Nimemuelewa mkurugenzi TCAA hii ni ajali kama zingine japo kuondokewa na mpendwa hakuzoeleki

Nimemuelewa mkurugenzi TCAA hii ni ajali kama zingine japo kuondokewa na mpendwa hakuzoeleki

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Jana mchana nilikuwa namsikiliza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga Tanzania akielezea juu ya ajali ya ndege ndani ya Ziwa Victoria. Nikawa nasoma maoni yanayopita pembeni ya kile kioo cha kinakilishi changu.

Alionekana kama anapiga siasa zile zile tunazozizoea kuzisikia kutoka kwa watanzania pindi inapotokea ajali mbaya yenye kuondoa uhai wa nguvu kazi na wengi kati ya hao marehemu wakiwa ni vijana sana, kwa kweli inasikitisha.

Ni kilio kikubwa kumsikia Mzazi akiongea namna alivyopoteza binti zake wawili tena wakiwa katika umri wa kuzalisha wa ujana. Ni simanzi kumsikiliza kaka yake RIP Rubani akiusoma wasifu wake pale msibani. Kuna yule dada aliyetoka masomoni Uturuki na kufaulu akirudi nyumbani kuiona familia yake kabla hajaanza kuishi, akiwa kijana mdogo sana.

Maisha yanapotutoka ni muda wa kuhuzunika toka ndani kabisa ya moyo. Lakini wenye akili na hekima zinazochanganyika na busara huangalia aina ya ajali iliyotokea na namna gani huko tuendapo tunaweza kuziona kama ni historia ajali hizi.

Mkurugenzi wa TCAA alieleza kwa kina historia ya uwanja wa ndege wa Bukoba na ni ukweli kuwa ile ni ajali ya pili tangu uwanja ule ujengwe na wakoloni mwaka 1940. Pengine ajali ya tatu inaweza kutokea mwaka 2055.

Kizuri ni kwamba kuna uchunguzi wa kitaalam unaoendelea kwa sasa ili kujua kwa kina chanzo cha ajali ile ni kipi haswa, wajuaji wa whatsapp hawajabaki nyuma wametengeza video ambazo kwa kitendo kile ni kosa la jinai lakini ndio TZ yetu ilivyo kila mtu anajua kila kitu!.

Wapo wanaokuja na maoni ya serikali kununua Aerial Loaders kwamba ndege inapozama basi iweze kuinuliwa kwa haraka, ni mawazo mazuri ndio lakini maamuzi ya kina ya kitaasisi yanajumuisha uwepo wa wafanya maamuzi wengi. Na hizi ni ajali tu, hazina kinga kama wasemavyo waswahili na kiswahili chao.

Jeshi la wanamaji linaweza kupitisha bajeti ya mabilioni ya pesa, machine hizo zikanunuliwa na halafu ikapita miaka 35 bila ajali kutokea, hicho chombo kilichonunuliwa kwa pesa nyingi ambazo ni kodi ya wananchi kiwe kinakaa tu bure kikiota kutu eti kikisubiri ajali itokee!.

Ni kweli jeshi la wanamaji inabidi liboreshwe, uwepo wao karibu na uwanja wa ndege wa Bukoba ni wa muhimu sana kuwepo wakiwa na vifaa vya kisasa, lakini kitaifa tusifanye maamuzi ya kukurupuka na yakajumuisha ufisadi humu humo na mwisho wa siku kitakachonunuliwa kinakuwa ni kama mapambo tu.

Nimemuelewa vyema mkurugenzi wa TCAA. Hakuna sababu ya msingi ya kutahayari na kila mtu akaja na maoni ambayo mengi kati ya hayo hata hayatekelezeki.

Siku njema wapendwa.
 
Maelezo ya mkurugenzi ni mazuri yana mapungufu kwa vile hakuelezea hali ya miundo mbinu ya zimamoto na uokoaji iliyoko uwanja wa ndege wa Bukoba,nk. Muhimu tungoje taarifa ya uchunguzi itatoa majibu ya kisera na mipango yenye mikakati ya muda mfupi, kati na mirefu kuhusu usalama wa anga,viwanja vyetu na uokoaji kwa ujumla.
 
Maelezo ya mkurugenzi ni mazuri yana mapungufu kwa vile hakuelezea hali ya miundo mbinu ya zimamoto na uokoaji iliyoko uwanja wa ndege wa Bukoba,nk. Muhimu tungoje taarifa ya uchunguzi itatoa majibu ya kisera na mipango yenye mikakati ya muda mfupi, kati na mirefu kuhusu usalama wa anga,viwanja vyetu na uokoaji kwa ujumla.
Wanaharakati waliitumia ajali ile kuuponda uwanja wa ndege Bukoba wakati hawana taarifa sahihi. Mkurugenzi akaweka sawa takwimu na pia akajenga hoja kuwa ajali haina kinga, iwe ya daladala iwe ya bajaji iwe ya ndege.
 
Jana mchana nilikuwa namsikiliza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga Tanzania akielezea juu ya ajali ya ndege ndani ya Ziwa Victoria. Nikawa nasoma maoni yanayopita pembeni ya kile kioo cha kinakilishi changu.

Alionekana kama anapiga siasa zile zile tunazozizoea kuzisikia kutoka kwa watanzania pindi inapotokea ajali mbaya yenye kuondoa uhai wa nguvu kazi na wengi kati ya hao marehemu wakiwa ni vijana sana, kwa kweli inasikitisha.

Ni kilio kikubwa kumsikia Mzazi akiongea namna alivyopoteza binti zake wawili tena wakiwa katika umri wa kuzalisha wa ujana. Ni simanzi kumsikiliza kaka yake RIP Rubani akiusoma wasifu wake pale msibani. Kuna yule dada aliyetoka masomoni Uturuki na kufaulu akirudi nyumbani kuiona familia yake kabla hajaanza kuishi, akiwa kijana mdogo sana.

Maisha yanapotutoka ni muda wa kuhuzunika toka ndani kabisa ya moyo. Lakini wenye akili na hekima zinazochanganyika na busara huangalia aina ya ajali iliyotokea na namna gani huko tuendapo tunaweza kuziona kama ni historia ajali hizi.

Mkurugenzi wa TCAA alieleza kwa kina historia ya uwanja wa ndege wa Bukoba na ni ukweli kuwa ile ni ajali ya pili tangu uwanja ule ujengwe na wakoloni mwaka 1940. Pengine ajali ya tatu inaweza kutokea mwaka 2055.

Kizuri ni kwamba kuna uchunguzi wa kitaalam unaoendelea kwa sasa ili kujua kwa kina chanzo cha ajali ile ni kipi haswa, wajuaji wa whatsapp hawajabaki nyuma wametengeza video ambazo kwa kitendo kile ni kosa la jinai lakini ndio TZ yetu ilivyo kila mtu anajua kila kitu!.

Wapo wanaokuja na maoni ya serikali kununua Aerial Loaders kwamba ndege inapozama basi iweze kuinuliwa kwa haraka, ni mawazo mazuri ndio lakini maamuzi ya kina ya kitaasisi yanajumuisha uwepo wa wafanya maamuzi wengi. Na hizi ni ajali tu, hazina kinga kama wasemavyo waswahili na kiswahili chao.

Jeshi la wanamaji linaweza kupitisha bajeti ya mabilioni ya pesa, machine hizo zikanunuliwa na halafu ikapita miaka 35 bila ajali kutokea, hicho chombo kilichonunuliwa kwa pesa nyingi ambazo ni kodi ya wananchi kiwe kinakaa tu bure kikiota kutu eti kikisubiri ajali itokee!.

Ni kweli jeshi la wanamaji inabidi liboreshwe, uwepo wao karibu na uwanja wa ndege wa Bukoba ni wa muhimu sana kuwepo wakiwa na vifaa vya kisasa, lakini kitaifa tusifanye maamuzi ya kukurupuka na yakajumuisha ufisadi humu humo na mwisho wa siku kitakachonunuliwa kinakuwa ni kama mapambo tu.

Nimemuelewa vyema mkurugenzi wa TCAA. Hakuna sababu ya msingi ya kutahayari na kila mtu akaja na maoni ambayo mengi kati ya hayo hata hayatekelezeki.

Siku njema wapendwa.
Sioni ubaya wa kununua mashine/ndege za kunyanyulia vitu

Can you predict miaka ya ajali kutokea ?
Suala la kujipanga kuwa na mashine hizo ni muhimu Sana haijalishi ajali itatokea au haitatokea
Maana hizo ni mashine Kazi haijalishi zinaleta faida ama laa! kiasi kwamba serikali iogope kununua
 
Sioni ubaya wa kununua mashine/ndege za kunyanyulia vitu

Can you predict miaka ya ajali kutokea ?
Suala la kujipanga kuwa na mashine hizo ni muhimu Sana haijalishi ajali itatokea au haitatokea
Maana hizo ni mashine Kazi haijalishi zinaleta faida ama laa! kiasi kwamba serikali iogope kununua
Basi,hata kama kununua vifaa wanaona hakuna ulazima
Basi angalau wawape mafunzo ya uokoaji ya kutosha+ wazamiaji

Ova
 
Jana mchana nilikuwa namsikiliza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga Tanzania akielezea juu ya ajali ya ndege ndani ya Ziwa Victoria. Nikawa nasoma maoni yanayopita pembeni ya kile kioo cha kinakilishi changu.

Alionekana kama anapiga siasa zile zile tunazozizoea kuzisikia kutoka kwa watanzania pindi inapotokea ajali mbaya yenye kuondoa uhai wa nguvu kazi na wengi kati ya hao marehemu wakiwa ni vijana sana, kwa kweli inasikitisha.

Ni kilio kikubwa kumsikia Mzazi akiongea namna alivyopoteza binti zake wawili tena wakiwa katika umri wa kuzalisha wa ujana. Ni simanzi kumsikiliza kaka yake RIP Rubani akiusoma wasifu wake pale msibani. Kuna yule dada aliyetoka masomoni Uturuki na kufaulu akirudi nyumbani kuiona familia yake kabla hajaanza kuishi, akiwa kijana mdogo sana.

Maisha yanapotutoka ni muda wa kuhuzunika toka ndani kabisa ya moyo. Lakini wenye akili na hekima zinazochanganyika na busara huangalia aina ya ajali iliyotokea na namna gani huko tuendapo tunaweza kuziona kama ni historia ajali hizi.

Mkurugenzi wa TCAA alieleza kwa kina historia ya uwanja wa ndege wa Bukoba na ni ukweli kuwa ile ni ajali ya pili tangu uwanja ule ujengwe na wakoloni mwaka 1940. Pengine ajali ya tatu inaweza kutokea mwaka 2055.

Kizuri ni kwamba kuna uchunguzi wa kitaalam unaoendelea kwa sasa ili kujua kwa kina chanzo cha ajali ile ni kipi haswa, wajuaji wa whatsapp hawajabaki nyuma wametengeza video ambazo kwa kitendo kile ni kosa la jinai lakini ndio TZ yetu ilivyo kila mtu anajua kila kitu!.

Wapo wanaokuja na maoni ya serikali kununua Aerial Loaders kwamba ndege inapozama basi iweze kuinuliwa kwa haraka, ni mawazo mazuri ndio lakini maamuzi ya kina ya kitaasisi yanajumuisha uwepo wa wafanya maamuzi wengi. Na hizi ni ajali tu, hazina kinga kama wasemavyo waswahili na kiswahili chao.

Jeshi la wanamaji linaweza kupitisha bajeti ya mabilioni ya pesa, machine hizo zikanunuliwa na halafu ikapita miaka 35 bila ajali kutokea, hicho chombo kilichonunuliwa kwa pesa nyingi ambazo ni kodi ya wananchi kiwe kinakaa tu bure kikiota kutu eti kikisubiri ajali itokee!.

Ni kweli jeshi la wanamaji inabidi liboreshwe, uwepo wao karibu na uwanja wa ndege wa Bukoba ni wa muhimu sana kuwepo wakiwa na vifaa vya kisasa, lakini kitaifa tusifanye maamuzi ya kukurupuka na yakajumuisha ufisadi humu humo na mwisho wa siku kitakachonunuliwa kinakuwa ni kama mapambo tu.

Nimemuelewa vyema mkurugenzi wa TCAA. Hakuna sababu ya msingi ya kutahayari na kila mtu akaja na maoni ambayo mengi kati ya hayo hata hayatekelezeki.

Siku njema wapendwa.

Unaandika kana kwamba hayo mabilioni tunayoyaokoa kwa kutowekeza kwenye vifaa vya uokozi yatumika kwingine kwenye tija kila wakati. Pengine ungeonyesha uchungu huu na fedha za umma kwenye ununuaji wa magari ya mabilioni ya hadhi ya wakubwa, upotevu tunaousoma kwenye ripoti za CAG kila mwaka, ufisadi na mengine kama hayo, ungekua na mantiki.

Kuleta hoja ya kiuchumi kupinga kuwekeza kwenye utayari wa majanga kwa kigezo kwamba pengine vifaa utakavyonunua havitatumika kwa miaka mingi, kwanza ni false economy, pili, kwenye nchi ambayo NSSF kukubali kuingia kwenye hasara ya mabilioni kutokana na mikataba mibovu ni jambo ambalo hata halibahatiki kupata wiki moja kwenye news cycle, ni kutokuwa mkweli au outright dishonest.
 
Unaandika kana kwamba hayo mabilioni tunayoyaokoa kwa kutowekeza kwenye vifaa vya uokozi yatumika kwingine kwenye tija kila wakati. Pengine ungeonyesha uchungu huu na fedha za umma kwenye ununuaji wa magari ya mabilioni ya hadhi ya wakubwa, upotevu tunaousoma kwenye ripoti za CAG kila mwaka, ufisadi na mengine kama hayo, ungekua na mantiki.

Kuleta hoja ya kiuchumi kupinga kuwekeza kwenye utayari wa majanga kwa kigezo kwamba pengine vifaa utakavyonunua havitatumika kwa miaka mingi, kwanza ni false economy, pili, kwenye nchi ambayo NSSF kukubali kuingia kwenye hasara ya mabilioni kutokana na mikataba mibovu ni jambo ambalo hata halibahatiki kupata wiki moja kwenye news cycle, ni kutokuwa mkweli au outright dishonest.
Mabilioni ya magari ni lazima yalete nongwa, tunayaongelea mabilioni kama vile ni pesa ambazo hatuna uchungu nazo.

Linganisha mabilioni hayo ni miradi kama ya umeme inayoendelea nchi nzima, linganisha fedha hizo nyingi na ukarabati wa bandari zote za fukwe ya TZ, ni pesa kidogo sana japokuwa kwa sasa zitaonekana ni nyingi kwani maji ni shida sana na ni kama vile serikali inashindwa kuja na suluhisho la kudumu.

Linganisha mabilioni hayo na ukweli kuwa kuna uwekezaji mkubwa sana unaokuja na unaofanywa ndani ya muda huu wenye kuleta faida pana kwa miaka mingi ijayo. Linganisha fedha hizo na mradi kama wa LNG wa gesi na faida zake kiuchumi.

Manunuzi ya hicho kifaa cha kuokolea ndege yatakula pesa nyingi na kwa muda mwingi kitakuwa kimekaa tu pale pembeni ya uwanja wa ndege wa Bukoba kikiwa hakina kazi ya kufanya. Na ni baadhi yetu humu watakaokuja na uzi unaohoji ni kwanini serikali inunue kifaa cha uokozi kwa pesa nyingi halafu kiishie kukaa tu bila ya kufanya kazi.
 
Jana mchana nilikuwa namsikiliza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga Tanzania akielezea juu ya ajali ya ndege ndani ya Ziwa Victoria. Nikawa nasoma maoni yanayopita pembeni ya kile kioo cha kinakilishi changu.

Alionekana kama anapiga siasa zile zile tunazozizoea kuzisikia kutoka kwa watanzania pindi inapotokea ajali mbaya yenye kuondoa uhai wa nguvu kazi na wengi kati ya hao marehemu wakiwa ni vijana sana, kwa kweli inasikitisha.

Ni kilio kikubwa kumsikia Mzazi akiongea namna alivyopoteza binti zake wawili tena wakiwa katika umri wa kuzalisha wa ujana. Ni simanzi kumsikiliza kaka yake RIP Rubani akiusoma wasifu wake pale msibani. Kuna yule dada aliyetoka masomoni Uturuki na kufaulu akirudi nyumbani kuiona familia yake kabla hajaanza kuishi, akiwa kijana mdogo sana.

Maisha yanapotutoka ni muda wa kuhuzunika toka ndani kabisa ya moyo. Lakini wenye akili na hekima zinazochanganyika na busara huangalia aina ya ajali iliyotokea na namna gani huko tuendapo tunaweza kuziona kama ni historia ajali hizi.

Mkurugenzi wa TCAA alieleza kwa kina historia ya uwanja wa ndege wa Bukoba na ni ukweli kuwa ile ni ajali ya pili tangu uwanja ule ujengwe na wakoloni mwaka 1940. Pengine ajali ya tatu inaweza kutokea mwaka 2055.

Kizuri ni kwamba kuna uchunguzi wa kitaalam unaoendelea kwa sasa ili kujua kwa kina chanzo cha ajali ile ni kipi haswa, wajuaji wa whatsapp hawajabaki nyuma wametengeza video ambazo kwa kitendo kile ni kosa la jinai lakini ndio TZ yetu ilivyo kila mtu anajua kila kitu!.

Wapo wanaokuja na maoni ya serikali kununua Aerial Loaders kwamba ndege inapozama basi iweze kuinuliwa kwa haraka, ni mawazo mazuri ndio lakini maamuzi ya kina ya kitaasisi yanajumuisha uwepo wa wafanya maamuzi wengi. Na hizi ni ajali tu, hazina kinga kama wasemavyo waswahili na kiswahili chao.

Jeshi la wanamaji linaweza kupitisha bajeti ya mabilioni ya pesa, machine hizo zikanunuliwa na halafu ikapita miaka 35 bila ajali kutokea, hicho chombo kilichonunuliwa kwa pesa nyingi ambazo ni kodi ya wananchi kiwe kinakaa tu bure kikiota kutu eti kikisubiri ajali itokee!.

Ni kweli jeshi la wanamaji inabidi liboreshwe, uwepo wao karibu na uwanja wa ndege wa Bukoba ni wa muhimu sana kuwepo wakiwa na vifaa vya kisasa, lakini kitaifa tusifanye maamuzi ya kukurupuka na yakajumuisha ufisadi humu humo na mwisho wa siku kitakachonunuliwa kinakuwa ni kama mapambo tu.

Nimemuelewa vyema mkurugenzi wa TCAA. Hakuna sababu ya msingi ya kutahayari na kila mtu akaja na maoni ambayo mengi kati ya hayo hata hayatekelezeki.

Siku njema wapendwa.
Mkurugenzi TCAA pia aliutaarifu umma kuwa ripoti ya awali itatoka ndani ya siku 14 na ripoti final itatoka baada ya miezi 12.
Ukifuatilia comments utagundua watu wengi hawana uelewa wa air crash investigations kiasi cha kulazimisha Mkurugenzi awaambie chanzo cha ajali.
Wanasahau kuwa Accident and incident investigation bureau iko chini ya wiraza ya ujenzi na uchukuzi na iko independent, hivyo waachwe wafanye kazi yao.
NB: Ziko ajali zilizochukua muda mrefu kuchunguza, mfano: Swiss air flight 111 from JFK to Switzerland iliyopata ajali 1998, uchunguzi wake ulitumia miaka 4 na nusu.
 
Mkurugenzi wa TCCA kwanza amefafanua kwamba hii ni ajali ya pili tangu uwanja ujengwe, hii ni ajali ya nne ambazo zinafahamika Bukoba. Ya kwanza mwaka 1969, mabaki ya hiyo ndege yaliwekwa Ihungo sec. School na Brother Felix (brutus), sijui kama bado yapo. Ndege ya pili ilianguka 1979 kiwanja cha bukoba, abiria wote walikufa, ilikuwa mali ya Jwtz. Ndege ya tatu ilianguka 1999 mali ya Jwtz, ilikuwa inatua kutokea ziwani, ikakosea hadi katikati ya uwanja kugusa udongo. Rubani kaamua kuruka tena, bawa moja likagonga mti, ndege ikaanguka, abiria zaidi ya 10 walitoka salama. Abiria mmoja alirudi ndani ya ndege kuokoa sanduku la maiti aliyokuwa analeta Bukoba, ghafla ndege ikaanza kuungua, huyo abiria 1 alikufa. Ajali ya juzi ni ya nne.
Kumbuka kila mwaka uwanja unatumia feza kufanya zoezi la uokozi. Tunapewa taarifa, ndege imeanguka ziwani, kisha tunaambiwa ni zoezi. Wanafanya zoezi bila kuogelea?
 
Mabilioni ya magari ni lazima yalete nongwa, tunayaongelea mabilioni kama vile ni pesa ambazo hatuna uchungu nazo.

Linganisha mabilioni hayo ni miradi kama ya umeme inayoendelea nchi nzima, linganisha fedha hizo nyingi na ukarabati wa bandari zote za fukwe ya TZ, ni pesa kidogo sana japokuwa kwa sasa zitaonekana ni nyingi kwani maji ni shida sana na ni kama vile serikali inashindwa kuja na suluhisho la kudumu.

Linganisha mabilioni hayo na ukweli kuwa kuna uwekezaji mkubwa sana unaokuja na unaofanywa ndani ya muda huu wenye kuleta faida pana kwa miaka mingi ijayo. Linganisha fedha hizo na mradi kama wa LNG wa gesi na faida zake kiuchumi.

Manunuzi ya hicho kifaa cha kuokolea ndege yatakula pesa nyingi na kwa muda mwingi kitakuwa kimekaa tu pale pembeni ya uwanja wa ndege wa Bukoba kikiwa hakina kazi ya kufanya. Na ni baadhi yetu humu watakaokuja na uzi unaohoji ni kwanini serikali inunue kifaa cha uokozi kwa pesa nyingi halafu kiishie kukaa tu bila ya kufanya kazi.
Kuna anayelalamikia gharama za bima na ajali hajawahi kupata au bajeti ya majeshi bila vita? Ndio false economy ninayoisema.

Hoja yangu ni kubania matumizi kwenye vyombo vya uokozi kwa kisingizio kwamba havitotumika, wakati huo huo matumizi mabovu, ufisadi, upigaji kila kona. Ningeelewa majibu yako kama hizo hela tunazookoa zinakwenda kwenye bandari, umeme bila wizi na ubadhirifu. Ndio maana nasema ni hoja danganyifu. Kama nchi, tumewahi kununua radar ambayo kuna walioona hatuhitaji Kwa matumizi yetu, tumejenga airport ya standard za kimataifa, licha ya wengi kushindwa kuona economic justification ya uwekezaji wake. Tazama huko utapata mifano sahihi ya matumizi mabaya kujenga hoja yako
 
Kuna anayelalamikia gharama za bima na ajali hajawahi kupata au bajeti ya majeshi bila vita? Ndio false economy ninayoisema.

Hoja yangu ni kubania matumizi kwenye vyombo vya uokozi kwa kisingizio kwamba havitotumika, wakati huo huo matumizi mabovu, ufisadi, upigaji kila kona. Ningeelewa majibu yako kama hizo hela tunazookoa zinakwenda kwenye bandari, umeme bila wizi na ubadhirifu. Ndio maana nasema ni hoja danganyifu. Kama nchi, tumewahi kununua radar ambayo kuna walioona hatuhitaji Kwa matumizi yetu, tumejenga airport ya standard za kimataifa, radar licha ya wengi kushindwa kuona economic justification ya uwekezaji wake. Tazama huko utapata mifano sahihi ya matumizi mabaya kujenga hoja yako
Mkuu Hey, hoja yako nimeielewa sana. Manunuzi ya vifaa vya uokoaji yanabidi yahusishe mamlaka za uokoaji kama Navy wenyewe, waone kama upo umuhimu na pesa za kufanya hivyo.

Radar zipo nne na zimenunuliwa kwa bei ya kueleweka na zinatumika kwa faida ya nchi kwa ujumla. Napingana na hoja yako kwamba matumizi makubwa tunayafanya mara kwa mara hivyo tununue tu hiyo Aerial Crane.

Kumbuka ajali imetokea mwaka 2022 na inaweza kuja kutokea tena 2050. Ajali za ndege ni mbaya siku zote lakini hutokea mara chache sana. Mchakato wa kununua hiyo crane unaweza kutengeneza wapigaji na upigaji na mtambo ukawa unaota kutu hapo uwanja wa ndege.
 
Labda kinunuliwe kama tunavyonunua mabomu kwa ajili ya kujihami na kujilinda wakati wa vita. Bila shaka nayo yana expire date yake, kwamba ukifika muda huo lazima uyateketeze na hukuyatumia.
Tatizo ninaloliona ni preventive maintenance yake. Je itakuwa consistent kwamba ikitokea kikahitajika kitumike effectively. Tuna tatizo sana la kupuuzia mambo, utaona tutakuwa moto sana kukifuatilia mwanzoni kinapoletwa na baadaye tutaanza kuambiana hakuna fungu la matengenezo.
 
Jana mchana nilikuwa namsikiliza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga Tanzania akielezea juu ya ajali ya ndege ndani ya Ziwa Victoria. Nikawa nasoma maoni yanayopita pembeni ya kile kioo cha kinakilishi changu.

Alionekana kama anapiga siasa zile zile tunazozizoea kuzisikia kutoka kwa watanzania pindi inapotokea ajali mbaya yenye kuondoa uhai wa nguvu kazi na wengi kati ya hao marehemu wakiwa ni vijana sana, kwa kweli inasikitisha.

Ni kilio kikubwa kumsikia Mzazi akiongea namna alivyopoteza binti zake wawili tena wakiwa katika umri wa kuzalisha wa ujana. Ni simanzi kumsikiliza kaka yake RIP Rubani akiusoma wasifu wake pale msibani. Kuna yule dada aliyetoka masomoni Uturuki na kufaulu akirudi nyumbani kuiona familia yake kabla hajaanza kuishi, akiwa kijana mdogo sana.

Maisha yanapotutoka ni muda wa kuhuzunika toka ndani kabisa ya moyo. Lakini wenye akili na hekima zinazochanganyika na busara huangalia aina ya ajali iliyotokea na namna gani huko tuendapo tunaweza kuziona kama ni historia ajali hizi.

Mkurugenzi wa TCAA alieleza kwa kina historia ya uwanja wa ndege wa Bukoba na ni ukweli kuwa ile ni ajali ya pili tangu uwanja ule ujengwe na wakoloni mwaka 1940. Pengine ajali ya tatu inaweza kutokea mwaka 2055.

Kizuri ni kwamba kuna uchunguzi wa kitaalam unaoendelea kwa sasa ili kujua kwa kina chanzo cha ajali ile ni kipi haswa, wajuaji wa whatsapp hawajabaki nyuma wametengeza video ambazo kwa kitendo kile ni kosa la jinai lakini ndio TZ yetu ilivyo kila mtu anajua kila kitu!.

Wapo wanaokuja na maoni ya serikali kununua Aerial Loaders kwamba ndege inapozama basi iweze kuinuliwa kwa haraka, ni mawazo mazuri ndio lakini maamuzi ya kina ya kitaasisi yanajumuisha uwepo wa wafanya maamuzi wengi. Na hizi ni ajali tu, hazina kinga kama wasemavyo waswahili na kiswahili chao.

Jeshi la wanamaji linaweza kupitisha bajeti ya mabilioni ya pesa, machine hizo zikanunuliwa na halafu ikapita miaka 35 bila ajali kutokea, hicho chombo kilichonunuliwa kwa pesa nyingi ambazo ni kodi ya wananchi kiwe kinakaa tu bure kikiota kutu eti kikisubiri ajali itokee!.

Ni kweli jeshi la wanamaji inabidi liboreshwe, uwepo wao karibu na uwanja wa ndege wa Bukoba ni wa muhimu sana kuwepo wakiwa na vifaa vya kisasa, lakini kitaifa tusifanye maamuzi ya kukurupuka na yakajumuisha ufisadi humu humo na mwisho wa siku kitakachonunuliwa kinakuwa ni kama mapambo tu.

Nimemuelewa vyema mkurugenzi wa TCAA. Hakuna sababu ya msingi ya kutahayari na kila mtu akaja na maoni ambayo mengi kati ya hayo hata hayatekelezeki.

Siku njema wapendwa.
Kipimo hiki hapa:

 
Mtoa mada huna akili, pia ni chawa. Mwenye akili timamu hawezi kusema tusinunue vifaa vya uokoaji kwa kuwa ajali zinatokea mara chache, hizi ni akili za ki chawa kabisa. Basi kwa akili hizi tufute na JWTZ maana vita ya mwisho Tz kupigana ni 1977, miaka 50 nyuma huko.
 
Umeanzisha mada kwa ajili yakutetea uzembe.Huu ujinga unakupa faida gani wakati kila kitu kiko wazi kua nchi haina kabisa mipango mikakati ya maana kwenye majanga yaliyowai kutokea zaidi ya viongozi kutoa pole na ubani..Hakuna mtu ambaye anakataa ajali kutokea bali watu wenye akili wanazungumzia namna ambavyo nchi imejipanga kutoa angalau huduma ya kwanza za uokoaji kwenye dharura.Mifano iko mingi tu ambayo hakuna tulichojifunza alafu wewe unakuja kutetea kwamba tuishi ivyo hivyo kwasababu ajali zipo tu.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Hey, hoja yako nimeielewa sana. Manunuzi ya vifaa vya uokoaji yanabidi yahusishe mamlaka za uokoaji kama Navy wenyewe, waone kama upo umuhimu na pesa za kufanya hivyo.

Radar zipo nne na zimenunuliwa kwa bei ya kueleweka na zinatumika kwa faida ya nchi kwa ujumla. Napingana na hoja yako kwamba matumizi makubwa tunayafanya mara kwa mara hivyo tununue tu hiyo Aerial Crane.

Kumbuka ajali imetokea mwaka 2022 na inaweza kuja kutokea tena 2050. Ajali za ndege ni mbaya siku zote lakini hutokea mara chache sana. Mchakato wa kununua hiyo crane unaweza kutengeneza wapigaji na upigaji na mtambo ukawa unaota kutu hapo uwanja wa ndege.
CHANGAMOTO YA UWANJA.

..kuna Mhandisi mmoja amehojiwa na Clouds ameeleza vizuri sana kwamba uwanja wa ndege wa Bukoba ni hatarishi.

..ameeleza kwamba runway yake ni fupi na hivyo kuwa changamoto ktk utuaji wa ndege nyingi zinazotumia uwanja huo.

..tatizo lingine ni uwepo wa milima kwa upande mmoja na kisiwa karibu na uwanja hivyo kulazimisha ndege kutua uwanjani hapo kutokea uelekeo mmoja.

..Na huyo Mhandisi amesema aliwasilisha ripoti za uchunguzi wake kwa Katibu Mkuu wa Wizara, RC wa Kagera, RAS wa Kagera, Mamlaka ya viwanja vya ndege, na Wabunge wa mkoa wa Kagera.

..Mhandisi anasema alionya na anaendelea kuonya kwamba uwanja wa Bukoba ni hatari kwa ndege nyingi zinazotua pale.

UZEMBE KTK UOKOAJI.

..Ni kweli kwamba ajali haina kinga.

..Je, uzembe ktk uokoaji nao hauna kinga?

..Hii sio ajali ya kwanza kutokea ktk Ziwa Victoria na kumekuwepo na malalamiko ya vyombo vyetu kukosa utayari na kutokuwa na vifaa.

..Binafsi sijaona kama tumejiongeza au tume'improve toka ajali ya Mv Bukoba, Mv Ukerewe, na sasa ajali ya Precision Airlines.

..Kuna ulazima wa kubadilisha MINDSET ya vyombo vyetu vya usalama ili vitilie mkazo masuala ya uokoaji ktk ajali na pamoja na majango.

..Masuala la mafunzo, na vifaa bora vya kazi lazima yatiliwe mkazo. Kulikuwa kutokea moto ktk kituo chetu cha mpaka wa Rusumo. Ilikuwa AIBU kubwa kwani helikopta ya kuzima moto huo ilibidi itoke Rwanda.

..Kulipotokea baa la Nzige, Tanzania iliaibika tena kwani tulikuwa hatuna ndege ya serikali kupambana na wadudu hao waharibifu.

..Ukiacha mafunzo, na vifaa, kuna suala la TARATIBU ZA UJENZI. Mfano ninaoweza kuutoa hapa ni kutokuwepo kwa njia za kuokoa watu wakati wa ajali ktk barabara zetu. Barabara zetu ni nyembamba mno na hazina nafasi kwa waokoaji kufika eneo ambako kuna ajali.

..Tunaweza kuwa na vifaa na mafunzo ya kutosha lakini kama hakuna miundombinu wezeshi kwa waokoaji tunazidi kufeli.
 
Mtoa mada huna akili, pia ni chawa. Mwenye akili timamu hawezi kusema tusinunue vifaa vya uokoaji kwa kuwa ajali zinatokea mara chache, hizi ni akili za ki chawa kabisa. Basi kwa akili hizi tufute na JWTZ maana vita ya mwisho Tz kupigana ni 1977, miaka 50 nyuma huko.
Ulivyoongea kwa msisitizo juu ya uchawa inaonyesha wewe ni chawa pro max kabisa. Sijapinga manunuzi ya hivyo vifaa, nimesema wahusika wa suala zima la uokoaji ndio watoe kauli ya kitaalam baada ya vikao halali kufanyika.

Pia suala la ajali ni gumu kulitabiri litatokea lini, unaweza kununua kifaa leo kikapata umuhimu wa kutumiwa miaka hamsini ijayo.

JWTZ ni tofauti kabisa na ajali hizi, hapo umedhihirisha kuwa wewe sio chawa tu, bali ni yule mtupu kabisa kichwani. Jeshi linailinda nchi muda wote miezi yote kumi na mbili kuna watu hawalali huko mipakani. Kama wewe unalala mpaka unakoroma tambua kuwa wapo wanajeshi huo usingizi wako ni kwa sababu yao.
 
CHANGAMOTO YA UWANJA.

..kuna Mhandisi mmoja amehojiwa na Clouds ameeleza vizuri sana kwamba uwanja wa ndege wa Bukoba ni hatarishi.

..ameeleza kwamba runway yake ni fupi na hivyo kuwa changamoto ktk utuaji wa ndege nyingi zinazotumia uwanja huo.

..tatizo lingine ni uwepo wa milima kwa upande mmoja na kisiwa karibu na uwanja hivyo kulazimisha ndege kutua uwanjani hapo kutokea uelekeo mmoja.

..Na huyo Mhandisi amesema aliwasilisha ripoti za uchunguzi wake kwa Katibu Mkuu wa Wizara, RC wa Kagera, RAS wa Kagera, Mamlaka ya viwanja vya ndege, na Wabunge wa mkoa wa Kagera.

..Mhandisi anasema alionya na anaendelea kuonya kwamba uwanja wa Bukoba ni hatari kwa ndege nyingi zinazotua pale.

UZEMBE KTK UOKOAJI.

..Ni kweli kwamba ajali haina kinga.

..Je, uzembe ktk uokoaji nao hauna kinga?

..Hii sio ajali ya kwanza kutokea ktk Ziwa Victoria na kumekuwepo na malalamiko ya vyombo vyetu kukosa utayari na kutokuwa na vifaa.

..Binafsi sijaona kama tumejiongeza au tume'improve toka ajali ya Mv Bukoba, Mv Ukerewe, na sasa ajali ya Precision Airlines.

..Kuna ulazima wa kubadilisha MINDSET ya vyombo vyetu vya usalama ili vitilie mkazo masuala ya uokoaji ktk ajali na pamoja na majango.

..Masuala la mafunzo, na vifaa bora vya kazi lazima yatiliwe mkazo. Kulikuwa kutokea moto ktk kituo chetu cha mpaka wa Rusumo. Ilikuwa AIBU kubwa kwani helikopta ya kuzima moto huo ilibidi itoke Rwanda.

..Kulipotokea baa la Nzige, Tanzania iliaibika tena kwani tulikuwa hatuna ndege ya serikali kupambana na wadudu hao waharibifu.

..Ukiacha mafunzo, na vifaa, kuna suala la TARATIBU ZA UJENZI. Mfano ninaoweza kuutoa hapa ni kutokuwepo kwa njia za kuokoa watu wakati wa ajali ktk barabara zetu. Barabara zetu ni nyembamba mno na hazina nafasi kwa waokoaji kufika eneo ambako kuna ajali.

..Tunaweza kuwa na vifaa na mafunzo ya kutosha lakini kama hakuna miundombinu wezeshi kwa waokoaji tunazidi kufeli.
Suala la runway kuwa fupi sio kweli. Mkurugenzi ameeleza kwa kirefu kwamba mazingira ya uwanja wa Bukoba yanaruhusu ndege kutua na kupaa muda wowote. Hizi ndege za precision zimeruka na kutua pale tangu 1992 hivyo ni ajali tu kama nyinginezo.

Nakubaliana na wewe suala la usalama kwanza kupewa kipaumbele, wazungu wanasema safety first.
 
Back
Top Bottom