Nimeshafanya Service Bajaji yangu nataka kuondoka kwenda Mwanza na abiria wawili

400km inaweza, kila baada ya 100km kituo cha dakika 15-20, mwendo 70km per hour
 
Uza hizo gari za CC kubwa nunua ist maisha yaendelee...kwa usafiri wa bajaji andika wosia kabisa...maana huko barabarani wewe ndio utakuwa mnyonge kila mmoja atakuwa anakuletea usoni wewe hivyo lazima wakuokote mtaroni ama wakusagie kwenye bajaji humo humo.
 
Mh hata usitishwe na yeyoote tembea tu ,ukifik dodoma pumzika ,kesho yake ulale igunga siku itakayofuata ni zooo so waache waongo hao ,nimewahi kutoka na bajaj from dsm to misoma tena bila wasiwsmasi yaani ,ukiwa na maswali njoo pm,chuma mwaka wa 4 sasa inapiga kazi mkendo
 
Bajaji inahitaji kupumzika kila baada ya kilometa kadhaa ili kupooza injini hivyo itaongeza muda wa kufika.

Bajaji haina utulivu barabarani hivyo itakufanya kuyumbayumba ovyo na kuwa na hatari ya kupata ajali.

Utachoka sana kutokana na usafiri wa bajaji kukaosa utulivu.

Haina uwezo mkubwa wa kupanda milima mikubwa kutokana na udogo wa injini hivyo itakupelekea matatizo njiani.

Uwezekano wa kupata break down ni mkubwa sana.

Sikushauri utumie hiyo bajaji kama unataka kuipeleka Mwanza tafuta usafiri wa malori ya mizigo uipakie humo na wewe utangulie na private car ama upande bus.
 
Bajaji haijawa designed kwa safari ndefu! Ipakie kwenye magari ya mizigo yaendayo mwanza kwa sababu hizi barabara zetu ni HATARI kwa usafiri wa bajaji sana sana usiku usijaribu kamwe MAISHA MAFUPI! LIVE LIFE TO THE FULLEST! Cheaper alternative to get you to mwanza nyie watatu ni kupanda basi !
 
😆😆😂 Yaan mpaka ukifika chalinze izo nauli za abiria wako zitakuwa zimeishiq mikononi mwa trafiki
 
Chizi maharifa una vitu vingi sana naiga hizo copy zako Ila sio ya kwenda na bajaji Mwanza
 
Wadau mbona kama mnanichanganya?jamaa wawili wanasema wameshawah enda tena mmoja alienda mpaka Musoma. Mi najua nikiisimamia hii bajaji nikakanyaga accerator mpka mwisho.kitu lazim kinyooke. Tena nataka niendeshe mwenyewe nimsipe bwana mdogo.maana hana uzoef.
 
Chai..
Huwezi kosa mafuta kama gari unazo..
Huo upepo barabarani na hako ka guta hata moro itachukua siku nzima
 
LAzima mgongwe na simba pale mikumi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…