Nimerepair trucks za DAF, Scania, MAN na Benz upande wa umeme lakini MAN tuwape mauwa yao, mpangilio wa mfumo wao wa umeme ni rafiki sana

Aaah okay kuna jamaa niliwahi kuona pale TBL mwanza wana repair BENZ za hapo kwahiyo wanakuwa ni kampuni kabisa ambayo mafundi wake wana utaalamu nazo?
GGM (Geita Gold Mine) wana Benz fln hv nadhan ni Actros ile, ila hadi leo wakitaka kurepair wanaletwa majamaa kutoka CFAO Motors coz ndo dealer wa benz hapa TZ.

So utaona mara nyingi kama sio dealer basi ni wataalam walospecialize na benz, na hao CFAO huwa wana ratiba ya kutoa mafunzo kwa mafundi mbalimbali almost kila mwaka
 
Okay nawafahamu CFAO motors.

Nawakubali sana hao Mercedes Benz huwa naangalia mara kwa mara schematic diagrams ya umeme ya gari zao.

Nilitamani sana siku moja kuja kufanyia kazi, ila ndiyo hivyo tena
 
Mkuu Scania series ipi au generation ipi imekaa rough kwenye wire.

Hiyo Scania kuanzia Series 3&4 ndio truck ambayo fundi yoyote hapa Tanzania anajifunzia ufundi na mafundi wamejaa hata uende Namtumbo,Namanyele,Sikonge,Nyakanazi hazijawahi kuwa pasua kichwa kama Daf au Iveco Stralis
 
Regional mkuu.
Kama unataka Rigid truck(Kipisi) Chukua Scania 94D au P94 zenye 310hp.

Kama unataka tractor truck chukua Scania used za South G410 & 114L au R420 hizi zote ni 6*4 na Man Diesel trucks kwa route za Regional. Scania Ex Uk na Ireland kwa bajeti ya kawaida zinakuwa na high mileage na nyingi zina axle configuration ya 4*2 ambapo utatakiwa uje ufanye modification upate 6*2 uongeze axle moja ambayo ni dead axle au tag axle ili ubebe mzigo vizuri
 
Na pia hzohzo kupiga shoti gari nzima sio kitu cha ajabu, umesahau hilo
 
Scania tangu zamani wamekuwa wakitoa training kwa madereva na mafundi.

Scania kama Toyota spea kibao mafundi mpaka chini ya msufi/mwembe
Sikatai scania ni kama toyota kwa magari makubwa.

Ila point hapa ni organization ya wiring.

Na pia same as toyota kama ni fundi 'cutting' basi kila waya utachubuliwa na kukatwa, ndipo hapo shoti zinapotokea

Ninachowapa heko scania ni hii SDP3 pekee, kwa scania inayosupport SDP3 wiring zake unaelekezwa humohumo kwenye hio diagnosis program, ila kuhusu organization ya wiring scania bado sana, kafungue MAN uone wiring zilivyopangwa chief.

Ni kama mainjinia wa toyota walivyo disassemble Tesla model 3 wakabaki wanatikisa vichwa tu na kusema Toyota kufikia hio level ya kuorganize wiring ni miaka 10 baadae
 
Asante kwa ushauri mzuri, ila MAN Diesel trucks naona kama bongo hawajazichangamkia sana.
 
Asante kwa ushauri mzuri, ila MAN Diesel trucks naona kama bongo hawajazichangamkia sana.
Saizi zimeongezeka mkuu na dealer wake Tanzania yupo Tabata Mobikey Trucks, ila kuna spare utozipata kwa wengine mpaka urudi pale kwao.

Kama hujali maneno ya watu Scania ndio truck ambayo haina complication na sawa na Toyota, Spare kila kona ukitaka Used zimejaa Tabata,Temeke Mwisho na Ilala kuna madealer kibao na maduka ya Amana Spare parts kila mikoa wanauza spare zake. Man Diesel ni truck imara miaka michache mbele spare zitazagaa ila bei haitokuwa sawa na Scania
 
Nasikia hata wanaojenga SGR wanatumia sana MAN, kama wakimaliza wakaziuza humuhumu TZ inaweza kuwa entry point nzr kwa mtu mwenye mtaji
 
Nasikia hata wanaojenga SGR wanatumia sana MAN, kama wakimaliza wakaziuza humuhumu TZ inaweza kuwa entry point nzr kwa mtu mwenye mtaji
Ndio, Mo alinunua horse kibao za mtumba za Man, Dollow Boy anazo kibao zinavuta trailer ya Tipper za makaa ya mawe. Wengine walivuta used na mpya hapo Mobikey na nyingine used zimeuzwa na Lawexport na Abbas Truck UK
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…