Nimepata huduma mbovu kutoka kwa Mfanyakazi wa NHIF - Dar, imebidi Kiongozi wake wa juu aingilie na kuniomba radhi

Nimepata huduma mbovu kutoka kwa Mfanyakazi wa NHIF - Dar, imebidi Kiongozi wake wa juu aingilie na kuniomba radhi

MeVSMe

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2024
Posts
270
Reaction score
425
Jamani mi natoa ya moyoni leo kwasababu naamini hapa JF ndo sehemu pekee nitaongea na kero yangu ikatatulika.

Huwa tunaambiwa mteja ni Mfalme, lakini huu ufalme mbona kama umegeukia Kwa watoa huduma?

Hili suala nilishaliona sana NHIF lakini kwasababu sikuwa na pa kuongelea basi likawa linauma.

Pale kuna wale watoa huduma unaowakuta dirishani ukienda wanahisi wao wanakusaidia, wanakupa msaada wakati ni jukumu lao.

Mimi binafsi ni Mwanachama wa NHIF nimejiunga na kifurushi cha TIMIZA.

Sasa nilienda kuchukua kadi pale NHIF plae katika ofisi zao zilizopo kweye jengo la PSSF, nimefika pale namkuta mbaba pale dirishani, picha linaanza naenda dirishani ananiangalia tu, nikamwambia nimekuwa kuchukua kadi.

Akauliza kwahiyo? Heee nikamwambia kwahiyo? Ndo akauliza hiyo kadi ni yako au nikamwambia ndio, akasema nani kalipia nikamwambia mume wangu, hee akasema mpaka aje yeye ndio tutatoa hiyo kadi.

I was like what!!!! Ila nikasema sawa kwa sababu kila sehemu ina sheria labda ndio sheria, nikamuuliza kaka hii Sheria imeanza lini maana mimi ndio nilikuja kufuata kadi ya mume wangu pamoja na watoto, sasa inakuwaje unasema siwezi kuchukua kadi yangu mpaka yeye?

Akasema "Sina muda wa kuongea sasa hivi, sogea pembeni nihudumia mtu mwingine 😟😟."

Aisee nilikasirika, nikabaki nimesimama akasema nakuitia mlinzi, heee nikamuuliza kaka una shida Gani?

Hee mara mlinzi akafika pale ohooo mara nikapelekwa kwenye ofisi hapo NHIF.

Nikaanza kuulizwa nikaeleza kila kitu ndio nikahudumiwa. Tena yule mtu wa ofisini alikuwa anaongea vizuri hadi akaomba msamaha.

Wana JF hii sio mara ya kwanza linatoke swala kama hili pale NHIF, kuna siku pia nilienda kusajili nikakuta mhudumu anamfokea mteja pale dirishani, I was like hivi hii ni namna gani ya kutoa huduma?

Jamani NHIF embu jitahidini kutoa huduma nzuri kwa wateja yaani tulipie vifurushi bei kubwa na bado tukija ofisini kwenu mtugombeze?

Wana JF Naomba nijue kama hili suala limenikuta mimi tu au na nyie mmekutana nalo
 
😁 ungeenda wiki ya mteja ungefurahia. Yani wwalikuwa wanatoa huduma ya kifalme hadi raha. Hadi nikajiuliza, ni hawa ninaowajua?
Unajua kwanini? Wiki ya mteja Huwa wanatafuta watu (ushers) WA kuhudumia wateja Huwa sio wao ndio maana huduma zinakuwa nzuri, ila watoa huduma WA kule ndani Zero😟😟😟
 
Ooooh mi nilijikuta nalia Kwa hasira yani
Pole sana mkuu hao ndo walivo ukienda Atcl utalia zaidi, pesa ni yako ila majibu kama kuna flight ni kubembelezana tu, huku anahudumia watenja huku ana chat na simu na workmate/mpenzi wana jisikia mpaka basi tu, hao watu wakistaafu siwaoneagi huruma kabisa, ukitoa waalimu wao wako peace [emoji111] sana sijui ni kwasbb ya mshahara mdogo.
 
Pole mkuu hao ndo walivo ukienda Atcl utalia zaidi, pesa yako ila majibu kama kuna flight ni kubembelezana tu, huku ahudumia wstenja huku ana chart na workmate wanajisikia mpaka basi, hao watu wakistaafu siwaoneagi huruma kabisa, ukitoa waalimu tu.
😟😟😟😟😟😟😟, aisee yaani sijui Hawa watu WA Serikali wakoje
 
Najaribu kuwaza ....

"Taarifa kwa umma...

Tumeona taarifa kutoka kwenye chanzo kimoja Cha mitandao ya kijamii ,mteja akilalamika kutopata huduma nzuri Toka kwenye taasisi yetu.

Tumefanya uchunguzi na kugundua kuwa hakukuwa na lugha ya kuudhi wala kejeli Bali ni mteja hakuelewa vizuri pindi alipoeleweshwa juu ya huduma zetu.

Tunapenda kuwahakikishia taasisi yetu inatosha huduma nzuri na kama Kuna tatizo ,mteja anaruhusiwa kuwasiliana na ofisi ya malalamiko au email yetu kwa msaada zaidi.

Ahsante."
 
Na mara nyingi hivi vifanyakazi vya chini ndo vina nyodo ukipelekwa kwa wakubwa juu ni wanyeyekevu sana!
Ni kweli ni kama ukamatwa na police mpelelezi asio kua na cheo kabisa atakusumbua mpaka kukuuliza majina ya babu na bibi zako ili aonekane anajua kazi sana, wakati kesi yenyewe ni yakawaida ya madai tu...... utumishi wa umma wengi washamba wametokea familia duni.
 
Kama
Jamani mi natoa ya moyoni Leo kwasababu naamini hapa JF ndo sehemu pekee nitaongea na kero yangu ikatatulika.

Huwa tunaambiwa mteja ni Mfalme, lakini huu ufalme mbona kama umegeukia Kwa watoa huduma????

Hili suala nilishaliona sana NHIF lakini kwasababu sikuwa na pa kuongelea basi likawa linauma.

Pale Kuna wale watoa huduma unaowaluta dirishani ukienda wanahisi wao wanakusaidia, wanakupa msaada wakati ni haki Yako.

Mimi binafsi ni mwanachama WA NHIF NIMEJIUNGA na kifurushi Cha TIMIZA.

Sasa nilienda kuchukua kadi nimefika pale namkuta mbaba pale dirishani picha linaanza naenda dirishani ananiangalia tu, nikamwambia nimekuwa kuchukua kadi.

Akauliza kwahiyo? Heee nikamwambia kwahiyo? Ndo akauliza hiyo kadi ni Yako au nikamwambia ndio,
akasema nani kalipia nikamwambia mume wangu, hee akasema mpaka aje yeye ndio tutatoa hiyo kadi .

I was like what!!!! Ila nikasema sawa kwasababu Kila sehemu Ina sheria labda ndio sheria, nikamuuliza kaka hii sheria imeanza lini maana Mimi ndio nilikuja kufuata kadi ya mume wangu pamoja na watoto, Sasa inakuwaje unasema siwezi kuchukua kadi yangu mpaka yeye?

Akasema Sina muda WA kuongea sasahivi, sogea pembeni nihudumia mtu mwingine 😟😟.

Aisee nilikasirika, nikabaki nimesimama akasema nakuitia mlinzi, heee nikamuuli kama una shida Gani?
Hee mara mlinzi akafika pale ohooo mara nikapelekwa Kwenye ofisi hapo NHIF.

Nikaanza kuulizwa nikaeleza Kila kitu ndio nikahudumiwa. Tena yule mtu wa ofisini alikuwa anaongea vizuri hadi akaomba msamaha.

Wana JF hii sio mara ya kwanza linatoke Swala kama hili pale NHIF, Kuna siku pia nilienda kusajili nikakuta muhudumu anamfokea mteja pale dirishani, I was like hivi hii ni Namna Gani ya kutoa huduma?

Jamani NHIF embu jitahidini kutoa huduma nzuri Kwa wateja yaani tulipie vifurushi bei kubwa na bado tukija ofisini kwenu mtugokeeee?

Wana JF Naomba nijue kama hili suala limenikuta Mimi tu au na nyie mmekutana nalo
Nadhani walikwa k
Jamani mi natoa ya moyoni Leo kwasababu naamini hapa JF ndo sehemu pekee nitaongea na kero yangu ikatatulika.

Huwa tunaambiwa mteja ni Mfalme, lakini huu ufalme mbona kama umegeukia Kwa watoa huduma????

Hili suala nilishaliona sana NHIF lakini kwasababu sikuwa na pa kuongelea basi likawa linauma.

Pale Kuna wale watoa huduma unaowaluta dirishani ukienda wanahisi wao wanakusaidia, wanakupa msaada wakati ni haki Yako.

Mimi binafsi ni mwanachama WA NHIF NIMEJIUNGA na kifurushi Cha TIMIZA.

Sasa nilienda kuchukua kadi nimefika pale namkuta mbaba pale dirishani picha linaanza naenda dirishani ananiangalia tu, nikamwambia nimekuwa kuchukua kadi.

Akauliza kwahiyo? Heee nikamwambia kwahiyo? Ndo akauliza hiyo kadi ni Yako au nikamwambia ndio,
akasema nani kalipia nikamwambia mume wangu, hee akasema mpaka aje yeye ndio tutatoa hiyo kadi .

I was like what!!!! Ila nikasema sawa kwasababu Kila sehemu Ina sheria labda ndio sheria, nikamuuliza kaka hii sheria imeanza lini maana Mimi ndio nilikuja kufuata kadi ya mume wangu pamoja na watoto, Sasa inakuwaje unasema siwezi kuchukua kadi yangu mpaka yeye?

Akasema Sina muda WA kuongea sasahivi, sogea pembeni nihudumia mtu mwingine 😟😟.

Aisee nilikasirika, nikabaki nimesimama akasema nakuitia mlinzi, heee nikamuuli kama una shida Gani?
Hee mara mlinzi akafika pale ohooo mara nikapelekwa Kwenye ofisi hapo NHIF.

Nikaanza kuulizwa nikaeleza Kila kitu ndio nikahudumiwa. Tena yule mtu wa ofisini alikuwa anaongea vizuri hadi akaomba msamaha.

Wana JF hii sio mara ya kwanza linatoke Swala kama hili pale NHIF, Kuna siku pia nilienda kusajili nikakuta muhudumu anamfokea mteja pale dirishani, I was like hivi hii ni Namna Gani ya kutoa huduma?

Jamani NHIF embu jitahidini kutoa huduma nzuri Kwa wateja yaani tulipie vifurushi bei kubwa na bado tukija ofisini kwenu mtugokeeee?

Wana JF Naomba nijue kama hili suala limenikuta Mimi tu au na nyie mmekutana nalo
Wasamehe bure, taasisi yao imepata hasara nyingi kwa kutohakiki kadi zao. kuna watu wengine mpaka walikuwa wanaaziamana kadi za matibabu.
 
Back
Top Bottom