KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 8,589
- 16,936
Nikiwa dukani kwangu napitia mahesabu ya mapato na matumizi ya wiki iliyopita, akaja mteja anataka madawa fulani, madawa hayo ni slow moving items hivyo huwa yanakaa store, hayapangwi dukani.
Basi nikaona si mbaya huyo mteja akiwa anahudumiwa (akisubiri dawa zake) aje ofisini kwangu anywe walau kikombe cha kahawa.
Mdada akaja ofisini, nikamwambia tea girl amwandalie kahawa mgeni. Baada ya muda mfupi akaletewa kahawa na story zikaendelea.
Tukawa tunaongea mengi, na akaniambia anauhitaji wa kazi kwani kasoma IT.
Basi kwenye story akanijulisha kuwa dawa anazituma Karatu, na ameagizwa azitume kwa basi la Dar Express. Akasema yeye hajui ofisi zilipo, mimi nikamwambia naijua ofisi yao ya Kisutu.
Akaniuliza kama Shekilango wana ofisi, nikamwambia sina uhakika, ila kwanini usicheki kwenye Google Map?
Nikapigwa na butwaa aliponiambia hajui kutumia Google Map. Yaani na degree yake ya IT hajui kutumia app hiyo muhimu? Nikajiuliza sasa nikimchukua huyu, atakuwa amekuja kujifunza kazi au kufanya kazi?
Anasema amesoma visual basic, java, na C++, kasoma networking na troubleshooting ahh, hamu ya kuendelea kumsikiliza ikakata kabisa.
Mzigo wake ulipokuwa tayari, nikamuaga na.kumuongezea 10,000 ya nauli.
Basi nikaona si mbaya huyo mteja akiwa anahudumiwa (akisubiri dawa zake) aje ofisini kwangu anywe walau kikombe cha kahawa.
Mdada akaja ofisini, nikamwambia tea girl amwandalie kahawa mgeni. Baada ya muda mfupi akaletewa kahawa na story zikaendelea.
Tukawa tunaongea mengi, na akaniambia anauhitaji wa kazi kwani kasoma IT.
Basi kwenye story akanijulisha kuwa dawa anazituma Karatu, na ameagizwa azitume kwa basi la Dar Express. Akasema yeye hajui ofisi zilipo, mimi nikamwambia naijua ofisi yao ya Kisutu.
Akaniuliza kama Shekilango wana ofisi, nikamwambia sina uhakika, ila kwanini usicheki kwenye Google Map?
Nikapigwa na butwaa aliponiambia hajui kutumia Google Map. Yaani na degree yake ya IT hajui kutumia app hiyo muhimu? Nikajiuliza sasa nikimchukua huyu, atakuwa amekuja kujifunza kazi au kufanya kazi?
Anasema amesoma visual basic, java, na C++, kasoma networking na troubleshooting ahh, hamu ya kuendelea kumsikiliza ikakata kabisa.
Mzigo wake ulipokuwa tayari, nikamuaga na.kumuongezea 10,000 ya nauli.