Nimepewa siri nashindwa kuitunza (roho inauma)

Tatizo siku mwana akijua na akajua kuwa ulikuwa unajua kitambo tena na wakati huo ndo ashaukwaa ule ugonjwa wetu kupitia kwa huyo mke wake. Ndo urafiki utaishia hapo....NA ATAKUONA WE NDO SNITCH MAISHA!!!
 
Ndugu yangu achana na mambo yasiyokuhusu. Ukimwambia jamaa yako wewe ndio utaonekana unavuruga ndoa yao na wala sio hao wapambe waliokupa story. Ukiona unakosa kifua basi wakwepe hao jamaa uachane nao kabisa kwenye Maisha yako au lah mkopeshe huyo jamaa hela akatengeneze gari yake ili usiwe na ukaribu nao.

Kama kujua kama mtoto sio wake ajue mwenyewe huko sio kwa kuambiwa na wewe. Halafu kumbuka "kitanda hakizai haramu" wazee wa zamani walisema
 
When two stimulus are repeatedly paired together stimulus one starts to acquire properties of stimulus two

To no truly I wondering water can be down but not all stimulus will finish because the sun will fabulous than the car although me travelled to Mars yesterday I will see you yesterday madam mahondaw and sir suzukiw
 
Nikodi mimi nikamteke huyo kijana atueleze kinagaubaga wala sio kazi ngumu!
Ndani ya siku masaa 24 namleta wewe nipe adress yake, picha yake namleta bila malipo akiwa analia sana
 
Halafu mtoto wa miezi 10 huwezi mfananisha bado na mtu mzima, sura za watoto wadogo huwa bado zabadilika badilika

Kabisa mkuu mi wangu ana miezi 11 na anafanana na padree wa huku kwetu mpaka kucheka 😂 sijajua baba watoto anawaza vipi ila sio sawa kwakweli mana mimi hata salamu ya karibu na padre sijawahi kusalimiana naee😁😁
 
mkuu unaweza kuta jamaa yako kifua hana ukimwambia unaweza ukasababisha janga au ukajiaibisha mwenyewe muda utafika tu ukweli utajulikana waachie mambo yao jamaa yako naye kayataka mwache apambane na hali yake
 
Mwokoe kijana mwenzio na maradhi kama kisukari, presha, matatizo ya moyo au Ukimwi.

Halafu kama mke anaendelea kuzini basi atakuwa anatafuta wa pili. Sasa kama akiwa nao watatu na jamaa akawa na mali mbili Tatu mke na mzazi mwenzie watawaza nini?

Okoa maisha. Ila uwe na uhakika sio ukurupuke.
 
Hiki ndicho kinachonipagawisha hata mimi najikuta naumia kuliko mhusika
Ili uweze kumsaidia huyo rafiki yako jaribu kwanza kuivaa nafsi yake. Fikiria ungekuwa ndio ww umetendewa hivo na unaendelea kusalitiwa.
 
We huna urafiki wa kweli vipo vitu unaweza ukamficha rafiki lakini sio kugegedewa mkewe hadi anazalishwa na mtoto
 
Hiki ndicho kinachonipagawisha hata mimi najikuta naumia kuliko mhusika
Fanya jambo umsaidie mwenzio mkuu. Maana huyo dem wake anaonekana ameridhika na huo uovu wake na anaonekana ataongeza na petii mwingine.
 
Naona kama ngoma itanigeukia mimi iwapo ishu haitakuwa kweli? Au kuna ile mwanaume anampenda sana mkewe wakaniona mimi kama mchonganishi.NITAJIONA KAMA NIMEKUWA SHANGINGI AU MMBEYA FULANI HIVI ALAFU MI MWANAUME KABISA WA MKOANI.
 
Serikali haitakubari kwa sababu ya kuepuka watoto wa mtaani
 
Hahahaha!!!

Hii kali
Kabisa mkuu mi wangu ana miezi 11 na anafanana na padree wa huku kwetu mpaka kucheka [emoji23] sijajua baba watoto anawaza vipi ila sio sawa kwakweli mana mimi hata salamu ya karibu na padre sijawahi kusalimiana naee[emoji16][emoji16]
 
NIP
Nipe namba ya huyo jamaa nimwambie ukwel then wewe utakuwa umemsaidia maana ataepeka future cost za kumlea huyo mtoto
 
Ninyi ndio husababisha nchi kuyumba kwa kukaa na siri za watu waovu. Sababu mnayotoa eti hayakuhusu! Usalama wa nchi huanzia usalama wa mtu mmoja (human security), halafu usalama wa jamii inayokuzunguka (societal security) ambayo kwa ujumla wake hutengeneza usalama wa taifa (national security).

Tatizo la mwenzako ni lako maana linaweza kukuathiri wakati na majira usoyajua. Kinachopaswa kuzozaniwa sio kuambiwa bali ataambiwaje na kwa kutumia njia (modus operandus) ipi!

Bazazi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…