Nimemuelewa mkurugenzi TCAA hii ni ajali kama zingine japo kuondokewa na mpendwa hakuzoeleki

Nimemuelewa mkurugenzi TCAA hii ni ajali kama zingine japo kuondokewa na mpendwa hakuzoeleki

Ulivyoongea kwa msisitizo juu ya uchawa inaonyesha wewe ni chawa pro max kabisa. Sijapinga manunuzi ya hivyo vifaa, nimesema wahusika wa suala zima la uokoaji ndio watoe kauli ya kitaalam baada ya vikao halali kufanyika.

Pia suala la ajali ni gumu kulitabiri litatokea lini, unaweza kununua kifaa leo kikapata umuhimu wa kutumiwa miaka hamsini ijayo.

JWTZ ni tofauti kabisa na ajali hizi, hapo umedhihirisha kuwa wewe sio chawa tu, bali ni yule mtupu kabisa kichwani. Jeshi linailinda nchi muda wote miezi yote kumi na mbili kuna watu hawalali huko mipakani. Kama wewe unalala mpaka unakoroma tambua kuwa wapo wanajeshi huo usingizi wako ni kwa sababu yao.
Narudia tena huna akili wewe, mwenye akili timamu yoyote hawezi kusema vifaa vya uokoaji visinunuliwe kwa kuwa ajali zinatokea mara chache. Vifaa vya JWTZ kama mabomu, vifaru na ndege za kivita zinanunuliwa kwa sababu gani kama vita ya mwisho ilikuwa 50yrs huko. Vitu vyote hivyo vinafanywa kwa ajili ya utayari, sasa kwa nini vifaa vya uokoaji tushindwe?
 
Suala la runway kuwa fupi sio kweli. Mkurugenzi ameeleza kwa kirefu kwamba mazingira ya uwanja wa Bukoba yanaruhusu ndege kutua na kupaa muda wowote. Hizi ndege za precision zimeruka na kutua pale tangu 1992 hivyo ni ajali tu kama nyinginezo.

Nakubaliana na wewe suala la usalama kwanza kupewa kipaumbele, wazungu wanasema safety first.

..sikiliza mahojiano ya Clouds na Eng.Mushumbusi.

..mimi nimemsikiliza na nimeshawishika na anachokisema kwamba runway ya uwanja wa ndege wa Bukoba ni hatarishi.
 
CHANGAMOTO YA UWANJA.

..kuna Mhandisi mmoja amehojiwa na Clouds ameeleza vizuri sana kwamba uwanja wa ndege wa Bukoba ni hatarishi.

..ameeleza kwamba runway yake ni fupi na hivyo kuwa changamoto ktk utuaji wa ndege nyingi zinazotumia uwanja huo.

..tatizo lingine ni uwepo wa milima kwa upande mmoja na kisiwa karibu na uwanja hivyo kulazimisha ndege kutua uwanjani hapo kutokea uelekeo mmoja.

..Na huyo Mhandisi amesema aliwasilisha ripoti za uchunguzi wake kwa Katibu Mkuu wa Wizara, RC wa Kagera, RAS wa Kagera, Mamlaka ya viwanja vya ndege, na Wabunge wa mkoa wa Kagera.

..Mhandisi anasema alionya na anaendelea kuonya kwamba uwanja wa Bukoba ni hatari kwa ndege nyingi zinazotua pale.

UZEMBE KTK UOKOAJI.

..Ni kweli kwamba ajali haina kinga.

..Je, uzembe ktk uokoaji nao hauna kinga?

..Hii sio ajali ya kwanza kutokea ktk Ziwa Victoria na kumekuwepo na malalamiko ya vyombo vyetu kukosa utayari na kutokuwa na vifaa.

..Binafsi sijaona kama tumejiongeza au tume'improve toka ajali ya Mv Bukoba, Mv Ukerewe, na sasa ajali ya Precision Airlines.

..Kuna ulazima wa kubadilisha MINDSET ya vyombo vyetu vya usalama ili vitilie mkazo masuala ya uokoaji ktk ajali na pamoja na majango.

..Masuala la mafunzo, na vifaa bora vya kazi lazima yatiliwe mkazo. Kulikuwa kutokea moto ktk kituo chetu cha mpaka wa Rusumo. Ilikuwa AIBU kubwa kwani helikopta ya kuzima moto huo ilibidi itoke Rwanda.

..Kulipotokea baa la Nzige, Tanzania iliaibika tena kwani tulikuwa hatuna ndege ya serikali kupambana na wadudu hao waharibifu.

..Ukiacha mafunzo, na vifaa, kuna suala la TARATIBU ZA UJENZI. Mfano ninaoweza kuutoa hapa ni kutokuwepo kwa njia za kuokoa watu wakati wa ajali ktk barabara zetu. Barabara zetu ni nyembamba mno na hazina nafasi kwa waokoaji kufika eneo ambako kuna ajali.

..Tunaweza kuwa na vifaa na mafunzo ya kutosha lakini kama hakuna miundombinu wezeshi kwa waokoaji tunazidi kufeli.
Hapo kwenye changamoto ya uwanja natofautiana kidogo na mhandisi.
Kama issue ni uwepo wa milima then uwanja wa Songwe unaweza kuwa hatarishi zaidi sababu umezungukwa na milima. Au uwanja wa Arusha ambao uko parallel na barabara ya magari.
The issue is Marubani wako well trained na well informed juu ya namna ya kuapproach uwanja husika kwa kuzingatia topography ya eneo husika.
 
Narudia tena huna akili wewe, mwenye akili timamu yoyote hawezi kusema vifaa vya uokoaji visinunuliwe kwa kuwa ajali zinatokea mara chache. Vifaa vya JWTZ kama mabomu, vifaru na ndege za kivita zinanunuliwa kwa sababu gani kama vita ya mwisho ilikuwa 50yrs huko. Vitu vyote hivyo vinafanywa kwa ajili ya utayari, sasa kwa nini vifaa vya uokoaji tushindwe?
Mkuu naona mkeo kakunyima unyumba hasira unakuja zimalizia katika uzi wangu!.

Kuna masuala yana umuhimu zaidi ya mengine, huwezi kufananisha jeshi la uokoaji wa abiria wa ndege inayoanguka.

Vipi kama hiyo ndege ingelipukia huko huko angani, hao waokoaji na vifaa vyao wangemuokoa nani?.

Kama ndege ingeangukia katikati ya ziwa hao waokoaji wangeweza vipi kufika na kufanya uokoaji?. Hivyo vifaa kama aerial loader ni ghali sana na uzoefu unaonyesha ajali zinatokea mara chache sana. Huyo rubani Rubaga ni mzoefu sana alikuwa, lakini siku ya mambo kuharibika haijulikani.

Ni maamuzi yanayofanyika kwa kuzingatia ushauri wa kitaalam wa mamlaka zenye kuhusika na uokoaji, kama wanaona inafaa kutumia mabilioni ya pesa ya walipa kodi kununulia kifaa ambacho kinakwenda kuozea katika yadi yao, basi sawa na wafanye hivyo.
 
Back
Top Bottom