Nimepata connection ya kwenda kusoma nje ila sasa ninafanya kazi. Naomba ushauri

Ofcourse kila sehemu kuna upuuzi,ila huwezi kuwaza negativity katika kila ishu za ughaibuni
Naomba unisamehe bure kwa kutaka kukupotosha! Nilipotoshwa pia! Pengine ningekuharibia fursa hii muhimu!

Ushauri wangu, elimu ni msingi wa maisha. Umuhimu wake unazidi huo mshahara wa 500k. Kama umejiridhisha na unamuamini rafiki yako nakushauri uende. Zaidi sana, mtegemee Mungu! Hiyo ni nafasi ya pekee wengi tunaitafuta na hatuipati! Kaongeze elimu ikupe maisha bora!
 
Pamoja kaka mkubwa umeonesha uungwana.
 
Ok nimekuelewa. Unapaswa kwanza ujiridhishe na maelezo anayokupatia huyo jamaa yako. Kwanza ujue hayo malipo yanayofanyika (In what basis/ conditions), je ni kwa mujibu wa taratibu za hiko chuo kwa wanafunzi wake au ni sheria ya hiyo nchi kuwalipa wananchi wake pamoja na foreigners?
Yote juu ya yote wewe ndiye utakayefanya uwamuzi wa mwisho baada ya moyo wako kuridhika/kutoridhika na maisha unayoishi sasa comparing to what your guy is instructing you coz siamini kama yote umeyaweka hapa akwambiayo.
 
Hebu tuambie huyo jamaa yako anasoma nchi gani? Tuanzie hapo maana kila nchi na sheria zake. Hakuna nchi inayo ruhusu mwanafunzi kufanya kazi anavyopenda. Hakuna!
 
Hebu tuambie huyo jamaa yako anasoma nchi gani? Tuanzie hapo maana kila nchi na sheria zake. Hakuna nchi inayo ruhusu mwanafunzi kufanya kazi anavyopenda. Hakuna!
Italia
Naomba kujua hizo sheria za italy
 
Unapotaka kwenda nje kusoma au kufanya kazi..

Inabidi utoke huku ukiwa na maamuzi kabisa
Je untaenda kusoma na kisha kurudi bongo?

Au utasoma huku ukifanya kazi huko na baada ya kumaliza utaendelea kuishi huko?

Wengi huchanganyikiwa kwenye kufanya maamuzi...!

Unaweza ukajisemea me nitaenda kusoma nikimaliza narudi bongo lakini baada ya kufika kule wazo lako likabadilika ukatamani unedlee kufanya kazi huko ikibidi hata kuishi huko..

Wakati huo unakuta hakuna mazingira uliyoyaanda kukusapoti kuishi huko kihalali.

Ushauri wangu nenda kasome, na hakika utapata na kazi huku ukiendelea na masomo.
kipato huko ni kikubwa kulinganisha na pesa ya huku hasa baada ya kumaliza kusoma na kupara ajira huko!
 
Cc lelulelu
Kila la kheri mkuu..
usisite kushare nasi taarifa mbali mbali hapa

 
Bla bla
 
Pole kwake , hakuwa na uwezo wa kujiongeza ..

Iwe bongo au mbele kama huwezi kujiongeza maisha haya itakula kwako tu
 
utapata na kazi ipa wakati unasoma kipato huko ni kikubwa kulinganisha na pesa ya huku hasa baada ya kumaliza kusoma na kuapa ajira huko!
Sijakuelewa vizuri mkuu hii ibara yako naomba irudiwee
 
Hizo ni taarifa zinazoonekana kama zinavutia.iko hiv.hujui anapiga mishe gani.ulaya na amerika kuna issue zingine zinaweza kuwa zinaingiza hela lakini haziko kimaadili.Zingine ni halali tuu.unjejaribu kutafuta muda wa kumtembelea kwanza ukajue anafanya nini.unaweza kuacha job hiyo inayoingiza kiasi kidogo halafu kwenda kule ukakuta mambo siyo.Utakuwa umepoteza mazima kabisa.yaani hutainuka kabisa,utakufa kwa mawazo.
 
Mkuu umenipa ushauri ambao sijauomba na wala sijautaka mimiSwali langu ni jjekama hiyo nafasi ipo kweli na jamaa ni mkweli je niache kazi au niache kusoma niendelee na kazi?
Sihitaji ushauri mwingine nje ya hilo swali
 
Chagua Moja
 
Mkuu umenipa ushauri ambao sijauomba na wala sijautaka mimiSwali langu ni jjekama hiyo nafasi ipo kweli na jamaa ni mkweli je niache kazi au niache kusoma niendelee na kazi?
Sihitaji ushauri mwingine nje ya hilo swali
Nenda kapate hela
 
Acha hiyo kazi nenda kasome, Hawa wanaocomment wengi hawana uelewa na haya mambo. Mwambie jamaa akuunganishe nenda kapige shule. Hiyo 3M kwa wazungu ni pesa ndogo Sana. Ila kwa bongo ni kubwa ndio maana wanashangaa tu hapa. Wamezoea kulipwa laki tatu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…