Nimetapeliwa na mtu aliyejitambulisha kama afisa Mikopo Mo Dewji Foundation

Mlianzaje mawasiliano na huyo jamaa aiseee!
Bora kama kukopa utumie app zinazotoa mikopo ndugu yangu sasa jamaa kashakuliza bana.
 
Tanzania Ina mabumunda wengi sana,wewe unataka mkopo alafu unaambowa tuma pesa,
na kila siku mnaambiwa matapeli yanatumia jina la Mo Foundetion na Jokate lakini nyie kwa ujinga wenu hamkomi tu.
Tz kuna mambugila wengi

Ova
 
Mwenyewe kaanzisha uzi kwa kujiamini masikiniπŸ™†β€β™€οΈπŸ™†β€β™€οΈ
 
Wewe utakuwa muha aliekuja juzi mjiniπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Wewe umemtumia hela mtu namba binafsi kabisa. Kila kitu hatua
 
POLE SANA.....
kwa ushauri,watu wengi tunakopa mtandaoni,kwahiyo kabla hujataka kukopa jaribu kuuliza watu wako wa karibu kuhusu kampuni unayotaka kukopa huenda utapata taarifa sahihi za kampuni au utapewa taarifa ya kampuni nyingine inayoweza kukufaa
hao matapeli wapo weengi sahivi,kuna wa nandy supermarket,kuna wale wa ajira lipia hera ya form nk
pole sana mkuu
 
Mkemia umeshindwa kung'amua kuwa chemical zilikuwa hazibalance???

Ila uzuri una namba ya Mo, mtwangie tena umwambie Bw. Khamisi kaingia chaka na pesa yako ya kufungulia account ya mkopo.
Hahaha, ila mna majibu mazuri, nafurahi
 
Asante ndg
 
Ukizaliwa tz we tayari ni kichekesho ndo mtoa mada sasa
 
Juzi kati nimetoka kumuokoa dada mmoja alitaka kupigwa 30,000, eti kapata bwana toka dubai, anataka amtumie 1,000,000 afanye biashara,wamekutana facebook

Sasa alitaka kupigwa kwa stahili ya kwamba atume hiyo hela ili afunguliwe account ya simu ambayo inaruhusu kupokea dola,nikamwambia mbona siku hizi mambo ya kutumia hela simpo

Jamaa ambaye yupo dubai,kamlengesha kwa jamaa wa bongo kuwa huyo ndio atamfungulia madam account ΓΏa simu ambayo inapokea dola,ili ikiwa tayar ndio tajir atume hela.

Nikamwambia madam ebu nipe namba ya huyo mbongo,nikahojiana nae pale akasema inatakiwa 30,000 afungue account,nikamwambia kwanini usimfungulie kabisa halafu utakata hela yako juu kwa juu,shughuli ikaishia hapo

Halafu nikamwambia madam acha ujinga,yaan mwamba umejuana juzi tu hlf akutumie milioni moja kirahisi rahisi

Sijui warembo wangapi huwa wanatapeliwa

Ngoja nami nibuni mbinu niwapate wajinga wanipe hela mingi
 
Kuna Joketi mikopo online pia πŸ˜‚
 
Na mkomeee ...

Inazungumzwa humu kila siku ...

Ukishaona unaambiwa utume hela ndo upate hela ujue tayali ni utapeli..

Yaani hata akili ya kuzaliwa tu huna..

Tuma tena ..

Pole sana Mkemia ...
Ngoja ukutwe wewe hata pole hupati.
 
Bora hata wewe umetapeliwa kidogo jipongeze......
Kuna mdada katapeliwa mil 10, yani mil 10 kavu ni huzuni sahivi hadi amekonda.

Aliunganishwa na mtu anaemuamini kuna mikopo riba kitonga atapewa mil 50 hivyo atoe mil 10 ili apewe, kakopa kakopa hukoo zikafika 10 akawapa wakopeshaji.....kifuatacho ITV sasa.....🀦
 
Noma sana, nimekutana na Add Instagram ya Mo foundation mikopo πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… nikaona ngoja nije JF kwa waungwana nijue kama ni kweli au sio kweli, kwa hiking nilichokiona hapa ndio nilichokiona kwenye lile tangazoπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…