Nimepoteza Kaka Yangu Niliyekuwa Namfuatia

Nimepoteza Kaka Yangu Niliyekuwa Namfuatia

And don't cry to your brothers funeral

He died inside longtime ago but you didn't care

...
Wengi wetu hatujui kuwa watu wanaofanya vitu visivyokawaida km ulevi kupindukia nk sio kwamba wana furaha ila wana mengi moyoni yanawatesa na hawana mtu wa kumkumbatia walie machozi
Ikishakuwa addiction hata familia nzima ikukumbatie ni kazi bure tu. Ndio maana kila kitu kinagakiwa kiwe kwa kiasi, kula, kunywa nk viwe kwa kiasi. Anything excessive is harmful.
 
Somo kubwa hapa halijaelewa kwa wengine. Ni kwamba ukiwa na ndugu mwenye tabia ya ndugu yangu huyo, mwimbie wimbo wa madhara ya pombe bila kuchoka; usimwaje ajiamulie kila kitu freely hata kama ni mtu mzima.

Pole, Binadamu ni vigumu sana kubadilika wakipata addiction kama hiyo. Ukimshauri sana mtagombana. Ni mpaka aamue mwenyewe au apate janga kubwa litalomwamsha.
 
Ungekausha tu mkuu...au ungesema tu nimefiwa na Kaka yangu....wewe una mapungufu mengi mno Kaka yako anajua sasa ashakufa hawezi kukutangaza kama hivi...wewe ushamwanika hii siyo fair game.....Tupo huru na vinywa vyetu ila tujaribu kusitiriana wapendwa🙏🏽 RIP bro
RIP Mpiganaji Mstaafu
 
Alirudi akaenda kulala moja kwa moja; mke wake alikuwa amezowea tabia hiyo ila safari hii inaonekan ilikuwa zaidi.
Hakuna cha zaidi wala pungufu, muda wake ulishafika.

Inna li Llahi wa Inna Ilayhi Rajiun.
 
Ungekausha tu mkuu...au ungesema tu nimefiwa na Kaka yangu....wewe una mapungufu mengi mno Kaka yako anajua sasa ashakufa hawezi kukutangaza kama hivi...wewe ushamwanika hii siyo fair game.....Tupo huru na vinywa vyetu ila tujaribu kusitiriana wapendwa[emoji1431] RIP bro
Mfichie aibu yake, sio kuitangazia Dunia. Huenda ni madhara ya vita. Vita vina mambo mengi!
Ulevi na tabia mbovu kama hizo sio za kuficha na hayo si mapungufu kwamba binadamu anakuwa hana uwezo wa kuyaacha, lazima ifike mahala watu waambiwe ukweli kuhusu tabia mbovu zinazoharibu maisha na afya.

Ulevi uliopitiliza ni janga baya linalotakiwa kukemewa na sio kufichwa, acheni upuuzi mnaoyakumbatia haya mambo ya kufichaficha tabia za kishenzi ktk jamii.
 
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Pole sana ndugu.....
Mimi nilikuwa mlevi wa kupindukia yaani sichagui pombe iwe za kizungu au kienyeji....hili jambo limeniuma sana....zingatia hatunywi kwa hiari...na kwenye kila "hangover ".....Kuna kiapo cha kuacha pombe.....
 
Ulevi na tabia mbovu kama hizo sio za kuficha na hayo si mapungufu kwamba binadamu anakuwa hana uwezo wa kuyaacha, lazima ifike mahala watu waambiwe ukweli kuhusu tabia mbovu zinazoharibu maisha na afya.

Ulevi uliopitiliza ni janga baya linalotakiwa kukemewa na sio kufichwa, acheni upuuzi mnaoyakumbatia haya mambo ya kufichaficha tabia za kishenzi ktk jamii.
Sawa mkuu
 
Pole brother , ila sijui kama ungeweza kumbadilisha kwa kuwa karibu, zimefika tuu na kila mtu kwa time yake, RIP
 
Ikishakuwa addiction hata familia nzima ikukumbatie ni kazi bure tu. Ndio maana kila kitu kinagakiwa kiwe kwa kiasi, kula, kunywa nk viwe kwa kiasi. Anything excessive is harmful.
Excessive indulgence leads to suffering
 
Nimesikitika sana mkuu kwahiyo wewe ulitaka afe Kwa malaria au agongwe na gari afe?

Kifo ni kifo mkuu. Kifo Cha kujitakia ama Cha aibu ni kunywa Sumu ama kujinyonga.
 
Jana nimepoteza kaka yangu niliyekuwa namfuatia; yeye alikuwa anaishi kijijini ambako ameishi tangu aliporudi vitani mwaka 1980. Alikuwa mtu mzima sana; kinachonisikitisha zaidi ni sababu ya kifo chake.

Alikwenda kunywa pombe za kienyeji na kendelea kunywa kwa siku mbili mfululizo bila kula; aliporudi nyumbani baada ya siku hizo akaenda kulala na hakuamka tena.

Ndugu yangu huyo alikuwa na matatizo sana ya kuhimili pombe kiasi kuwa ukoo wote ulimkatia tamaa; kwa bahati mbaya sana yeye ndiye aliyekuwa amebaki mkubwa peke yake kwenye ukoo huko kijijini, kwa hiyo hakukuwa na mwenye sauti juu yake. Nimeanza kufikiri kuwa huenda mimi ningekuwapo mara kwa mara pale kijijini huenda asingepotoka kufikia kiasi cha kupoteza maisha yake kwa njia ya aibu namna hiyo.

Ukiwa na ndugu mwenye tabia za marehemu kaka yangu, jitahidi uwe unatenga muda wa kumshauri mara kwa mara kuhusu pombe asitumbukie kwenye janga lililotufika sisi.

Kazi ya Mungu haina makosa

Mungu ampumzisha roho yake anakosatahili
Kama alikuwa veteran kwanza kwa niaba ya wengine i thank him for his service to his country. Second veteran wengi waliporudi hawakuwa na support, na pombe ni tatizo la wengi ambao wame experience traumatic events sababu ya vita. Its seems he has several PTSD isi why akakimbilia pombe. No support from gov or baadhi ya wanao mzunguka.
Carry his memory but also it time jamii yetu iache ku ignore mental health issues
 
Kama alikuwa veteran kwanza kwa niaba ya wengine i thank him for his service to his country. Second veteran wengi waliporudi hawakuwa na support, na pombe ni tatizo la wengi ambao wame experience traumatic events sababu ya vita. Its seems he has several PTSD isi why akakimbilia pombe. No support from gov or baadhi ya wanao mzunguka.
Carry his memory but also it time jamii yetu iache ku ignore mental health issues
Unazani Nini kifanyike maana mdogo angu pia anapitia haya mapito anakunywa Sana nimeongea wee wazazi wameongea wee hasikilizi what to do..?? Nipo kwenye dillema for sure..
 
Back
Top Bottom