Mwizukulu mgikuru
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 5,715
- 13,739
Leo asubuhi nikapanda zile gari hapa daressalam al maarufu zinaitwa daladala konda akawa anamsumbua abiria wa kike hataki kumrudishia chenji yake ikabidi niingilie ule ugomvi kwa kumpiga konda mkwara mzito mwisho wa siku akaanza kulalamika kuwa yeye ana familia na mimi sina familia. Kwa kunitazama tu akaniita mimi ni bachela.
Hivi wakuu bachela muonekano wake uko vipi na mwenye familia muonekano wake uko vipi?
Hivi wakuu bachela muonekano wake uko vipi na mwenye familia muonekano wake uko vipi?