Nimepata mchumba Mchaga wa marangu nijulisheni tabia zao

Natarajiwa kuolewa jamani nimempta mwanaume mmarangu si vibaya nikijua tabia zao ili nikatulie kwenye.ndoa jamani
Hongera , ni vigumu Sana kumfahamu mwenzio kwa kupitia kabila lake, kila mmoja ana malezi na makuzi yake binafsi. Naamini mmekuwa kwenye mahusiano muda WA kutosha hivyo umeweza kumsoma mwenzio.

Kila la kheri
 
Olewa tu Sister.

Au unataka kuolewa na Mnyakyusa?

Muhimu Muheshimu huyo mwanaume, timiza wajibu wako kama Mke.

Mengine muachie Mungu.
 
Natarajiwa kuolewa jamani nimempta mwanaume mmarangu si vibaya nikijua tabia zao ili nikatulie kwenye.ndoa jamani

Siku hizi hakuna sana tabia za kabila moja kwani watu wanachanganyika sana katika kukua/malezi;
Ila kwa ujumla wamarangu wako poa, hawana mambo mengi.
Kwa ujumla wachaga hawana mambo mengi sijui uwe na shoo kali nk nk; wao wanataka mtu anayejitambua na kuwazia maendeleo (mchakarikaji) hata kama shoo ni ya kuunga unga.
Kwa mtu anayefikiri shoo ndio itambeba, namshauri, ajaribu mikoa mingine sio KILIMANJARO......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…