Nimepoteza Kaka Yangu Niliyekuwa Namfuatia

Nimepoteza Kaka Yangu Niliyekuwa Namfuatia

And don't cry to your brothers funeral

He died inside longtime ago but you didn't care

...
Wengi wetu hatujui kuwa watu wanaofanya vitu visivyokawaida km ulevi kupindukia nk sio kwamba wana furaha ila wana mengi moyoni yanawatesa na hawana mtu wa kumkumbatia walie machozi
What to do ? Maana mdogo angu pia anasumbuliwa na addiction ya pombe na yeye Pombe na yeye na POMBE balaa. Nimeongea wee tumeongea wee lakini habadirik mpaka tumechoka...
 
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Pole mkuu, usijione mwenye hatia, huenda hata ungekuwa karibu isingesaidia. Pole sana.sana.
 
What to do ? Maana mdogo angu pia anasumbuliwa na addiction ya pombe na yeye Pombe na yeye na POMBE balaa. Nimeongea wee tumeongea wee lakini habadirik mpaka tumechoka...
Siyo suala la kuongea tu.

Kuweni karibu nae, mtafutieni kitu cha kufanya awe bize.

Msimkaripie wala kumdharau, mtu husikiliza watu wanaomheshimu na kumjali.
 
Siyo suala la kuongea tu.

Kuweni karibu nae, mtafutieni kitu cha kufanya awe bize.

Msimkaripie wala kumdharau, mtu husikiliza watu wanaomheshimu na kumjali.
Ni mtaratibu Sanaa anakunywa kwa Siri then akirud home analala Kama amekufa..

Tuna muheshimu na anakazi yake nzurii TU tatizo Ni Hilo ulevi ulio pitilizaa balaa

Sijui kalogwa na Nani na Nini maana mpaka naogopa Nini kimemkumbaa Ni Maumivu kwa kweli..
 
Ninakubaliana na wewe kumfichia aibu yake, lakini sidhani kama kuna anyemfahamu personally hapa, kwa hiyo hii ni habari kwa watu wote wanaoweza kupata cha kujifunza kuhusu ndugu wenye tabia hizo. Elewa kuwa ni ndugu yangu toka nitoke; kwa hiyo usidhani ninaandika kwa furaha.

Tabia ya pombe haikutokea vitani; aliporudi alitulia na kujenga familia yake vizuri; huu unywaji wa hovyo ni tabia ya aliyejenga ukubwani.
Alipoteza dhumuni kuu la maisha!

Kuna eneo alilipigania sana likamsaliti akaona maisha hayana maana kabisa!!

Wapo wengi sana!
 
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Poleee Sanaa Mkuuu
Shikmooo Mkuu

Mungu ampe Pumziko jema

Kikubwa tumuombe kwa Mola wetu
 
Unazani Nini kifanyike maana mdogo angu pia anapitia haya mapito anakunywa Sana nimeongea wee wazazi wameongea wee hasikilizi what to do..?? Nipo kwenye dillema for sure..
Well what he needs is someone who understands anachopitia. Clearly he saw lot of things, lakini pia ile attachment aliyokuwanayo jeshini, uraiani haipati ( ile brotherhood ), is why anaona hamumuelewi, or ana feel utumishi wake katika jeshi haudhaminiki despite ya yale aliyo yafanya serikali imemtupa

Let him determine what is he comfortable talking about, and don’t push.
Mchukue nenda nae mbali somewhere hajswahi kwenda, enjoy nae , mjengee mazingira ya kufunguka , in no time ataongea.

Remind him that hayuko peke ake, na wengine kama yeye au wasio kama yeye wana stories they can share about their readjustment. Or kama mna ndugu wa karibu au rafiki sake ambao wako in service au walitoka huko lakini wako vizuri sasa, unaweza wa involve kwenye hili wakaongea nae
 
Well what he needs is someone who understands anachopitia. Clearly he saw lot of things, lakini pia ile attachment aliyokuwanayo jeshini, uraiani haipati ( ile brotherhood ), is why anaona hamumuelewi, or ana feel utumishi wake katika jeshi haudhaminiki despite ya yale aliyo yafanya serikali imemtupa

Let him determine what is he comfortable talking about, and don’t push.
Mchukue nenda nae mbali somewhere hajswahi kwenda, enjoy nae , mjengee mazingira ya kufunguka , in no time ataongea.

Remind him that hayuko peke ake, na wengine kama yeye au wasio kama yeye wana stories they can share about their readjustment. Or kama mna ndugu wa karibu au rafiki sake ambao wako in service au walitoka huko lakini wako vizuri sasa, unaweza wa involve kwenye hili wakaongea nae
Nafanyia kazi huu ushauri ntakupa mrejesho..
 
Ni mtaratibu Sanaa anakunywa kwa Siri then akirud home analala Kama amekufa..

Tuna muheshimu na anakazi yake nzurii TU tatizo Ni Hilo ulevi ulio pitilizaa balaa

Sijui kalogwa na Nani na Nini maana mpaka naogopa Nini kimemkumbaa Ni Maumivu kwa kweli..
Ili asinywe kwa siri, msitumie lugha kali kwny kumshauri, ikibidi msindikize kwny kunywa, ahisi mko pamoja.

Siku moja mchukue kamnunulie pombe, hapo ndio ataanza kukuelewa.
 
Back
Top Bottom