Nimepoteza Kaka Yangu Niliyekuwa Namfuatia

Nimepoteza Kaka Yangu Niliyekuwa Namfuatia

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
 
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baaya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Mfichie aibu yake, sio kuitangazia Dunia. Huenda ni madhara ya vita. Vita vina mambo mengi!
 
Pole sana, mwendo ameumaliza kishujaa..... apumzike kwa amani.
 
And don't cry to your brothers funeral

He died inside longtime ago but you didn't care

...
Wengi wetu hatujui kuwa watu wanaofanya vitu visivyokawaida km ulevi kupindukia nk sio kwamba wana furaha ila wana mengi moyoni yanawatesa na hawana mtu wa kumkumbatia walie machozi
 
ila wanajf, dah

anyways kuna mtu huwa anasema kifo huwa kinatafuta sababu tu kikifika.
 
Ungekausha tu mkuu...au ungesema tu nimefiwa na Kaka yangu....wewe una mapungufu mengi mno Kaka yako anajua sasa ashakufa hawezi kukutangaza kama hivi...wewe ushamwanika hii siyo fair game.....Tupo huru na vinywa vyetu ila tujaribu kusitiriana wapendwa🙏🏽 RIP bro
 
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Pole sana
 
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Pole mno.
Ila kuhusiana na pombe ukiijua akili ya binadamu vizuri, yaani nature of our brain pombe, vileo, kamari, aina yoyote Ile ya drugs hairusiwi Mana mtu akishaonja kuacha ni kazi mno yaani mno ni sawa na masikini kuwa tajiri inabidi aamue from inside na awe na hasira mno otherwise tegemea Teja milele
 
Mfichie aibu yake, sio kuitangazia Dunia. Huenda ni madhara ya vita. Vita vina mambo mengi!
Ninakubaliana na wewe kumfichia aibu yake, lakini sidhani kama kuna anyemfahamu personally hapa, kwa hiyo hii ni habari kwa watu wote wanaoweza kupata cha kujifunza kuhusu ndugu wenye tabia hizo. Elewa kuwa ni ndugu yangu toka nitoke; kwa hiyo usidhani ninaandika kwa furaha.

Tabia ya pombe haikutokea vitani; aliporudi alitulia na kujenga familia yake vizuri; huu unywaji wa hovyo ni tabia ya aliyejenga ukubwani.
 
Pole sana pengine usingeweza kusaidia hata kama ungekuwepo
Maana hata huko walikuwepo watu walioshauri usijalaumu muombee apate pumziko jema maana ameona mengi mno yaliyomfanya aingie kwenye pombe ili awese kuyasahau
 
Back
Top Bottom