Nimeombwa hela na mwanafunzi

Nimeombwa hela na mwanafunzi

NIMEONA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2019
Posts
3,862
Reaction score
5,693
Habarini.

Kuna jambo limenitokea, linanipa maswali na mshangao kiasi.

Ninakaa jirani na shule, jirani sana tu. Ni mtu mzima mimi, 35 yrs. Kwa sasa shule nyingi zipo ktk makambi kwa vidato vya 2 na 4, hii ni mojawapo pia.

Jioni ya leo, nikiwa sina hili wala lile nimepumzika tu nasikia hodi ikigongwa. Nilipomruhusu aingie bs alikuwa n mwanafunzi flan wa kidato cha pili aliamkia na kisha akaniomba tshs 500/=. Nilipigwa na bumbuazi kupita maelezo lkn nikajifanya sina nilichokishangaa.

Nikamuuliza unataka kununua nn akajibu anataka kununua samaki alie ugali (akilini nilitegemea nisikie peni au daftari). Nikampa tshs. 2000/=. Aliipokea haraka, akashukuru kisha huyo haraka akaondoka.

Bandugu, tangu muda huo nimetafakari mara kutafakari ujasiri wa huyo binti bado sijapata majibu mpaka nimemua nifanye sharing nanyi kisa hiki.
 
Kwa miaka 35 mtoto wa form 2 ni mwanao kabisa, amekuchukulia kama baba yake na hauna madhara tena kwake.
Tembea kifua mbele kwa kupata heshima unayostahili.
Ungekuwa baharia wa miaka 21 asingethubutu.
Inawezekana kweli mtoto anamchukulia ivo, ila sio tabia ya kuiendekeza kwa mtoto wa kike form 2 kuombaomba pesa
 
Back
Top Bottom