Nimepewa siri nashindwa kuitunza (roho inauma)

Nimepewa siri nashindwa kuitunza (roho inauma)

Kwa hapo wewe ndio utakuwa chanzo cha hao kufarakana ukiingia kichwa kichwa ila wanawake hawa .,hawaaminiki ,hawalindiki , hawaridhiki ,dah! Ila we mwamba nyamaza kama huyajui ili mradi wanaishi kwa amani hayo mengine wachie wenyewe
 
Wakutanishe huyo dada wa kazi huyo mwanaume na wewe wanawake huwa wanasiri sana sana aseh

Kabla ya hapo weka jamaa afanye uchuguzi kuhusu huyo Mtoto kwanini huwa wanampeleka kwa jirani na je wanalipia kuangaliziwa huyo mtoto
Na nani huwa anashinda naye muda wote (mwingi) mchana

Au tafuta hela uchukue jamaa mmoja anaye ishi humo ndani mpeni hata laki mbili laki tatu swaiba wa jamaa kabisa ambaye anapelekewa mtoto nazani jibu zuri utapata Mkuu lakutoshaa kabisa

Mwisho kabisa ndio unamchua jamaa na mtoto wote wanaenda kupima DN jibu kamili linapatikana sasa
 
Kaushaa,tu Ila Kama unapenda mahisiano ya best yako na mke wake jaribu kuchunguza pata hints za uthibitisho mfate mke wake mchane akizingua mwamshie kwa mmewe
Kabisa, cha msingi hapo ni ku discourage hiyo tabia ya huyo mama kwenda na mtoto kwa huyo jamaa mwingine mwenye hivyo vikorombwezo vya mtoto. Kitanda akizai haramu, ila heshima iwepo. Jamaa aendelee kulea mtoto tu cha msingi ana vidhibitisho kuwa mtoto ni wakwake, mke akizingua baadae kumpa mtoto jamaa wa nje basi itabidi ampigie gharama za kulea mimba hadi mtoto alipofika.
 
Mkuu achana nayo kabisa usiingilie..

Washkaji wengine akili hawana,yalinitokea nikaonekana sio..

Saizi naangalia tu movie.
 
....hii imenikera mno...pole in advance rafiki wa Billie wa Jf
 
Watu8 watoto wanabadilika sura ila kuna mambo yasiyojificha...masikio, pua, mdomo, miguu....


Usimwambie jamaa...ila mara nyingi anzisha stori zinazoelekea huko kama atajiongeza.

Cha kushangaza.

Baba, mtoto anapelekwa kucheza usipopajua mweleze hili kwa namna ya kuzunguka. Anatakiwa apajue mwanae apelekwapo.

Wewe mwenyewe kuna mambo ayafanyao mkeo ukiambiwa utakufa kwa ugonjwa wa moyo...tutafanyaje sasa kikubwa tuombeane uzima usifedheheke.
 
Kaka

Tomboka tu. Cha kufia nini? Akipenda achukue, akichukia aipotezee. Ya nini kufa kihoro? Tomboka tu mkubwa.

Njia sahihi, siku ukienda vijijini, nunua.sinu ya mwanakijiji kwa bei kubwa then akinda ujumbe au piga simu ukiwa umebadili sautiyo halafu tomboka tu. Yanini kufa kwa fundo la roho? Tomboka tu

Bazazi
 
Kama ingekuwa ni mimi nimekutikana na hilo kashikashi ningechofanya ni kuandaa mazingira ya kumpima mtoto na mimi DNA, ikithibitika sio wangu basi nachukua ushahidi wangu narudi home nampatia huyo mke wa mtu na kumwambia, "mama, malezi mazuri ya mtoto ni pande mbili yani baba na mama, chukua mtoto nenda kwa babake mkalee mtoto wenu, nilifikiria kumuua huyu mtoto lakini nafsi ikaniambia hausiki malaika huyu, nikafikiria kukuua wewe malaya nikaona malaika atabaki bila mama hausiki" chukua mtoto ondokeni kabla sijachukua maamuzi yote mawili niliyopingananayo.
 
  • Thanks
Reactions: THT
Usiingilie ndoa ya mwenzio kwa story za umbea wa watu waache ukweli utakuja kujulikana mbeleni ila we usiwe chanzo
 
Kama ingekuwa ni mimi nimekutikana na hilo kashikashi ningechofanya ni kuandaa mazingira ya kumpima mtoto na mimi DNA, ikithibitika sio wangu basi nachukua ushahidi wangu narudi home nampatia huyo mke wa mtu na kumwambia, "mama, malezi mazuri ya mtoto ni pande mbili yani baba na mama, chukua mtoto nenda kwa babake mkalee mtoto wenu, nilifikiria kumuua huyu mtoto lakini nafsi ikaniambia hausiki malaika huyu, nikafikiria kukuua wewe malaya nikaona malaika atabaki bila mama hausiki" chukua mtoto ondokeni kabla sijachukua maamuzi yote mawili niliyopingananayo.
Unakuta unajitutumua kusomesha vizuri sio na kila weekend unawaringishia wenzio kutoka na mwanao out...

Tehteh...huku mke anachekea tumboni hili boya nalo hata halijielewi.

Hiyo hasira ni kubwa mkuu chutama tu uone aibu uendelee na maisha.
 
Huyo ni wewe wala sio mimi
What if Wanafamilia Wanajua na walisha yamaliza ila nyie wapambe wa Nje hamjui?

Kumpeleka mtoto kwa Jirani Sio Sababu...!!!

Hata mimi Nikaumua kumfananisha mtoto wangu na wako na Nikaruhusu mindset yangu ikubali kufanisha naweza sema mtoto wangu kafanana Na wewe

Wewe Kazi yako ni kwenda Kumchukua jamaa na Kuelekea Kazini Mengine Yaache!

Mimi hata rafiki zangu wakija Kwangu huwa wanajua Wafanye yote maongezi kuhusu familia yanguu waachee tuongee mengine ila chochote kuhusu familia Yangu Ni Big no! Either kiwe kizuri au kibaya Ni Big No! Hiyo ndio principle yangu ya Maisha Na wala mm huwa siwezi kwenda Ongelea Familia ya Mtu
 
Ya kwao yaache Kama yalivyo..Kama ilipangwa kubumburuka ipo siku yatabumburuka tu.
 
Back
Top Bottom