Nimemsikiliza Godbless Lema katika The Big Ajenda Star TV, yupo vizuri kichwani kuwazidi wapinzani wote hapa Tanzania

Nimemsikiliza Godbless Lema katika The Big Ajenda Star TV, yupo vizuri kichwani kuwazidi wapinzani wote hapa Tanzania

mm namuona ni mlalamikaji zaidi sio problems solver

Maani huwezi kuja laumu watumishi kulipwa pesa ndogo wakati vyanzo vyetu vya mapato vipo very limited.

Angekuja na experience ya huko alipotoka na kushauri tufanye 1, 2, 3 ili kukuza mapato yetu ili years to come tulipe maslai mazuri kwa watumishi wetu.

Tofauti na hapo lema ni mtafuta attention zisizo na maana.

..lakini kulalamika ndio mwanzo wa kutafuta suluhu ya matatizo yetu.

..ccm wanataka turidhike na hali mbaya ya uchumi ili wao waendelee kula raha na kudumu madarakani.
 
Lema ana Akili nyingi Sana Kichwani na pia ana Huwezo mzuri wa kuchambua Mambo ya kiasiasa ,kiuchumi,kijamii na kiutamaduni.


Watz Wamefungwa Akili na wanaamini umasikini ni mpango wa Mungu kumbe sio kweli .

Nimeshtushwa alipoongelea Mwalimu kulipwa lakitano na Askari police anayeanza Kazi kulipwa laki nee. Sasa kwa huu mshahara huwezi hata kujenga nyumba Wala kusomesha watoto shule za maana zaidi ya kuendelea kuwa masikini wa kutupwa.


Kiufupi Chadema wamuongezee Lema ulinzi mkali maana huyu ndo nabii mbeba maono tuliyekuwa tunamsubiri mwana wa Adam


Nillikuwa sitaki kupiga kura lakini lazima nipige kura 2025 na ntaajiandikisha Arusha badala ya Bukoba Ahsante Sana Lema.
Lema yupo vyema.
 
Back
Top Bottom