Nimemshangaza mwanafunzi wangu huyu, nahofia asije akatangaza hili

Nimemshangaza mwanafunzi wangu huyu, nahofia asije akatangaza hili

Ndiyo maana wagonjwa milembe hawaonekani kumbe mko mitaani mnatumia na simu kabisa
 
Habarini natumai mu wazima vijana wenzangu kwa wazee. Mimi ni mkufunzi katika chuo fulani kikubwa hapa Dar es Salaam.

Kwa watu waleee wa teleportation astral na vikolombwezo vingine, natumai mmenielewa hapa.

Nilikuwa ofisini ni asubuhi tu muda huu huu kama dk 50 tu zilizopita, alinifuata kuhusu suala lake la course work.

Nikamuelekeza safi tu, sasa akawa anauliza maswali ambayo kwa umri na level yake ya elimu aliyofikia, ni ya kipumbavu ninaweza kuyaita hivyo.

Hivyo nikakasirika na bila kutambua nikawa naongea sauti 7 kwa wakati mmoja... alitetemeka mno yule dogo, uzuri ni kwmba nilishtuka mapema nikapunguza munkari, ilikuwa ni kitendo cha kama sec 10+ hivi.

Nashindwa kuelewa alishtuka kwa mimi kufoka wakati hakuzoea kuniona kwenye hali ile,au alishtuka kwa kuwa niliongea kwa sauto saba pasipo kujua?

Nimepata hofu mno,nimejaribu kumzuga zuga huyu dogo na naona muelekeo ni mzuri.

Kwa changamoto ya namna hii naitatuaje hasa ikitokea kwenye kituo cha kazi? Na ukizingatia kazi yenyewe inahusisha watu wengi eneo moja yaani wahadhiri na wanafunzi?

Nalikabili vipi hil endapo likiwa kubwa?
Wewe ndo yule mkufunzi ambaye dogo wa kiume alikuja kukuanzishia thread humu kwa unamtisha?
 
Back
Top Bottom