Nimepiga marufuku utamaduni wa mgeni kushukuru kwa chakula kila baada ya kula

Nimepiga marufuku utamaduni wa mgeni kushukuru kwa chakula kila baada ya kula

kilambimkwidu

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2017
Posts
6,097
Reaction score
7,199
Naomba nikosolewe au kupongezwa kwa utaratibu nilioelekeza nyumbani kwangu kwamba ni marufuku wife kupokea shukrani za mgeni anaeshukuru kwa chakula.

Hii imekua ikitokea hata kwa wageni ambao wanaishi muda mrefu, kwamba kila anapomaliza kula anamuangalia “mama mwenye nyumba” na kumshukuru kwa chakula.

Nimekataza hilo na kuelekeza shemeji yenu wakati wote kutoa elimu kwa upole kwa mgeni atakayeshukuru kuwa hatuna utaratibu huo na asiwe na hofu, ajisikie huru na kwakuwa ni mgeni wetu tunatamani ajione ni sehemu ya familia na anahaki na fursa sawa na wengine tuliopo.

Binafsi naona utamaduni huo ni unaguzi na unachochea madaraja na kufanya mgeni aendelee kujihisi ni mgeni wakati wote na chakula kwake aone kama hisani ambayo hakustahili kupata.

Nafikiri kwanini mgeni huyo asishukuru anapomaliza kuangalia televisheni kipindi anachokipenda, au ashukuru kila asubuhi kwa kupewa chumba cha kulala.

Baadhi ya familia hadi mtoto anashukuru kwa chakula kila anapomaliza kula. Hapana, hilo nimekataza.

(Picha haihusiani)
 

Attachments

  • IMG_0171.jpeg
    IMG_0171.jpeg
    81 KB · Views: 6
Kushukuru ni utaratibu wa kila siku bila kujali ugeni au wewe huwa hushukuru, wanao je?
Nimemshangaa sana huyu ndugu , kwa hiyo mgeni tu ndio asishukuru au hadi watoto wake nao wasishukuru?
Na huyo mgeni anakatazwa asishukuru kwenye kula tu au kila kitu lets say mkimpatia fedha akanunue mahitaji yake mengine nayo hapaswi kushukuru pia?
Nikimsaidia mtu wangu wa karibu akishukuru nitamjibu asante kwa kushukuru basi siwezi kukataa shukrani ya jambo la kweli
 
Nimemshangaa sana huyu ndugu , kwa hiyo mgeni tu ndio asishukuru au hadi watoto wake nao wasishukuru?
Na huyo mgeni anakatazwa asishukuru kwenye kula tu au kila kitu lets say mkimpatia fedha akanunue mahitaji yake mengine nayo hapaswi kushukuru pia?
Nikimsaidia mtu wangu wa karibu akishukuru nitamjibu asante kwa kushukuru basi siwezi kukataa shukrani ya jambo la kweli
Kushukuru ni jambo jema sana na ni vizuri kuwa n utaratibu ndani ya familia iwe kuna ugeni au La.
Inawezekana mleta mada huwa hashukuru kwa lolote.
 
Utaratibu Wa Nyumban Kwangu Watoto Wakimaliza Kula Kwanza Kumshukur Allah Aliewaruzuqu Kisha Mpishi Na Mtafutaji Wa Chakula, Hainuki Mtoto Kwenye Mkao Bila Kushukur, Pia Wakipewa Kitu Ima Nimetoa Mimi Au Mtu Yeyote Lazma Kushukur Tena Mama Yao Kawaongezea Na Hii (Allah Akuzidishie Zaidi Ya Ulichotoa au Allah Akupe Badali Ya Ulichotoa) So Akija Mgeni Ataona Aibu Yeye Mwenyew Kutoshukuru Ikiwa Watoto Ambao Ni Wajibu Wangu Kuwahudumia Wanashukuru, Pia Ni Katika Tabia Mzuri Na Utamaduni Wa Kitanzania Hata Wew Mwenywe Umsaidie Mtu Kitu Halaf Ageuke Kimy Kimya Bila Hata Kusema Ahsante Kuna Hali Utajihisi.
 
Kushukuru (kwa jambo lolote zuri sio kula tu) ni utamaduni wa mtu yeyote mstaarabu hasa kwa sisi watanzania.
Ndio maana hata ukienda dukani ukatoa pesa ukapewa bidhaa bado tunasema ahsante licha ya kwamba umeingia gharama.
Shukrani ni suala la mindset zaid na ndio maana tunafunsishwa kushukuru kwa kila jambo.
 
Naomba nikosolewe au kupongezwa kwa utaratibu nilioelekeza nyumbani kwangu kwamba ni marufuku wife kupokea shukrani za mgeni anaeshukuru kwa chakula.

Hii imekua ikitokea hata kwa wageni ambao wanaishi muda mrefu, kwamba kila anapomaliza kula anamuangalia “mama mwenye nyumba” na kumshukuru kwa chakula.

Nimekataza hilo na kuelekeza shemeji yenu wakati wote kutoa elimu kwa upole kwa mgeni atakayeshukuru kuwa hatuna utaratibu huo na asiwe na hofu, ajisikie huru na kwakuwa ni mgeni wetu tunatamani ajione ni sehemu ya familia na anahaki na fursa sawa na wengine tuliopo.

Binafsi naona utamaduni huo ni unaguzi na unachochea madaraja na kufanya mgeni aendelee kujihisi ni mgeni wakati wote na chakula kwake aone kama hisani ambayo hakustahili kupata.

Nafikiri kwanini mgeni huyo asishukuru anapomaliza kuangalia televisheni kipindi anachokipenda, au ashukuru kila asubuhi kwa kupewa chumba cha kulala.

Baadhi ya familia hadi mtoto anashukuru kwa chakula kila anapomaliza kula. Hapana, hilo nimekataza.

(Picha haihusiani)
Sijajua kwa wengine ila katika makuzi yangu umekuwa ni utaratibu wa kushukuru baada ya chakula kwa watoto wote , hivyo shukrani sio adhabu ni tendo jema la kutambua mchango na upendo

Ndio maana mpaka kesho chakula natafuta mwenyewe kwa jasho langu lakini namshukuru Mungu kwa riziki na mpishi kwa kukiandaa
 
Naomba nikosolewe au kupongezwa kwa utaratibu nilioelekeza nyumbani kwangu kwamba ni marufuku wife kupokea shukrani za mgeni anaeshukuru kwa chakula.

Hii imekua ikitokea hata kwa wageni ambao wanaishi muda mrefu, kwamba kila anapomaliza kula anamuangalia “mama mwenye nyumba” na kumshukuru kwa chakula.

Nimekataza hilo na kuelekeza shemeji yenu wakati wote kutoa elimu kwa upole kwa mgeni atakayeshukuru kuwa hatuna utaratibu huo na asiwe na hofu, ajisikie huru na kwakuwa ni mgeni wetu tunatamani ajione ni sehemu ya familia na anahaki na fursa sawa na wengine tuliopo.

Binafsi naona utamaduni huo ni unaguzi na unachochea madaraja na kufanya mgeni aendelee kujihisi ni mgeni wakati wote na chakula kwake aone kama hisani ambayo hakustahili kupata.

Nafikiri kwanini mgeni huyo asishukuru anapomaliza kuangalia televisheni kipindi anachokipenda, au ashukuru kila asubuhi kwa kupewa chumba cha kulala.

Baadhi ya familia hadi mtoto anashukuru kwa chakula kila anapomaliza kula. Hapana, hilo nimekataza.

(Picha haihusiani)
Mkuu shukran ni Dua we hutaki ?
We ni mchoyo ndo maana hutak asante
Alafu waambie mwenyewe wageni sio kumsukumia mke wako aseme
 
Suala la kushukuru siyo la mgeni wala la kwenye chakula tu hata wewe unatakiwa kuwafundisha watoto wako kushukuru kila wema wanaofanyiwa, hata wakielekezwa njia waseme asante, hata akipewa zawadi aseme asante, hata wife wako akikuandalia nguo za kuvaa sema asante.

Watoto waliofundishwa kushukuru hata barabarani akikuomba kuovertake ukampisha akapita akifika mbele atawasha Hazard lights kama ishara ya kushukuru.

Moyo wa mtu asie na shukurani hauna chochote isipokua kiburi.
 
Naomba nikosolewe au kupongezwa kwa utaratibu nilioelekeza nyumbani kwangu kwamba ni marufuku wife kupokea shukrani za mgeni anaeshukuru kwa chakula.

Hii imekua ikitokea hata kwa wageni ambao wanaishi muda mrefu, kwamba kila anapomaliza kula anamuangalia “mama mwenye nyumba” na kumshukuru kwa chakula.

Nimekataza hilo na kuelekeza shemeji yenu wakati wote kutoa elimu kwa upole kwa mgeni atakayeshukuru kuwa hatuna utaratibu huo na asiwe na hofu, ajisikie huru na kwakuwa ni mgeni wetu tunatamani ajione ni sehemu ya familia na anahaki na fursa sawa na wengine tuliopo.

Binafsi naona utamaduni huo ni unaguzi na unachochea madaraja na kufanya mgeni aendelee kujihisi ni mgeni wakati wote na chakula kwake aone kama hisani ambayo hakustahili kupata.

Nafikiri kwanini mgeni huyo asishukuru anapomaliza kuangalia televisheni kipindi anachokipenda, au ashukuru kila asubuhi kwa kupewa chumba cha kulala.

Baadhi ya familia hadi mtoto anashukuru kwa chakula kila anapomaliza kula. Hapana, hilo nimekataza.

(Picha haihusiani)
Icho chakula bila shaka anayekileta ni huyo Mama sio wewe
 
Back
Top Bottom