa, nlifurahia mapenzi ya mke kwa miaka 2 tu ya kwanza ya ndoa. Wakati namwoa mke wangu alikuja na mtoto ambaye alidai ni wa kwangu nami nikampokea, ila kadri siku zinavyosonga namwona kabisa mtoto huyu sio dam yangu kwani hana anachofanania na mimi tofauti tu na tabia kachukua za kwangu , nisichokula naye hali, si kwa kuniiga bali vinakuja natulary. Kingine sina ile parental feeling na huyu mtoto, yaan naweza kumpenda mtoto wa ndugu yangu zaidi kuliko huyu mwanangu, nimempeleka boarding school yaan hata sifikirii kana nina mtoto huko japo nawajibika kwa kila kitu, Amezaliwa mtoto wa 2 mwaka jana ni binti, huyu wala hina swali anafanana na mimi kama mayai, and ninampenda kiasi hata cha kutoa uhai wangu nikampa, huyu kunamda nakaa nimemwangalia tuuu hata sijui naangalia kitu gani.
Kingine nlichoanza kupata machungu ni kunyimwa papuchi, hii ilianza mwaka wa 2 wa ndoa nikawa napangiwa weekend tu ndo napewa, ilileta ugomvi sana, yy akaenda chuo ambacho ninkama 50km toka tunapoishi kwa makubaliano kuwa kila weekend aje, matokeo yake akawa anakuja kwa mwezi na baadae akawa anakuja wakifunga. Nikaona isiwe shida nikawa namfuata huko. Baadae napo ikaonekana ruhusa za kutoka ni shida afu anatoka na uniform kuingia gest ni tabu tu.
Nikaacha kuwa nakwenda, rafiki yanfu akanishauri nitafute mchepuko, nikafanya hivo hadi nikamsahau kabisa.
Nimeendelea hivo kwa maumivu maana sikuzoea kuchepua, baadae nikawa mzoefu nikaona ni haki yangu kuchepuka hata akinikamata nlikuwa namwambia unaweza kuondoka ama kutafuta mwanaume mwingine akuoe.
Shida nliyonayo sasa ni kuwa natumia hela nyingi sana kuchepuka karibu nusu ya mshahara wangu unaishia kwa wanawake. Sina mshahara mkubwa saaana, si wa chini pia.huwa naangalia chain ya wanawake nilokwishatembea nao ni wengi kidogo toka nlipooa. Nikiri tu kabla ya kuoa sikuwahi kufanya ngona saaaana. Yy ni kama alikuwa mwanamke wangu wa 3, hivo sikuwa na experience na wanawaka. Hata kumwoa sikuchukua mda wa kumfahamu maana tulikuwa tunaishi mikoa tofauti so tulitongozana kwenye simu tu na tukafikia hatua ya kuoana tukiwa tumekutana mara 2 au 3 hivi. Kwa ss nikihesabu nilokwisha date nao wanafikia hata 30
Sasa hivi sina hisia naye hata kidogo toka alipobeba mima alikataa kushiriki tendo la ndoa, na baada ya kujifungu sijamgusa wala kuomba papuchi na mtoto ana miezi 7sasa.

Kuna kipindi nafikiria kuoa mke mdogo niwe nao wawili, wasiwasi wangu ni dini nitatengwa hadi na ndugu zangu( hili sio tatizo kubwa sana najua litaisha kadri mda unavyoenda), ila tatizo kubwa sijapata mwanamke sahihi wa kuanzisha naye fakilia kama mke mdogo. Kila ninaokuwa nao maona sio wife material. Natamani sana kuoa mtoto wa kiislam kutoka tanga, arusha, zanzibar, au kigoma awe km mke mdogo.





Vijana wenzangu mnapotea kwa kukosa maarifa, unajua makosa yako lakini au unamyoshea kidole tu mwenzako? Kwanza umenishangaza kumchukia mtoto pasipo sababu, kwanini unamchukia na kumbuka chuki haijifichi unahisi mkeo hajajua kama unamchukia mwanao chanzo cha ulofa wako kimeanzia hapo, kama huamini mtoto ni wako si kapime DNA, sipendi kuona mtu hatumii akili, ona sasa umeishia kuwa na wanawake 30 bado unasema unampenda mkeo
 
Mwanaume ndiyo nguzo katika familia, nyumba hujengwa na nguzo ila kama nguzo zikawa sio imara zikajengwa na ratio ndogo ya cement hapo hakuna nyumba, wewe ni mfano wa nguzo dhaifu, umeshindwa kuitetea familia yako umeishia kutembea na michepuko then unakuja unasema unampenda mkeo, umemtafutia visababu vingi sana ukasahau yako, mahusiano ni two way kama wewe tabia zako mbovu mkeo pia atakua na tabia mbovu tu, hujajijenga kikamilifu mwanaume ni sharti usimame na familia yako kile kiapo cha kanisani kuishi kwa raha na shida na mpaka kifo ni hukumu hiyo tayari umeshajifunga, kutafuta mke wapili unahisi umetatua tatizo, nyama ni hile hile bucha ni tofauti
 
Naona wengi wameshauri na mimi niweke mchango wangu.....
I
i. Mpende huyo mtoto wako wa kwanza wala huna sababu ya kulinganisha sijui nini wala nini; Ukimpa shetani nafasi atashinda
Huyo ni mtoto wako wala hana kosa lolote na utashangaa akaja kuwa mkombozi wa kukusaidia ukiwa mtu mzima
ii. Kuhusu matatizo yako na mkeo
Naona tatizo la msingi la ndoa yenu ni kuwa; mwanammke hana ham ya kufanya mapenzi; sasa hilo ndio ungeshuhulika nalo sio kwenda kwa michepuko;
Kuna sababu nyingi hufanya mwanamke akose ham ya kufanya mapenzi; baadhi zaweza kuwa;
1. Stress/Mawazo - umesema anasoma hivyo ujue kama shule ni ngumu kwake hawezi kuwa na ham
2. Anatumia dawa za kupanga uzazi- baadhi ya dawa hufanya mwanamke akose ham ya kufanya mapenzi kabisa
3. Kusemwa/kugombezwa - mwanamke akigombezwa gombezwa hupoteza kabisa ham ya kufanya mapenzi
4. Humtoshelezi- mwanamke hukosa ham ya kufanya mapenzi kama mwanamme anajiangalia mwenyewe/hamfikishi
5. usafi - mwanamke hukosa ham kama mwenzi anapenda kufanya kabla ya kujiweka safi (kuoga+ mswaki)
6. Kuzaa - kuna wanawake wengi tu wakizaa; hamu ya kufanya mapenzi huweza kuongezeka au kupungua na changamoto hizo zinabebwa na wanaume na wala huwasikii wakilalamika mitaani kwa kuwa niwaelewa
7. nk

Huyo bado anaonekana kuwa mwanamke mwema; mpe nafasi kabla ya kumuhukumu kumbe yaweza kuwa makosa yanatokea kwako. Fuatilia hayo na mengine unaweza ukaona wapi unakosea
 
Nashauri kwa wanaume ambao bado hawajawa tayari kuingia kwenye ndoa nashauri wasiingie maana mnaingia na kukutana na chanagamoto ndogo tu na mnayumba sana, kuna watu wana matatizo wewe kunyimwa papuchi tu tayari umeshatembea na michepuko 30,hivi hujui hormones zao za kuwa na hamu na tendo hushuka wakina mama wengi punde anapojifungua, ni scientific problem ila wewe umechukulia personal
 
Kitendo cha mkeo kukunyima haki yako ya ndoa inaonesha kuna tatizo ambalo hapa kwenye uzi wako umekataa kuandika.Umenishangaza kuweka chuki kwa mtoto kisa hajafafa nawe uzi wako kuna vitu vingi umefukia ili unekane u sahihi.
 
1.Anakufumania mara kwa mara,huombi msamaha unamwambia kama anataka kuondoka aondoke,inaonesha yeye anakuvumilia ilihali umeshamchoka
2.wakati unamuoa hukuwa mzoefu sana kwenye masuala ya ngono,je unahisi unamridhisha kunako sita kwa sita?
3.kuhusu kunyimwa tendo mara nyingi inasababishwa na shoo mbovu kitandani,mwanaume mwenye shoo ya uhakika ananyimwaje sasa kwa mfano?inawezekana pia ukawa sio romantic mapenzi ni sanaa
Sikushauri kumuacha huyo mwanamke inawezekana akawa anakuvumilia kwa mengi kuliko unayomvumilia wewe
📌📌
 
Sidhani kama unafahamu jinsi inavyouma unavyohisi mtoto siyo wako? Labda nikugusie kidogo,humchukii mtoto,ila kama baba roho inakataa kuwajibika kwa kupenda,unakuwa unaforce kwa vile mahitaji mengine ni muhimu kwa mtoto.
Unahisi vipi kama mtoto si wako hali ya kuwa mke hajawahi kuonesha dalili ya kushit maana jamaa kwenye Uzi wake hajaandika mkewe aliwahi msaliti ninachoona kwake yeye ndiye hajatulia so anahisi na mkewe alikuwa hivyo akapatikana mtoto asiyefanana nae inachekesha😃
 
Vijana wenzangu mnapotea kwa kukosa maarifa, unajua makosa yako lakini au unamyoshea kidole tu mwenzako? Kwanza umenishangaza kumchukia mtoto pasipo sababu, kwanini unamchukia na kumbuka chuki haijifichi unahisi mkeo hajajua kama unamchukia mwanao chanzo cha ulofa wako kimeanzia hapo, kama huamini mtoto ni wako si kapime DNA, sipendi kuona mtu hatumii akili, ona sasa umeishia kuwa na wanawake 30 bado unasema unampenda mkeo
Umeongea vizuri mkuu,tafadhali huyo ndugu mimi namshauri ,
1)mpende mkeo mwaka wa kumi bado mnaanza vituko,upendo uvumilia,hautafuti sababu,upendo hauhesabu makosa,upendo haukosi kuwa na adhabu,kwa nini hamwezi kusameheana?,na kurekebisha makosa yenu.!.
2)Nijuavyo mimi wakati unadhani wewe ndo una maumivu mengi,yawezekana tukimsikiliza mkeo hapa ataongea kwa machozi na majonzi mengi kuliko wewe,
3)Hakuna hasiye na makosa kati yenu kikubwa na ninauhakika kuwa chanzo cha matatizo utakuwa ni wewe kwa sababu mala nyingi sisi wanaume hatuonagi kama tunakoseaga.
4)Rudi kwa mke wako kajishushe omba msamaha ili umpe nafasi ya kufunguka yote yaliyoko moyoni mwake,
5)Usimwache mkeo kwa chochote, na kuonana na mwamke kwa mda mfupi siyo tatizo kwani kuna waliokaa kwenye uchumba zaidi ya mwaka na walipo oana wakaachana,pili usimchukie mkeo kwa sababu ya mtoto unayeisi siyo wako kwa sababu atakama si wako wewe mtunze na mhudumie tu,kwa sababu ilikuwa ni vigumu mno mkeo kukwambia mtoto si wako wakati anataka kuolewa na wewe na mda mwingine ata kama mtoto si wako haimaanishi kwamba alikuwa muhuni sana ila sherani yuko kazini kuvuruga mausiano.
6)Nitakomea hapa na kama utaitaji ushauri zaidi utani DM,Katika yote unayofanya ujue kuna Mungu mwenye kuhukumu bila ubaguzi jitaidi kumtegemea Mungu katika maamzi unayotamani kuyafanya,Kikubwa ni kuvumiliana mimi na mke wangu tuna miaka saba tu,ila tunaishi vizuri sana na hatuna Mtoto mpaka sasa na tuko vizuri,Siku ukifika mbele za Mungu atakushangaa kwani atakuletea walio pita mazito kuliko wewe.....
Kila la kheri.
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] hapa kaua tena aliletewa na mtoto juu
waliingia kwenye game wakiwa 1-0 mwenzake anaongoza kwa goli la ugenini,lazima apate moto ndoa c mchezo inahitaji wananume wa shoka walioaga kwao
 
Walipo andika " akamfanyia wakufanana nae"hamkuelewa tu?

Kosa ni lako ww mwenyewe ndio chanzk cha yote hayo. Hile ACTION ulio ionesha ya kutokumpenda/kumjari mtoto wako wa kwanza (ambaye niwa kwanza kwake) ndio ilileta yote hayo, alichokifanya yeye ni kuonesha REACTIONS kwako kwa tabia yako ya kibaguzi. Rudisha upendo kwa mtoto wako wa kwanza na yeye atakupa positive reaction kwenye mapenzi yenu.

Michepuko ni njia bora ya kusaidia kuvunja/kuharibu familia yako, usikimbilie kuchepuka kwa kuhisi unatatua matatizo yako.
Kaa nae chini muongee umwambie makosa yake na ww umpe nafasi ya kuongea yaliyo moyon mwake then msamehane muanze upya.

KUMBUKA DHAMANA YA NDOA YENU IPO MIKONONI MWENU NINYI WENYEWE
 
Yaani mwanamke aninyime K" alafu Bado naishi naye?????heeheee
 
1.wanaume mnapenda kuwa namwanamke aliyejificha tabia..yani kwenu ninyi mwanamke akishaonyesha tabia zake kabla ya ndoa mnampiga chini na kumuona hafai..kumbe ulikuwa una uwezo wa kuangalia mapungufu ya tabia kama yanatekebishika ukamwambia badilika moja mbili tatu na mambo yakaenda,so unaenda ishi na mtu angalau unamfahamu.utasikia nataka kuoa mwanamke mfia dini[emoji1]sasa hakuna wanawake wanamambo mengi kama hao(ingawa si wote)hao wakija kuufahamu ulimwengu wa nje ya kufia Dini umekwenda na maji sheikh.
Hakuna binadamu asiye na mapungufu katika hii dunia cha msingi ni kujua na namna ya kuishi na kuchukuliana.upendo na kusameheana vikitawala kati yenu.

2.hakuna haja ya kumchukia malaika wa Mungu(mtoto)bila sababu.kama una wasiwasi juu ya huyo mtoto nenda kimya kimya kacheki DNA ikijulikana si wako hakuna haja ya kuendelea na hiyo mwanamke maana huo uongo wa kukubambikia mtu mtoto umezidi levels zote.hauvumiliki.

3.hizo tabia za mkeo mpaka kufikia hapo..wewe mwanaume ndie uliyeruhusu huo ufala wote.mwanamke ni lazima aijue nafasi yake kama mwanamke sio akupande kichwani.halafu Huyo mwanamke inaonesha ana mwanaume mwingine Chief.
Kingine nyie wanaume pia jitahidini kuwa wabunifu na romantic kwa wake zenu.hata nyie huwa mnajisahau pia.mnaamini kuwa mwanamke ni kumhudumia tu na kumfanya fyoko fyoko kitandani [emoji57]

4.michepuko si suluhisho kabisa aiseh.tafuta muda wa kukaa peke yako sehemu iliyotulia(hapo usihusishe mchepuko kwenye safari yako)Hebu nenda kajitafakari kwa kina kama watoto wako ndio wanaokupa sababu ya kuishi na kufurahia maisha tafadhali tafadhali kuwa na muda nao.usiwapeleke boarding school ili upate muda sahihi wa kufurahi a nao.tafuta fuckmate ruhusu maisha yaendelee.ukiwa siriazi na mahusiano ya nje hakuna hatua kwenye maisha utapiga na hata hayo mahusiano ya nje yanamambo meusi mno..ukubali ukatae mwanaume hautakuwa peke yako kwenye maisha ya nje....

5.pole kwa changamoto unazopitia chief.aliyepewa kucha hana upele,mwenye upele hana kucha.mapenzi ya kindezi sana *****
Kipendhiiiiiiih leo nkuletee nn? Sio kwa madini haya.
 
Back
Top Bottom