Nimeota nipo nje ya mwili wangu, ndoto hii inamaana gani?

Mda si mrefu, ila kifo chako hakitakuwa cha kawaida, inaonekana utachukuliwa msukule na ndugu watazika tu kitu chenye mfano wa mwili wako. Ongeza maombi, pia unaweza ni PM kwa ajili ya maombi zaidi na sadaka. Amen
Nilitaka niseme pia, huenda ameshachukuliwa msukulee.
 
Yaani kwa mfano mtu umevuta bangi Kali ile ya kisimiri haujala ukashiba,stress zimejaa kichwani,madeni,nchi ilivyo,ngono Kila mara,mirungi, visungura,ugoro,energy drinks na maandazi ya bakresa,uchovu!

Vitu kama hivi lazima uone na ukiwa unaweza mambo za uchawichawi unaweza Rudi kwako jioni ukaona shati ulilofua ukatundika kwako ni jini
 
Wewe ushachukuliwa msukule. Sasa ambia watu wako wap umeweka pesa maana hutoboi. Nasisitiza wewe ni msukule! Au umeanza kuvuta bangiii ukubwani
 
Huwa inashauriwa ukiota ndoto usimwambie mtu
 
huyu anatuchosha akili kumbe ni mdau kindakindaki wa Azam energy...mkuu acha hayo makitu utakufa unatembea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…