Nimepanda miti minne, mitatu mbele ya hotel ya Kebby's na mmoja ilipokuwa shule ya Mwenge Open Academy (MOA)

Nimepanda miti minne, mitatu mbele ya hotel ya Kebby's na mmoja ilipokuwa shule ya Mwenge Open Academy (MOA)

KING MIDAS

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2010
Posts
8,589
Reaction score
16,936
Jana tarehe 17/12/2024 nilipanda miti minne mtaa wa Mwenge Kijijini.

Nimepanda jumla ya miti minne, mmoja mbele ya ilipokuwa shule ya Mwenge Open Academy (MOA), na mingine mitatu nimepanda mbele ya Kebby's Hotel.

NI utamaduni wangu wa kupanda miti kandokando ya barabara ili kuwafanya waendao kwa miguu wapate hewa safi chini ya kivuli watembeapo kwa miguu.

Maeneo mengine niliyopanda miti ni pamoja na Boko, Bahari Beach, Mikocheni, Ununio na Oyster Bay.

Kila ninapopanda miti siiachi hivihivo, huiwekea mbolea na kumwagilia mpaka pale inaposhika kabisa na kuweza kujitegemea yenyewe.

Karibuni wana JF tufunge mwaka kwa kupanda miti kwenye maeneo yanayotuzunguka.

Mimi pia ni mwanachama wa TREE OF LIFE FOUNDATION
IMG20241217060611.jpg


img20241217060238-jpg.3179597
 

Attachments

  • IMG20241217060238.jpg
    IMG20241217060238.jpg
    1.1 MB · Views: 11
Unapanda michungwa na milimao mjini?
Ndio, miche mbalimbali ya matunda ikiwemo miembe, mizambarau, mistafeli NK ili waenda kwa miguu wasipate kivuli tu, Bali pia fursa ya kupata matunda wawapo njiani.

Kumbuka, Watanzania wengi Hawana uwezo wa kununua matunda ndio maana hadi kuna msemo "MATUNDA HADI NIANDIKIWE NA DAKTARI"
 
Jana tarehe 17/12/2024 nilipanda miti minne mtaa wa Mwenge Kijijini.

Nimepanda jumla ya miti minne, mmoja mbele ya ilipokuwa shule ya Mwenge Open Academy (MOA), na mingine mitatu nimepanda mbele ya Kebby's Hotel.

NI utamaduni wangu wa kupanda miti kandokando ya barabara ili kuwafanya waendao kwa miguu wapate hewa safi chini ya kivuli watembeapo kwa miguu.

Maeneo mengine niliyopanda miti ni pamoja na Boko, Bahari Beach, Mikocheni, Ununio na Oyster Bay.

Kila ninapopanda miti siiachi hivihivo, huiwekea mbolea na kumwagilia mpaka pale inaposhika kabisa na kuweza kujitegemea yenyewe.

Karibuni wana JF tufunge mwaka kwa kupanda miti kwenye maeneo yanayotuzunguka.

Mimi pia ni mwanachama wa TREE OF LIFE FOUNDATION View attachment 3179601

img20241217060238-jpg.3179597
KAMA HUTOJALI, NAOMBA KUJIUNGA NA HICHO CHAMATAFADHALI,IKIWEZEKANA, PAMOJA NA FAMILIA YANGU KWA UJUMLA.
 
Afya njema niliyopewa na Mwenyezi Mungu ni kibali tosha kwa Mimi kufanya yaliyojaa mema na sahihibkwa jamii yangu na kwa mazingira yanayonizunguka.
Pitia hizi sheria, usije ukalamika kuwa unaonewa😏
  1. Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (Environmental Management Act, No. 20 of 2004)
  2. Sheria ya Misitu (Forests Act, No. 14 of 2002)
  3. Sheria ya Ardhi (Land Act, No. 4 of 1999)
  4. Kanuni za Miji (City by-laws)
 
Pitia hizi sheria, usije ukalamika kuwa unaonewa😏
  1. Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (Environmental Management Act, No. 20 of 2004)
  2. Sheria ya Misitu (Forests Act, No. 14 of 2002)
  3. Sheria ya Ardhi (Land Act, No. 4 of 1999)
  4. Kanuni za Miji (City by-laws)
Nimevunja Sheria ipi kati ya hizo?
 
Pitia hizi sheria, usije ukalamika kuwa unaonewa😏
  1. Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (Environmental Management Act, No. 20 of 2004)
  2. Sheria ya Misitu (Forests Act, No. 14 of 2002)
  3. Sheria ya Ardhi (Land Act, No. 4 of 1999)
  4. Kanuni za Miji (City by-laws)
Umeshawahi kuona wapi MTU kashitakiwa kwa kwa kupanda miti?
 
Back
Top Bottom