Nimerudi kazini sijamkuta mke wangu, nauliza majirani naambiwa ameondoka kwenda kwao

Nimerudi kazini sijamkuta mke wangu, nauliza majirani naambiwa ameondoka kwenda kwao

Aisee pole sna mkuu
Ni bora kukataliwa kuliko kukimbiwa maaana utavaki na maswali 100 bila majibu
Why , how , when , what
Mara utaanza kuwaza au una kibamia hakimkuni vzur kafuata muhogo
Yaan usiombe yakukute
 
Bro tuambie ukweli, jibu maswali haya:
1. Una hali ngumu kimaisha? (Kama ndio, Usijali ni mapito)
2. Ana kitu moyoni hakijamtoka? Labda mligombana
3. Wewe mwenye tabia zako ni zipi?
Ushauri: mtafute huyo mpangaji aliyepokea simu ya mkeo na kusema anakaribia kwao uongee naye vizuri....kwa vyovyote vile atakuwa kamwambia kwanini kaondoka. Wanawake hawana siri atakwambia tu....kama aliweza kukwambia hivyo basi kuna vingine anaficha. Ongea vizuri na mpangaji huyo.

Ikifika masaa 24 katoe taarifa polisi. Halafu kausha hao ndugu zake wasikusumbue-usipokee simu zao.
 
Nafanya kazi mbali na ninapoishi kwa hiyo huwa ninalala huko ninakofanyia kazi ambako nimepanga chumba cha dharura.

Siku ya jtano wiki hii niliagana na mke wangu kuwa naelekea kazini na nitarudi siku ya alhamisi au ijumaa akaitikia na tukaagana vizuri.

Mshtuko wa moyo nilioupata ni pale nilipojisikia kurudi siku ya pili yake yaani Alhamisi baada ya kugonga mlango kwa muda bila majibu nikaamua niulize jirani aliko mke wangu, najibiwa jana ulipoondoka mkeo nae kasafiri ila funguo hizi hapa. Nilihisi kuishiwa nguvu lakini nilijikaza nikachukua ufunguo taratibu nikaingia ndani kiukweli sijaamini macho yangu hakukua na kitu chake hata kimoja zaidi ya kuniachia picha za ndoa.

Nimeumia sana na huo ulikuwa mwisho wa kupata usingizi hadi sasa. Nimempigia simu lakini haipatkani, ndugu zake hawajui yuko wapi ila leo hii Jumamosi mpangaji mmoja kanionea huruma kaniambia aliongea na mke wangu siku ya Alhamisi jioni na alimfahamisha kuwa anakaribia kufika kwao Chamwino Dodoma akitokea kwetu Mtwara.

Lakini kwao nikiuliza naambiwa haonekani na simu hapatikani, sijui cha kufanya kwanini mke wangu wa ndoa lakini amenitoroka. Naombeni mnishauri nini nifanye kwa kuwa suala hili limevuruga kichwa changu.

Mara ya mwisho kuwasiliana nae ilikuwa jioni Alhamisi kwa kum SMS kupitia private Facebook nikamuuliza uko wapi? Akanijibu kwa kifupi "my lovely husband ".Mpaka sasa simpati kwa simu.
Fuatilia tu kama Yuko salama. Mengine hayakuhusu tafuta pesa,tafuta pesa tafuta pesa tafuta pesàaaaaa
 
Kama ameamua kuondok bila sababu wew endelea na mambo yako atarudi mwenyewe vilevile kwasab nyie watu wazim bana kwann muanze kuchoshana [emoji124]
 
Bro tuambie ukweli, jibu maswali haya:
1. Una hali ngumu kimaisha? (Kama ndio, Usijali ni mapito)
2. Ana kitu moyoni hakijamtoka? Labda mligombana
3. Wewe mwenye tabia zako ni zipi?
Ushauri: mtafute huyo mpangaji aliyepokea simu ya mkeo na kusema anakaribia kwao uongee naye vizuri....kwa vyovyote vile atakuwa kamwambia kwanini kaondoka. Wanawake hawana siri atakwambia tu....kama aliweza kukwambia hivyo basi kuna vingine anaficha. Ongea vizuri na mpangaji huyo.

Ikifika masaa 24 katoe taarifa polisi. Halafu kausha hao ndugu zake wasikusumbue-usipokee simu zao.
Hali yangu kimaisha ni kawaida kwa kuwa nina kila chakula kinachohitajika nyumbani lakini pia huwa ninanunua samaki wanakuwepo kwa friji hadi anaondoka walikuwepo. Labda ana kitu moyoni lakini si angesema baada ya kufika kwao?
 
Hali yangu kimaisha ni kawaida kwa kuwa nina kila chakula kinachohitajika nyumbani lakini pia huwa ninanunua samaki wanakuwepo kwa friji hadi anaondoka walikuwepo. Labda ana kitu moyoni lakini si angesema baada ya kufika kwao?
Pole brother
Umeprove kafika kwao?
Kama ndio wewe kausha kimyaa
Inaonekana unampenda sana mkeo ila ndio hivyo kasepa kimya kimya. Piga kazi, tuliza nafsi.
 
Mkuuu pole ila ukiona hivi huyo co chaguo la Mungu.....angekuua bora kaondoka yeye...
 
Pesa niliacha na hakuchukua hata sent yangu.
Mimi pia niligusia suala la pesa za matumizi kwenye comment yangu,napesa uliacha,kiufupi siri kubwa unayo wewe mwenyewe.kuna mlolongo wa mambo ulikuwa unahesabiwa bila wewe kujijua.
 
Nenda karipot polisi ili lolote baya likimkuta huko usijekuwa suspect
 
Toa tarifa polisi za kupotea mkeo kisha kaa kimya tuliza akili ninaimani 65% ndugu zake wanafaham alipo wakiendelea kuliza wambie swala liko pplisi wao ndo wsnalifanyia kazi, endelea na uchunguzi kujua tatizo ni nini mpaka aondoke
 
Back
Top Bottom